Tuesday, July 12, 2022

KIWANDA CHA LABIOFAM KIBAHA KUPANULIWA

Serikali za Tanzania na Cuba zipo katika mchakato wa kupanua kiwanda cha Labiofam kilichopo Kibaha, Pwani cha kuzalisha viuadudu vya mazalia ya mbu ili kiwe na uwezo wa kuzalisha mbolea na dawa nyingine za kuua wadudu waharibifu wa mazao ya kilimo.

Hayo yamesemwa leo tarehe 12 Julai 2022 jijini Dar Es Salaam na Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Dkt Grace Magembe wakati wa ufunguzi wa kikao kati ya Serikali za Tanzania na Cuba cha kujadiliana kuhusu upanuzi wa kiwanda hicho kinachoendeshwa kwa ubia baina ya Serikali hizo mbili.

Dkt. Magembe ambaye ni kiongozi wa ujumbe wa Tanzania unaojadiliana na ujumbe wa Cuba, alisema kuwa ana matumaini makubwa katika kikao hicho cha siku mbili, wajumbe watafikia makubaliano yatakayokuwa na manufaa kwa wananchi wa pande zote mbili.

 

“Kama unavyofahamu asilimia 70 hadi 80 ya Watanzania ni wakulima, hivyo, uwepo wa kiwanda hiki na uzalishaji wa mbolea na viuadudu ni fursa nzuri kwa wakulima wetu na nchi kuendeleza sekta ya kilimo pamoja na wananchi kujipatia kipato kwa mazao watakayovuna”, Dkt. Magembe alisema.

 

Kwa upande wake kiongozi wa ujumbe wa Cuba ambaye ni Mkurugenzi wa Uhusiano wa Kimataifa kutoka Wizara ya Kilimo ya nchi hiyo, Bw. Orlando Diaz Rodriguez alisema kuwa uwepo wa kiwanda hicho ni ishara ya wazi ya uhusiano mzuri uliopo kati ya Cuba na Tanzania.

Aidha, naye alielezea matumaini yake kuwa majadiliano hayo ya siku mbili yatakuwa na faida kubwa kwa maendeleo ya sekta ya kilimo ya Tanzania na azma ya Serikali ya kupamabana na ugonjwa wa malaria na hatimaye kuuangamiza kabisa.


Kiongozi wa ujumbe wa Cuba ambaye ni Mkurugenzi wa Uhusiano wa Kimataifa kutoka Wizara ya Kilimo ya nchi hiyo, Bw. Orlando Diaz Rodriguez akitoa neno wakati wa ufunguzi wa kikao kati ya Serikali za Tanzania na Cuba cha kujadiliana kuhusu upanuzi wa kiwanda cha LABIOFAM cha Kibaha. Kulia kwake ni Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Dkt Grace Magembe ambaye ni Kiongozi wa timu ya majadiliano ya Tanzania. 


Kiongozi wa ujumbe wa Cuba ambaye ni Mkurugenzi wa Uhusiano wa Kimataifa kutoka Wizara ya Kilimo ya nchi hiyo, Bw. Orlando Diaz Rodriguez akielezea matumaini yake kuwa kikao cha majadiliano kitakuwa na manufaa kwa pande zote mbili

Wataalamu wa Tanzania wanaoshiriki kikao cha majadiliano kati ya Tanzania na Cuba kuhusu upanuzi wa kiwanda cha LABIOFAM kinachoendeshwa kwa ubia kati ya Cuba na Tanzania

Mkurugenzi Mwendeshaji wa Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC),     Dkt. Nicolous Shombe akiongea jambo katika kikao cha majadiliano kati ya Tanzania na Cuba kuhusu upanuzi wa kiwanda cha LABIOFAM kinachoendeshwa kwa ubia kati ya Cuba na Tanzania

Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Mhe. Valentino Mlowola akiongea jambo katika kikao hicho. Mwingine ni MKurugenzi wa Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Swahiba Mndeme

Balozi wa Cuba nchini Tanzania, Mhe. Yordenis Despaigne Vera akiongea jambo katika kikao cha majadiliano kati ya Tanzania na Cuba kuhusu upanuzi wa kiwanda cha LABIOFAM
Wajumbe wa Tanzania na Cuba wakiwa katika ufunguzi wa kikao cha majadiliano kati ya Tanzania na Cuba kuhusu upanuzi wa kiwanda cha LABIOFAM kinachoendeshwa kwa ubia kati ya Cuba na Tanzania

Naibu Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Dkt Grace Magembe (katikati), Kiongozi wa ujumbe wa Cuba ambaye ni Mkurugenzi wa Uhusiano wa Kimataifa kutoka Wizara ya Kilimo ya nchi hiyo, Bw. Orlando Diaz Rodriguez (kulia) na Mkurugenzi Mwendeshaji wa Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC), Dkt. Nicolous Shombe wakiwa katika picha ya pamoja na ujumbe wa Tanzania na Cuba unaofanya majadiliano kuhusu upanuzi wa kiwanda cha LABIOFAM

 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.