Wednesday, July 27, 2022

WAZIRI MULAMULA ATOA WITO KWA AFRIKA KUTHAMINI MCHANGO WA WANAWAKE KATIKA KUJENGA UCHUMI


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) ametoa wito kwa Jumuya ya Afrika kutambua na kuthamini mchango wa Wanawake kwenye maendeleo ya uchumi. 

Waziri Mulamula ameyasema hayo alipokuwa akifungua Mkutano wa Uchumi wa Wanawake Afrika (Pan-African Women Economic Summit 2022) uliofanyika tarehe 26 Julai 2022 jijini Dar es Salaam. Waziri Mulamula ameeleza kuwa pamoja na mchango mkubwa unaotolewa na wanawake kwenye maendeleo, bado katika maeneo mengi barani Afrika hawatambui na kuthamini ipasavyo mchango huo hivyo kufifisha jitihaza za kundi hilo muhimu na lenye idadi kubwa barani katika kujenga uchumi wa familia na Taifa kwa ujumla.

Waziri Mulamula aliendelea kubainisha kuwa endapo mchango wa wanawake ungetambuliwaingewapa motisha zaidi ya kuendelea kushiriki katika shughuli za maendeleo kwenye jamii na kajikwamua dhidi ya umaskini uliokithiri na hali ngumu ya maisha. 

Pamoja na hayo Waziri Mulamula akifafanua zaidi hoja yake alieleza kuwa kutambua mchango wa wanawake kwenye uchumi ni muhimu kwa mamlaka mbalimbali kuanza kufikiria namna ya kuwavutia wanawake kuendesha shughuli zao katika sekta rasmi. 

"Wanawake wa Kiafrika ni wajasiriamali wa hali ya juu, wanamiliki theluthi moja ya biashara zote barani Afrika, Hata hivyo wajasiriamali wanawake wana uwezekano mkubwa wa kuendesha biashara ndogo ndogo katika sekta isiyo rasmi, wakijihusisha na shughuli za ongezeko la thamani la chini ambazo huvuna faida ndogo. Wanaelekea kuwa wajasiriamali wa lazima, badala ya fursa, wakiongozwa na biashara ndogo na ukosefu wa njia mbadala” Alisema Waziri Mulamula.

Kwa upande Mkurugenzi wa Tanzania Women CEO’s Roundtable Bi. Emma Kawawa akizungumza kwenye hafla ufunguzi wa mkutano huo, alieleza kuwa lengo la mkutano huo ni pamoja na kuwahamasisha wanawake kushiri katika shughuli rasmi za uzalishaji mali. 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akipokelewa na Waandaaji wa Mkutano wa Uchumi wa Wanawake Afrika alipowasili katika mkutano uliofanyika jijini Dar es Salaam. Tarehe 26 Julai 2022
Sehemu ya washiriki wa Mkutano wa Uchumi wa Wanawake Afrika wakifualia mjadala ulikokuwa ukiendelea
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiwa katika picha ya pamoja waandaaji na baadhi ya washiriki wa Mkutano wa Uchumi wa Wanawake Afrika uliofanyika jijini Dar es Salaam
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb) akisisitiza jambo wakati wa akifungua Mkutano wa Uchumi wa Wanawake Afrika (Pan-African Women Economic Summit 2022) uliofanyika jijini Dar es Salaam

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.