Friday, February 24, 2017

Katibu Mkuu wa Mambo ya Nje azungumza na Balozi wa Sweden nchini

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Aziz Mlima akizungumza na Balozi wa Sweden hapa nchini, Mhe. Katarina Rangnitt. Katika mazungumzo yao walijadili namna ya kuendelea kuimarisha ushirikiano kati ya Tanzania na Sweden. Mazungumzo hayo yalifanyika Wizarani tarehe 24 Februari, 2017
Balozi Rangnitt nae akimweleza jambo Balozi Mlima wakati wa mazungumzo yao
Mazungumzo yakiendelea. Kulia ni Bi. Tunsume Mwangolombe, Afisa Mambo ya Nje na kushoto ni Afisa kutoka Ubalozi wa Sweden.
Balozi Mlima akimpatia Balozi Rangnitt kadi yake ya mawasiliano ikiwa na  anuani mpya za Dodoma.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.