Thursday, July 21, 2022

KATIBU MKUU BALOZI SOKOINE AKUTANA NA MABALOZI PUNDE BAADA YA KUAPISHWA


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine (katikati) Mhe. Balozi Dkt. Suleiman Haji Suleiman (kulia) na Mhe. Luteni Jenerali Mathew Edward Mkingule Balozi wa Tanzania nchini Zambia (kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja 

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine tarehe 20/07/2022 alikutana na kufanya mazungumzo na Mhe. Balozi Dkt. Suleiman Haji Suleiman na Mhe. Luteni Jenerali Mathew Edward Mkingule Balozi wa Tanzania nchini Zambia katika ofisi za Wizara jijini Dodoma.

Balozi Sokoine katika mazungumzo hayo yaliyofanyika muda mfupi baada ya viongozi hao kuapa kutumikia nyadhifa hizo katika hafla iliyofanyika Ikulu jijini Dodoma alisisitiza kuwa pamoja na kukuza uhusiano wa kidiplomasia ni muhimu pia kuendelea kuongeza jitihada katika kutekeleza sera ya diplomasia ya uchumi kwenye vituo vyao vya uwakilishi. 

Aidha Katibu Mkuu Balozi Joseph Sokoine amewapongeza Waheshimiwa Mabalozi kwa kuteuliwa katika nafasi hizo na amewatakia kheri katika utekelezaji wa majukumu yao. 
Mazungumzo yakiendelea

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine (kulia) Mhe. Balozi Dkt. Suleiman Haji Suleiman (kushoto) na Mhe. Luteni Jenerali Mathew Edward Mkingule Balozi wa Tanzania nchini Zambia (katikati) wakiwa kwenye mazungumzo yaliyofanyika katika ofisi za Wizara jijini Dodoma

BALOZI MUSHY ATAFUTA FURSA NCHINI AUSTRIA


Balozi wa Tanzania nchini Austria, Mhe. Celestine J. Mushy  (katikati) akutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo la Austria (Austrian Development Agency - ADA), Mhe. Balozi Friedrich Stift (kushoto) na Mkurugenzi wa  Idara ya Programme na Miradi ya Kimataifa, Bw. Heinz Habertheuer.  Viongozi hao walizungumzia masuala ya namna ya kuisaidia na kuiingiza Tanzania  kwenye  kundi la nchi zinazopewa kipaumbele kwa miradi inayofadhiliwa na Shirika hilo.   Vilevile, Mkurugenzi alieleza kuwa wanakamilisha mpango wa kuongezea mtaji wa Kampuni ya BioTan Group Ltd ya mwekezaji wa Austria inayozalisha na kubangua Korosho bila matumizi ya  kemikali (organic cashewnut).






 


Wednesday, July 20, 2022

MKUTANO WA KAMATI YA MAWAZIRI WANAOSHUGHULIKIA URATIBU NA UDHIBITI WA MAAFA WAFANYIKA MALAWI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Sera, Bunge na Uratibu, Mhe. George Simbachawene (Mb.), ameongoza ujumbe wa wa Tanzania kwenye Mkutano wa Kamati ya Mawaziri wanaoshughulika na Uratibu na Udhibiti wa Maafa kwa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) uliofanyika tarehe 19 Julai, 2022, Lilongwe, Malawi.


Mkutano huu pamoja na masuala mengine, ulijadili agenda kuhusu Uendeshaji wa Kituo cha Operesheni za Dharura na huduma za Kibinadamu cha SADC na kuhimiza Nchi Wanachama kukamilisha michakato ya ajira za kushikiza ili Kituo hicho kiweze kupata watumishi wa kutosha ili kukiwezesha kutekeleza majukumu yake kikamilifu.

Akichangia hoja katika agenda hii, Mhe. Simbachawene aliipongeza Sekretarieti ya SADC kwa jitihada mbalimbali zinazotekelezwa na pia alishauri kuwa Sekretarieti ya SADC iangalie njia mbalimbali za kushirikiana na wadau wa maendeleo katika kuimarisha utendaji kazi wa Kituo hicho.

