Thursday, July 21, 2022

KATIBU MKUU BALOZI SOKOINE AKUTANA NA MABALOZI PUNDE BAADA YA KUAPISHWA


Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine (katikati) Mhe. Balozi Dkt. Suleiman Haji Suleiman (kulia) na Mhe. Luteni Jenerali Mathew Edward Mkingule Balozi wa Tanzania nchini Zambia (kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja 

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine tarehe 20/07/2022 alikutana na kufanya mazungumzo na Mhe. Balozi Dkt. Suleiman Haji Suleiman na Mhe. Luteni Jenerali Mathew Edward Mkingule Balozi wa Tanzania nchini Zambia katika ofisi za Wizara jijini Dodoma.

Balozi Sokoine katika mazungumzo hayo yaliyofanyika muda mfupi baada ya viongozi hao kuapa kutumikia nyadhifa hizo katika hafla iliyofanyika Ikulu jijini Dodoma alisisitiza kuwa pamoja na kukuza uhusiano wa kidiplomasia ni muhimu pia kuendelea kuongeza jitihada katika kutekeleza sera ya diplomasia ya uchumi kwenye vituo vyao vya uwakilishi. 

Aidha Katibu Mkuu Balozi Joseph Sokoine amewapongeza Waheshimiwa Mabalozi kwa kuteuliwa katika nafasi hizo na amewatakia kheri katika utekelezaji wa majukumu yao. 
Mazungumzo yakiendelea

Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Joseph Sokoine (kulia) Mhe. Balozi Dkt. Suleiman Haji Suleiman (kushoto) na Mhe. Luteni Jenerali Mathew Edward Mkingule Balozi wa Tanzania nchini Zambia (katikati) wakiwa kwenye mazungumzo yaliyofanyika katika ofisi za Wizara jijini Dodoma

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.