Friday, February 17, 2017

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje akutana na Balozi Mteule wa Oman

Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Susan Kolimba akizungumza na Balozi Mteule wa Oman nchini, Mhe. Ali Abdullah Al Mahruqi alipomtembelea Wizarani leo, Jijini Dar es Salaam. Mazungumzo yao yalijikita katika masuala ya ushirikiano na juu ya ukamilishaji wa makubaliano ya kibiashara na uwekezaji ili kuweza kunufaika na ushirikiano wa kidiplomasia ambao umekuwa ukizidi kuimarika baina ya mataifa hayo mawili.
Mhe. Al Mahruqi akimweleza Naibu Waziri mipango ya kiutendaji ya Ubalozi wa Oman nchini na jinsi Serikali yake ilivyojidhatiti katika kuhakikisha mahusiano yaliyopo yataelekeza nguvu zaidi katika kusimamia sekta zinazogusa kukuza uchumi wa wananchi.
Mhe. Al Mahruqi akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika ofisi za Wizara, kulia ni Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Abdallah Kilima.
Picha ya pamoja wakiagana mara baada ya mazungumzo.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.