Mkutano huu wa Mawaziri ulitanguliwa na Kikao cha Makatibu Wakuu wa Kamati ya Mawaziri wanaoshughulikia masuala ya Uratibu na Uthibiti wa Maafa, kilichofanyika tarehe 17 Julai 2022. Meja Jenerali Michael  Mumanga, Mkurugenzi wa Maafa, Ofisi ya Waziri Mkuu - Idara ya Maafa, aliongoza ujumbe wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Kikao hicho. Pamoja nae aliambatana na Afisa Mwandamizi kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Idara ya Maafa, Afisa Mwandamizi kutoka Kurugenzi ya Hali ya Hewa na Afisa Mambo ya Nje kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. 



Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu - Sera, Bunge na Uratibu, Mhe. George Simbachawene (wa pili kushoto), ameongoza ujumbe wa wa Tanzania kwenye Mkutano wa Kamati ya Mawaziri wanaoshughulika na Uratibu na Udhibiti wa Maafa kwa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) uliofanyika tarehe 19 Julai, 2022, Lilongwe, Malawi. Pichani Mhe. Simbachawene akiwa katik apicha ya pamoja na Wajumbe kutoka Nchi za SADC walioshiriki mkutano huo.

Picha ya pamoja

 

WAZIRI MULAMULA AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA MKUTANO WA 24 WA KAMATI YA MAWAZIRI WA SADC

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Liberata Mulamula ameongoza ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa 24 wa Kawaida wa Kamati ya Mawaziri wa Asasi ya Ushirikiano katika masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (MCO) uliofanyika jijini Pretoria, Afrika Kusini kuanzia tarehe 16 hadi 19 Julai, 2022. 

 

Mkutano huo ambao ulitanguliwa na Mkutano wa Makatibu Wakuu pamoja na mambo mengine umepokea na kujadili agenda mbalimbali zilizowasilishwa kwao ikiwemo Mapitio ya Utekelezaji wa Maamuzi ya Mkutano wa 23 wa MCO na Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC; Hali ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Kanda; na Tathmini ya Hali ya Ulinzi na Usalama katika Kanda.

 

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano huo, Mwenyekiti wa Kamati hiyo ambaye pia ni Waziri wa Uhusiano wa Kimataifa na Ushirikiano wa Afrika Kusini, Mhe. Dkt. Naledi Pandor amesema hali ya usalama katika kanda kwa ujumla inaridhisha na kwamba Nchi Wanachama wa SADC ziendelee kujitolea katika masuala ya ulinzi na usalama kwa maslahi mapana ya wananchi wa nchi hizo.

 

Kadhalika amesisitiza nchi wanachama kuendelea kupambana na ugaidi na vitendo vyote vya kigaidi katika Kanda huku akipongeza  Misheni ya SADC nchini Msumbiji (SAMIM) kwa kazi nzuri wanayoendelea kuifanya nchini humo ambapo wamefanikiwa kurejesha hali ya amani na usalama katika Jimbo la Cabo Delgado. 

 

Kuhusu utekelezaji wa maazimio yatokanayo na Mkutano wa 23 wa Kamati hiyo ya Mawaziri, Mhe. Dkt. Pandor amezipongeza Nchi Wanachama  na Sekretarieti ya SADC kwa kutekeleza maazimio hayo kwa takriban asilimia 81. 

 

“Utekelezaji huu bila shaka unadhihirisha dhamira ya dhati iliyopo miongoni mwetu ya kuhakikisha tunafikia lengo la kuimarisha amani na utulivu katika kanda”, alisema Mhe. Pandor.

 

Akizungumzia masuala ya demokrasia katika nchi wanachama, Mhe. Pandor amesisitiza nchi wanachama kuendelea kuendesha chaguzi zake kwa kufuata miongozo ya kidemokrasia ya SADC na ile ya nchi husika ili chaguzi hizo zikamilike kwa amani na utulivu.

