Friday, July 1, 2022

TANZANIA YASHIRIKI KONGANANO LA MIJI DUNIANI

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeshiriki Kongamano la Kumi na Moja la Miji Duniani, lililofanyika jijini Katowice, Poland tarehe 26 hadi 30 Juni 2022.

Ujumbe wa Tanzania umeongozwa na Balozi wa Tanzania nchini Kenya na Mwakilishi katika Shirika la UN Habitat Mhe. John Simbachawene

Katika kongamano hilo, Balozi Simbachawene alieleza hatua zinazochukuliwa na Serikali katika kuleta maendeleo endelevu ya miji kwa kutengeneza sera ya maendeleo ya miji, kuwekeza kwenye miundombinu, kuwezesha sekta binafsi na kuhamasisha utunzaji wa mazingira katika miji. 

Kupitia konganabo hilo, Balozi Simbachawene alipata nafasi ya kuzungumza na wadau mbalimbali wa maendeleo wakiwemo UN Habitat, AfDB, UNECA, UNDP, Islamic Fund, Saudi Fund, European Commission ambao aliwaelezea kuhusu mipango ya Serikali ya kuendeleza miji na kuwaomba kuiunga mkono Serikali katika utekelezaji wa mipango hiyo ili kutimiza lengo Namba 11 la Umoja wa Mataifa  la Maendeleo Endelevu  linalohusu maendeleo  makazi na miji na (SDG 11).

Mbali na Balozi Simbachawene, Balozi wa Ujerumani anayewakilisha pia nchini Poland Mhe. Dkt. Abdalah Possi pia alishiriki kongamano hilo.  

Taasisi nyingine zilizoshiriki ni pamoja na Shirika la Nyumba Tanzania (NHC), Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, Ofisi ya Rais -TAMISEMI, Manispaa ya Jiji la Dodoma, TARURA na DART.






No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.