Thursday, April 25, 2024
BARAZA LA MAWAZIRI EAC LAKUTANA JIJINI ARUSHA.
Wednesday, April 24, 2024
KATIBU MKUU, CCM AWAPONGEZA MABALOZI WAKIKAMILISHA WARSHA YA SIKU 4 KIBAHA
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Emmanuel Nchimbi akizungumza na Mabalozi wa Tanzania wanaoshiriki warsha ya siku 4 katika Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Julius Nyerere mjini Kibaha, Pwani. |
Warsha ikiendelea |
Tuesday, April 23, 2024
TUMIENI UZOEFU KUHARAKISHA MADADILIKO, BALOZI KUSILUKA
Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka akiongea na Mabalozi katika warsha ya kutathimini utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje inayofanyika mjini Kibaha, Pwani. |
Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka akiongea na Mabalozi katika warsha ya kutathimini utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje inayofanyika mjini Kibaha, Pwani. |
Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka akiongea na Mabalozi katika warsha ya kutathimini utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje inayofanyika mjini Kibaha, Pwani. |
Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka akifuatilia mjadala uliokuwa ukiendelea kwenye warsha ya Mabalozi ya kutathimini utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje inayofanyika katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere mjini Kibaha, Pwani |
Kutoka Kushoto; Waziri wa Mambo ya Nje na Ushikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses, Naibu Waziri Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk na Naibu Waziri anayeshughulikia masuala ya Afrika Mashariki Mhe. Stephen Byabato wakifuatilia warsha ya Mabalozi ya kutathimini utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje inayofanyika katika Shule ya Uongozi ya Mwalimu Julius Nyerere mjini Kibaha, Pwani |
Monday, April 22, 2024
RAIS SAMIA ARIDHISHWA NA KAZI YA MABALOZI NA KUWATAKA KUONGEZA JUHUDI
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba akimkaribisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwahutubia Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania sehemu mbalimbali duniani waliokusanyika mjini Kibaha kwa warsha ya kutathimini utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje |
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba akimkaribisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwahutubia Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania sehemu mbalimbali duniani waliokusanyika mjini Kibaha kwa warsha ya kutathimini utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje |
Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania sehemu mbalimbali duniani waliokusanyika mjini Kibaha kwa warsha ya kutathimini utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje wakifurahia jambo wakati Rais wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan alipokuwa akiwahutubia kwa njia ya mtandao. |
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. January Makamba akimkaribisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwahutubia Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania sehemu mbalimbali duniani waliokusanyika mjini Kibaha kwa warsha ya kutathimini utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje |
Mabalozi wakifuatilia hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan |
Sehemu ya Mabalozi na Viongozi wa Wizara wakifurahia jambo wakati Rais wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan alipokuwa akiwahutubia kwa njia ya mtandao. |
Sehemu ya mabalozi wa wakifuatilia hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyoitoa kwa njia ya mtandao. |
Sehemu ya mabalozi wa wakifuatilia hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyoitoa kwa njia ya mtandao. |
Sehemu ya mabalozi wa wakifuatilia hotuba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyoitoa kwa njia ya mtandao. |
Mkurugenzi wa Mawasiliano Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akiwasilisha mada kwenye warsha ya kutathimini utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje |
Mkurugenzi wa Mawasiliano Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akiwasilisha mada kwenye warsha ya kutathimini utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje |
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwahutubia Mabalozi wanaoiwakilisha Tanzania sehemu mbalimbali duniani kwanjia ya mtandao waliokusanyika mjini Kibaha kwa warsha ya kutathimini utekelezaji wa Sera ya Mambo ya Nje
|
Saturday, April 20, 2024
MABALOZI WA TANZANIA WAJIFUNGIA KIBAHA KUTAFAKARI NA KUJIPANGA UPYA
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (Mb) akisisitiza jambo alipokuwa akizungumza na Mabalozi kuelekea warsha inayotarajiwa kuanza tarehe 21 Aprili 2024 mjini Kibaha, Pwani |
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba (Mb) akizungumza kwenye kikao kazi kuelekea warsha ya Mabalozi inayotarajiwa kuanza tarehe 21 Aprili 2024 mjini Kibaha, Pwani |
Sehemu ya Mabalozi wakifurahia jambo wakati Waziri Makamba akizungumza kwenye kikao cha maandalizi kuelekea warsha ya Mabalozi inayotarajiwa kuanza tarehe 21 Aprili 2024 mjini Kibaha, Pwani |
Mwenyekiti wa Umoja wa Mabalozi Wastaafu Mhe. Balozi Aziz Ponary Mlima akizungumza kwenye kikao cha maandalizi kuelekea warsha ya Mabalozi inayotarajiwa kuanza tarehe 21 Aprili 2024 mjini Kibaha, Pwani |
Friday, April 19, 2024
MHE. RAIS SAMIA AWAKARIBISHA WAFANYABIASHARA WA UTURUKI KUSHIRIKI MAONESHO YA SABASABA
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ametoa mwaliko rasmi kwa Jumuiya ya Wafanyabiashara na Wawekezaji wa Uturuki kushiriki Maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam maarufu kama Sabasaba yanayotarajiwa kufanyika nchini mwishoni mwa mwezi Juni 2024.
Mhe. Rais Dkt. Samia ametoa mwaliko huo wakati akifungua rasmi Kongamano la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Uturuki lililofanyika leo tarehe 19 Aprili 2024 jijini Istanbul na kuhudhuriwa na zaidi ya wafanyabiashara na wakezaji 150 kutoka nchi hizi mbili.