 

“Katika kujenga amani na utulivu katika kanda, SADC itaendelea kuzingatia misingi ya demokrasia ili kuzuia migogogoro kwa maslahi mapana ya wananchi katika kanda. Kwa kuzingatia misingi hiyo SADC kama kanda itaendelea kuendesha chaguzi kwa kufuata misingi ya demokrasia, uwazi, amani na ukweli. Serikali za Angola na Lesotho zitakuwa na uchaguzi mkuu mwezi Agosti na Oktoba mwaka huu mtawalia. Tunawatakia wanachama wenzetu uchaguzi wa amani” alisisitiza Mhe. Pandor.



Awali akizungumza, Katibu Mtendaji wa SADC, Bw. Elias Magosi amesema kuwa Sekretarieti ya SADC itaendelea kushirikiana na Nchi Wanachama hususan katika kukabiliana na changamoto mbalimbali zilizopo katika kanda zikiwemo za kiusalama, kijamii na kiuchumi.

 

Pia alimpongeza Mwenyekiti wa Kamati ya Mawaziri anayemaliza muda wake Mhe. Pandor kwa kazi nzuri aliyofanya katika kipindi chote na kumkaribisha Mwenyekiti mpya ambaye ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Namibia na kumwahidi ushirikiano.

 

Mbali na Mhe. Balozi Mulamula, Ujumbe wa Tanzania ulimjumuisha pia Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Dkt. Stergomena Tax, Mwakilishi wa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Mnadhimu Mkuu wa Jeshi, Lt. Jenerali Salum Othman, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Kuzuia na  Kupambana na Rushwa,  Kamishna wa Polisi Salum  Hamduni, Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Mhe. Meja Jenerali Mstaafu Gaudence Milanzi, Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Agnes Kayola.Kupambana na Rushwa,  Kamishna wa Polisi Salum  Hamduni na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga.

 

Waziri wa Mambo ya Nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiongoza ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano wa 24 wa Kawaida wa Kamati ya Mawazirii wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC-MCO) uliofanyika Pretoria, Afrika Kusini tarehe 19 Julai 2022. Mkutano huo umemjumuisha pia Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Mhe. Dkt. Stergomena Tax, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na  Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma M. Rajab, Mwakilishi wa Mkuu wa Majeshi na Mnadhimu Mkuu wa Jeshi, Mhe. Lt. Jenerali Salum Othman na Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Mhe. Meja Jenerali Mstaafu Gaudence Milanzi

 Mhe. Balozi Mulamula na Mhe. Dkt. Tax wakiwa wamesimama kwa heshima kutekeelza itifaki za ufunguzi wa mkutano ikiwemo kupigwa wimbo wa Taifa la Afrika Kusini na ule wa SADC
Mhe. Dkt. Tax akiwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma M. Rajab wakatib wa Mkutano wa 24 wa Kamati ya Mawaziri wa SADC
 

Mwakilishi wa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Mnadhimu Mkuu wa Jeshi, Mhe. Lt. Jenerali Salum Othman (kulia) akiwa na Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Mhe. Meja Jenerali Mstaafu Gaudence Milanzi kwenye Mkutano wa 24 wa Kamati ya Mawaziri wa SADC

Mkutano ukiendelea

 

Tuesday, July 19, 2022

DKT. MPANGO ASISITIZA UTUNZAJI WA MAZINGIRA YA BAHARI

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amezisihi nchi wanachama 22 zinazoshiriki Warsha ya Umoja wa Mataifa ya kutathmini Hali ya Mazingira ya Bahari kuhakikisha kuwa wanalinda mazingira ya bahari, kuongeza uelewa pamoja na kujenga uwezo juu ya utawala wa bahari. 

Rai hiyo imetolewa na Dkt. Mpango leo Jijini Dar es Salaam wakati akifungua kongamano hilo la siku tisa lililozikutanisha nchi 22 na washiriki zaidi ya 50 kwa lengo la kujadili usimamizi na utunzaji wa bahari. 

