Tuesday, May 14, 2013

Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa akutana kwa mazungumzo na Mwakilishi wa UNIDO hapa nchini

Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy (kulia) akizungumza na Mwakilishi wa Shirika la Kimataifa la Maendeleo ya Viwanda (UNIDO) hapa nchini, Bw. Emmanuel Kalenzi alipofika Wizarani leo. Katika mazungumzo yao walizungumzia kuhusu maendeleo ya viwanda hapa nchini ikiwa ni pamoja na juhudi zinazofanywa na UNIDO kwa kushirikiana na SIDO katika kuendeleza viwanda vidogo vidogo katika mikoa mbalimbali hapa nchini.

Bw. Kalenzi akifafanua jambo kwa Balozi Mushy wakati wa mazungumzo yao.

Balozi Mushy (katikati) akiendelea na mazungumzo na Bw. Kalenzi huku Bi. Jubilata Shao, Afisa Mambo ya Nje akinukuu mazungumzo hayo.

Balozi Mushy akiagana na Bw. Kalenzi mara baada ya mazungumzo yao.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.