Amesema maonesho hayo ya biashara ambayo ni makubwa Afrika Mashariki hutoa fursa ya kuwakutanisha wafanyabiashara na kuwawezesha kubadilishana taarifa na uzoefu, kujua taarifa mpya za masoko na bidhaa pamoja na kuuza bidhaa zao.
Kadhalika Mhe. Rais Samia ametumia fursa hiyo kuwakaribisha wafanyabiashara na wawekezaji kutoka Uturuki kuja kuwekeza nchini na kuitaja Tanzania kama nchi yenye fursa lukuki kama vile ardhi yenye rutuba kwa ajili ya kilimo, Hifadhi za wanyama kwa ajili ya utalii, nishati, madini ikiwemo Tanzanite ambayo hupatikana nchini Tanzania pekee na fursa za biashara na uwekezaji.
Amesema Serikali yake imeendelea kuboresha mazingira ya ufanyaji biashara na uwekezaji ambapo pamoja na mambo mengine imewekeza katika kujenga miundombinu inayoiunganisha Tanzania na nchi nyingine jirani ikiwemo Reli ya Kisasa ya SGR.
Vilevile, Mhe. Rais Samia alitumia fursa hiyo kuzipongeza Wizara za Mambo ya Nje za nchi hizi mbili kwa kuandaa kwa mafanikio Kongamano hilo ambalo ni jukwaa muhimu katika kukuza ushirikiano kwenye sekta ya biashara na uwekezaji.
Kwa upande wake, Makamu wa Rais wa Uturuki, Mhe. Cevdet Yilmaz ambaye alishiriki Kongamano hilo, amesema nchi yake itaendelea kuimarisha ushirikiano na Tanzania katika sekta ambazo nchi hiyo imepiga hatua ikiwemo Utalii, Usafirishaji, Biashara na Uwekezaji.
Awali akizungumza kwenye Kongamano hilo, Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji amesisitiza umuhimu wa nchi hizi mbili kushirikiana na Sekta Binafsi katika kufikia malengo ya kukuza uchumi kwa manufaa ya wananchi wa mataifa haya.
Kadhalika ametoa rai kwa Jumuiya ya Wafanyabiashara wa Tanzania kuunga mkono juhudu nyingi zinazofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia na mataifa mbalimbali ikiwemo Uturuki ili kutengeneza mazingira wezeshi ya ufanyaji biashara za kuvuka mipaka kwa Watanzania.
Mhe. Rais Samia yupo nchini Uturuki kwa ziara ya kitaifa kufuatia mwaliko wa Rais wa nchi hiyo, Mhe. Recep Tayyip Erdogan.
Rais wa Jamhuri ya Mungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akifungua rasmi Kongamano la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Uturuki lililofanyika jijini Istanbul, Uturuki tarehe 19 Aprili 2024. Pamoja na mambo mengine Mhe. rais Samia alitumia nafasi hiyo kuwaalika wafanyabiashara kutoka Uturuki kushiriki Maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam yanayotarajiwa kuanza mwishoni mwa mwezi Juni 2024 |
Waziri wa Viwanda na Biashara, Dkt. Ashatu Kijaji akizunumza wakati wa Kongamano la Baishara kati ya Tanzania na Uturuki |
Mhe. Rais Dkt. Samia akiwa na Makamu wa Rais wa Uturuki, Mhe.
Cevdet Yilmaz pamoja na viongozi wengine akiwemo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. January Makamba wakati wa Kongamano la Biashara kati ya Tanzania na Uturuki |
Makamu wa Rais wa Uturuki, Mhe. Cevdet Yilmaz akizungumza wakati wa Kongamano la Biashara kati ya Tanzania na Uturuki |
Kongamano la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Uturuki likiendelea |
Mhe. Rais Samia na Makamu wa Rais wa Uturuki, Mhe. Yilmaz na viongozi wengine wakiwa wamesimama kwa ajili ya heshima ya nyimbo za mataifa haya mawili zikipigwa wakati wa ufunguzi rasmi wa Kongamano la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Uturuki lililofanyika Jijini Istanbul tarehe 19 Aprili 2024 |
Mkurugenzi wa Biashara za Kimataifa na Diplomasia ya Uchumi katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikano wa Afrika Mashariki Balozi John Ulanga (mwenye tai y abuluu) akiwa na wageni waalikwa na wafanyabiashara kutoka Tanzania kwenye Kongamano la Biashara kati ya Tanzania na Uturuki. |
Mkurugenzi wa Sheria atika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikano wa Afrika Mashariki, Dkt. Gift Kweka akiwa na Afisa Mambo ya Nje, Bi. Mariam Killo wakishiriki Kongamano la Baiashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Uturuki |
Kongamano likiendelea |
Sehemu ya Wafanyabiasha na wawekezaji wa Uturuki wakishiriki Kongamano |
Mhe. Waziri Makamba akibadilishana mawazo na mmoja wa wageni waalikwa walioshiriki Kongamano la Biashara na Uwekezaji kati ya Tanzania na Uturuki |
Kongamano likiendelea |
Sehemu ya washiriki wa Kongamano |
Mhe. Rais Samia na Viongozi wengine wakishiriki sehemu ya utaratibu wa ufunguzi wa Kongamano la Biashara kati ya Tanzania na Uturuki |