Dkt. Mpango ameongeza kuwa vitendo vya kisayansi na teknolojia vinahitajika zaidi katika kusaidia kulinda mazingira ya bahari pamoja na ushirikishwaji wa wadau wote ikiwemo vijana na wanawake katika mijadala mbalimbali ya utunzaji wa mazingira ya bahari kwa kuwa wao ni sehemu ya suluhisho. 

“Endapo tutasimamia bahari na mazingira yake itasaidia kuongeza wigo wa ajira na kusaidia mamilioni ya watu kutoka kwenye umaskini. Kuna hitaji la kuongeza hatua zaidi kulinda mazingira ya bahari na rasilimali zinazohusiana. Tunapaswa kufanya mabadiliko ya kuboresha usimamizi na utunzaji wa bahari,” alisema Dkt. Mpango.

Nawapongeza wadau wote ambao wamekuwa wakishirikiana na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kutatua changamoto zinazokabili mazingira ya bahari na pia kutekeleza lengo namba 14 la Maendeleo Endelevu SDGs ikiwa ni pamoja na ufadhili wa lengo hilo kwani utunzaji wa Bahari na mazingira yake ni muhimu kwa maendeleo ya kijamii na kiuchumi.

Ni matumaini yangu kuwa kupitia warsha hii, mtaimarisha ujuzi, uwezo wa kisheria na kisayansi katika nyanja ya masuala ya bahari ili kufikia Ajenda ya mwaka 2030 ya Maendeleo Endelevu katika muktadha wa masuala ya bahari.

Kwa upande wake, Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira, Dkt. Selemani Jafo amesema dunia inajielekeza kuangalia ni jinsi gani bahari kwa ujumla wake inaweza kuwa nyenzo ya kujenga uchumi na masuala mbalimbali ya kijamii hivyo warsha hiyo itajadili taarifa mbalimbali za mwenendo wa kiuchumi na kijamii kuhusiana na bahari.

“Kongamano hili litasaidia katika majadiliano ili kubadilishana uzoefu wa masuala ya bahari, kujengeana uwezo kwa watafiti mbalimbali na kujionea jinsi gani mataifa mengine yanatumia fursa za bahari kujenga uchumi na kuondoa umasikini kwa wananchi wake,” alisema Dkt. Jafo

Naye Katibu Mkuu Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi – Zanzibar, Dkt. Aboud Jumbe amesema kuwa mkutano huo unasaidia kuwakutanisha wataalam mbalimbali kutoka nchi wanachama kujadili fursa za kiuchumi na kijamii za bahari.

“Tunahitaji taarifa sahihi za kisayansi, kimazingira, kiuchumi lakini pia taarifa ambazo ni rahisi kumfikia mwananchi na kufahamu hali halisi ya mazingira yake lakini pia taarifa hizo ziweze kusaidia hususan wavuvi, usafiri wa baharini hivyo ni muhimu kuwa na taarifa hizo,” alisema Dkt. Jumbe  

Kongamano hilo la masuala ya bahari limeratibiwa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa kushirikiana na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (Nemc).

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akiwasilisha hotuba yake wakati wa ufunguzi wa Warsha ya Umoja wa Mataifa ya kutathmini Hali ya Mazingira ya Bahari Jijini Dar es Salaam
Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP) Christine Musisi akiwasilisha hotuba yake katika  Warsha ya Umoja wa Mataifa ya kutathmini Hali ya Mazingira ya Bahari Jijini Dar es Salaam

Warsha ya Umoja wa Mataifa ya kutathmini Hali ya Mazingira ya Bahari Jijini Dar es Salaam


Meza kuu ikiongozwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango katika picha ya pamoja na viongozi waandamizi wa Serikali katika Warsha ya Umoja wa Mataifa ya kutathmini Hali ya Mazingira ya Bahari Jijini Dar es Salaam



Washiriki wa warsha ya Umoja wa Mataifa ya kutathmini Hali ya Mazingira ya Bahari wakifuatilia warsha



BALOZI ZA TANZANIA ZATAKIWA KUONGEZA KASI KATIKA KUTANGAZA FURSA ZA KIUCHUMI ZILIZOPO NCHINI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula ametoa wito kwa Mabalozi wa Tanzania nje kuongeza kasi katika utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi hususan katika kutangaza utalii, kuvutia wawekezaji na kuhamasisha biashara baina ya Tanzania na nchi mbalimbali duniani.

