Monday, July 11, 2022

BALOZI MULAMULA AKUTANA NA WANAFUNZI-DIASPORA WA MAREKANI.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula amekutana na walimu na wanafunzi wenye asili ya Afrika na Marekani wanaofundisha na kusoma vyuo mbalimbali vya Marekani ambao wapo nchini kwa ziara ya kikazi hadi tarehe 17 Julai 2022.

Ziara hiyo iliyoratibiwa na Mtanzania-Diaspora, Bi Zawadi Sakapala ambaye ni mmiliki wa kituo cha “Community Centre” kilichopo Kijichi jijini Dar Es Salaam inalenga pamoja na mambo mngine, kutoa fursa kwa wanafunzi hao kujifunza masuala ya utamaduni wa Tanzania na kubadilishana ujuzi na uzoefu katika masomo ya sayansi, ufundi, ufundishaji na Usimamizi wa watoto wadogo (daycare).

Katika kikao hicho, Bi Zawadi alimfahamisha Mhe. Balozi Mulamula kuwa kituo chake kimekuwa kikishirikiana na vyuo vikuu mbalimbali nchini Marekani kuratibu ziara za walimu na wanafunzi wenye asili ya Afrika na Marekani kutembelea nchi za Afrika kwa ajili ya kubadilishana uzoefu katika sekta ya elimu.

Hivyo, ili kuimarisha sekta ya elimu katika nchi za Afrika, kikao hicho kiliazimia kuongeza jitihada za kuhamasisha Waafrika wengi zaidi kujiunga na vyuo vya Marekani, kuunganisha vyuo vya Afrika na Marekani, wanafunzi-Watanzania wanaopata fursa ya kusoma Marekani, watumike kufundisha lugha ya Kiswahili ikiwa ni moja ya njia ya kueneza lugha hiyo duniani pamoja na kwahimiza watu wenye asili ya Afrika kutumia elimu, ujuzi na maarifa waliyopata wakiwa ughaibuni kuinua jamii za nchi za Afrika.

Wakati huo huo, Balozi Mulamula amekutana na Ujumbe wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Programu ya Maendeleo (UNDP) ambao upo nchini kwa ajili ya kufanya mazungumzo na wadau wa siasa ili kubainisha maeneo ambayo, shirika hilo linaweza kusaidia katika uendeshaji wa uchaguzi mkuu ujao.

Ujumbe huo unaongozwa na Afisa Uchaguzi Mkuu katika Idara ya Siasa na Masuala ya Amani ya Umoja wa Mataifa, Bw. Akinyemi Adegbola umefanikiwa kufanya vikao na wadau mbalimbali ikiwa ni pamoja na Tume ya Taifa ya Uchaguzi, wawakilishi wa vyama vya siasa na asasi za kiraia, umepokea maoni ya wadau hao ya maoneo yanayohitaji msaada na umeahidi utayafanyia kazi kikamilifu. Maeneo hayo ni pamoja na uelimishaji wa wapiga kura, msaada wa kiufundi katika upigaji na uandikishwaji wa wapiga kura na teknolojia ya mawasiliano wakati zoezi la uchaguzi.

Kwa upande wake, Balozi Mulamula aliueleza ujumbe huo kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan katika kipindi kifupi cha uongozi wake ameonesha dhamira ya dhati ya kuboresha mazingira ya kisiasa nchini, kwa kuhamasisha majadiliano ya kisiasa, ushirikishwaji wa wadau wote, umoja na mshikamano wa kitaifa. Hivyo, aliuhakikishia ujumbe huo kuwa uchaguzi ujao utaendelea kuwa huru, haki na amani kama ilivyo desturi ya Tanzania.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akiongea na walimu na wanafunzi wenye asili ya Afrika na Marekani (hawapo pichani) wanaosoma na kufundisha vyuo mbalimbali vya Marekani ambao wapo nchini kwa ziara maalum hadi tarehe 17 Julai 2022.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akimsikiliza mmoja wa mwanafunzi anayesoma katika vyuo vikuu vya Marekani kuhusu mikakati ya kusaidia vijana wa Afrika kupata elimu bora itakayoweza kukabili mazingira ya dunia ya sasa.

Mhitimu wa Shahada ya Uzamivu kutoka Chuo Kikuu cha Howard cha nchini Marekani ambaye pia ni Kiongozi wa Taasisi ya 3GC Inc. akieleza shughuli za taasisi hiyo zinazolenga kuwasaidia vijana wa Afrika 
Mkurugenzi wa Kitengo cha Diaspora katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi James Bwana na Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali, Balozi Mindi Kasiga wakifuatilia mazungumzo baina ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula na walimu na wanafunzi wenye asili ya Afrika na Marekani wanaosoma na kufundisha vyuo mbalimbali vya Marekani


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akimvisha scurf ya bendera ya Tanzania, mmiliki wa kituo cha “Community Centre” kilichopo Kijichi jijini Dar Es Salaam, Bi. Zawadi Sakapala

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akiwa katika picha ya pamoja na walimu na wanafunzi wenye asili ya Afrika na Marekani wanaosoma na kufundisha vyuo mbalimbali vya Marekani



BALOZI MULAMULA AKUTANA NA  AFISA UCHAGUZI MKUU WA UN


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akiwa katika mazungumzo na Afisa Uchaguzi Mkuu katika Idara ya Siasa na Masuala ya Amani ya Umoja wa Mataifa, Bw. Akinyemi Adegbola yaliyofanyika jijini Dar Es Salaam

Baadhi ya ujumbe uliongozana na Afisa Uchaguzi Mkuu katika Idara ya Siasa na Masuala ya Amani ya Umoja wa Mataifa, Bw. Akinyemi Adegbola kwenye mazungumzo ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula na Afisa huyo.

Ujumbe wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula ukifuatilia mazungumzo yake na Afisa Uchaguzi Mkuu katika Idara ya Siasa na Masuala ya Amani ya Umoja wa Mataifa

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akiagana na ujumbe wa UNDP ambao upo nchini kwa ajili ya kuzungumza na wadau wa siasa kuhusu uchaguzi.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akiwa katika picha ya pamoja na ujumbe wa UNDP ambao upo nchini kwa ajili ya kuzungumza na wadau wa siasa kuhusu uchaguzi.


BALOZI MULAMULA AKUTANA NA MWAKILISHI MKAZI WA UN WOMEN

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akiwa katika mazungumzo na Mwakilishi Mkazi wa  UN Women, Bi.  Hodan Addou kwenye Hoteli ya Seana jinini Dar Es Salaam.


BALOZI MULAMULA AKUTANA NA  BALOZI MTEULE LT. JEN. MATHEW EDWARD MKINGULE 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akiwa katika mazungumzo na Balozi Mteule Lt. Jen. Mathew Edward Mkingule yaliyofanyika jijini Dar Es Salaam


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushiikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akiwa na Balozi Mteule Lt. Jen. Mathew Edward Mkingule baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika jijini Dar Es Salaam


 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.