Friday, May 17, 2013

Tanzania na Canada zasaini Mkataba wa Kulinda na Kukuza Uwekezaji


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K.Membe (Mb.), kwa pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje wa Canada, Mhe. John Baird wakisaini Mkataba wa Kulinda na Kukuza Uwekezaji (FIPA) kati ya Tanzania na Canada. Hafla hiyo fupi ilifanyika Wizarani tarehe 16 Mei, 2013.

Mhe. Membe na Mhe. Baird wakiendelea kusaini mkataba huo huku Maafisa wa Sheria kutoka Tanzania na Canada wakishuhudia. Kushoto kwa Mhe. Membe ni Bw. Abdallah Mtibora, Afisa Mambo ya Nje katika Kitengo cha Sheria, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Rajab Gamaha akiwa na Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika, Balozi Dora Msechu (katikati), na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara hiyo Bibi Grace Shangali wakishuhudia uwekaji saini wa Mkataba wa FIPA.

Wajumbe wengine waliokuwepo kushuhudia tukio hilo la uwekaji saini wa Mkataba wa FIPA.

Mhe. Membe  na Mhe. Baird wakibadilishana Mkataba huo mara baada ya kusaini.
Mhe. Membe na Mhe. Baird wakionesha kwa Wajumbe Mkataba waliosaini.

Mhe. Membe akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusu Mkataba wa FIPA.


Waandishi wa Habari pamoja na Wajumbe wengine wakimsiliza Mhe. Membe alipokuwa akitoa ufafanuzi kuhusu Mkataba wa Kukuza na Kulinda Uwekezaji kati ya Tanzania na Canada (FIPA).

Mhe. Baird nae akizungumza machache kuhusu mkataba huo.



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.