 

Balozi Mulamula ametoa wito huo alipotembelea Ubalozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini hivi karibuni na kuzungumza na Watumishi katika Ubalozi huo.

 

Mhe. Balozi Mulamula ambaye alipokelewa ubalozini hapo na Balozi wa Tanzania nchini humo, Meja Jenerali Mstaafu, Mhe. Gaudence Milanzi amesema kuwa, tangu Mhe. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania aingie madarakani, ameonesha kwa vitendo na kasi ya hali ya juu katika kutangaza fursa mbalimbali zinazopatikana nchini ikiwemo utalii, uwekezaji, biashara na utamaduni na kuwataka Mabalozi kwenda sambamba na kasi hiyo ya Mhe. Rais Samia ili kupata matokeo tarajiwa katika kukuza uchumi wa nchi.

 

“Nazipongeza Balozi zote kwa jitihada mbalimbali zinazoendelea kufanyika katika kutangaza fursa mbalimbali zilizopo nchini. Kasi nyumbani ni kubwa, hivyo nawasisitiza na ninyi Mabalozi wetu kuongeza kasi ili kwenda pamoja na kasi ya Mhe. Rais wetu ambaye amekuwa mstari wa mbele katika kuitangaza nchi,” alisema Balozi Mulamula.

 

Kadhalika amesema kuwa Wizara inaendelea kuimarisha mifumo mbalimbali ikiwemo Diplomasia ya Umma na Diplomasia ya Kidijitali ili kuwezesha nchi kujitangaza zaidi na kurahisisha mawasiliano na kwamba ataendelea kufanya vikao kazi na Mabalozi kila baada ya miezi mitatu ili kukumbushana masuala mbalimbali katika kuboresha utendaji kazi.

 

Akizungumzia utendaji katika Ubalozi wa Afrika Kusini, Waziri Mulamula alimpongeza Balozi Milanzi kwa kujenga umoja miongoni mwa Watumishi wa Ubalozi huo na kusisitiza kuendelea kutekeleza majukumu yao kwa weledi, nidhamu, ushirikiano, uadilif na ubunifu.

 

“Namshukuru Balozi kwa kujenga umoja miongoni mwenu. Nasisitiza ushirikiano, nidhamu, uadilifu, muwe wabunifu na  mfanye kazi zenu kwa weledi. Naomba mzingatie kuiwakilisha nchi vizuri kwani mmebeba taswira ya nchi” alisisitiza Balozi Mulamula.

 

Pia, Waziri Mulamula aliupongeza ubalozi huo kwa kulipa kipaumbele suala la Diaspora ambao idadi yao ni kubwa nchini humo na kuwasisitiza kuendelea kuwashirikisha Diaspora katika kuchangia maendeleo ya nchi. 

 

Vilevile, Mhe. Waziri Mulamula alitumia fursa ya kuwa nchini humo kutembelea nyumba mbili zinazomilikiwa na Serikali ili kuona hali ya nyumba hizo kwa ajili ya kutoa mapendekezo ya jinsi ya kuziboresha ili kuiwezesha Serikali kunufaika nazo kama vitega uchumi. Nyumba moja kati ya hizo inamilikiwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na nyingine inamilikiwa na Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL).

 

Kwa upande wake Balozi Milanzi, alimshukuru Mhe. Balozi Mulamula kwa kutenga muda na kutembelea Ubalozi huo na kuahidi kutekeleza maelekezo yote aliyotoa kwao. 

 

Mhe. Balozi Mulamula yupo nchini Afrika Kusini akiongoza Ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano wa 24 wa Kawaida wa Kamati ya Mawaziri wa Asasi ya Ushirikiano katika masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (MCO) utakaofanyika jijini Pretoria, Afrika Kusini tarehe 19 Julai, 2022.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika Ubalozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini. Kulia ni Balozi wa Tanzania nchini humo, Mhe. Meja Jenerali Mstaafu Gaudence Milanzi. Mhe. Waziri Mulamula yupo nchini humo akiongoza ujumbe wa Tanzania kwenye Mkutano wa Kawaida wa 24 wa Kamati ya Mawaziri wa SADC wa Ushirikiano katika masuala ya Siasa, Ulinzi na Usalama utakaofanyika Pretoria tarehe 19 Julai 2022. Wanaoshuhudia ni Balozi wa Tanzania nchini humo, Mhe. Meja Jenerali Mstaafu Gaudence Milanzi na Mkurugenzi wa Mawasiliano katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga
 

 

Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Mhe. Meja Jenerali Mstaafu Gaudence Milanzi akimkaribisha Mhe. Balozi Liberata Ubalozini kwa ajili ya kuzungumza na Watumishi wa Ubalozi huo
Mhe. Waziri Mulamula akizungumza na Watumishi wa Ubalozi (hawapo pichani) wa Tanzania nchini Afrika Kusini
 Mhe. Balozi Mulamula akiendelea na mazungumzo na Watumishi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini alipotembelea ubalozi huo hivi karibuni
         
 
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma M. Rajab ambaye aliambata na Waziri Mulamula Ubalozini hapo naye akichangia jambo wakati wa mazungumzo hayo
Naibu Katibu Mkuu, Balozi Fatma (kushoto) akiwa na Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kikanda, Balozi Agnes Kayola wakifuatilia mazungumzo kai ya Mhe. Balozi Mulamula na Watumishi wa Ubalozi (hawapo pichani)
Mkurugenzi wa Mawasiliano katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga akiwa na Afisa wa Ubalozi Mwandamizi, Bw. Peter Shija wakifuatilia kikao kati ya Mhe. Waziri na Watumishi wa Ubalozi huo

Sehemu ya Watumishi wa Ubalozi wakiwa kwenye kikao na Mhe. Balozi Mulamula. Kulia ni Mkuu wa Utawala Ubalozini, Bw. Deogratius Dotto akiwa na Bi. Happiness Godfrey, Afisa katika Ubalozi huo

 Sehemu nyingine ya Watumishi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini. Kushoto ni Bibi Faith Masaka na Bw. Rweyemamu
     


 Kikao kikiendelea
              



Afisa katika Ubalozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Bi. Happiness Godfery akimkabidhi zawadi ya ua Mhe. Balozi Mulamula mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa OR Tambo jijini Johannesburg. Mhe. Balozi Mulamula yupo nchini humo kwa ajili ya kushiriki Mkutano wa 24 wa Kamati ya Mawaziri wa SADC

Mhe. Balozi Mulamula akisalimiana na Mkuu wa Utawala katika Ubalozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Bw. Deogratius Dotto wakati wa mapokezi yake mara baada ya kuwasili nchini humo. Wengine katika picha ni Mkurugenzi wa Mawasiliano, Balozi Kasiga na Mwakilishi wa Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini, Bw. Peter Shija
 
Mhe. Balozi Mulamula akipata maelezo kuhusu moja ya nyumba zinazomilikiwa na Serikali zilizopo nchini Afrika Kusini alipozitembelea kwa ajili ya kufanya tathmini ya nyumba hizo.  Kati ya nyumba hizo mbili,  moja inamilikiwa na Serikali ya Mapinduzi Zanzibar na nyingine inamilikiwa na ATCL

Mhe. Waziri Mulamula  kwa pamoja na Naibu Katibu Mkuu, Balozi Fatma wakiangalia nyumba hiyo (haipo pichani)

Mhe. Balozi Mulamula akipata maelezo kuhusu nyumba inayomilikiwa na ATCL alipotembelea eneo hilo jijini Johannesburg