Friday, May 31, 2013

Mhe. Membe awasilisha Hotuba ya Bajeti Bungeni

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akiwasilisha Bungeni Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwa Mwaka wa Fedha 2013/2014. Hotuba hiyo iliwasilishwa tarehe 30 Mei, 2013.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Mahadhi Juma Maalim (Mb.) akifuatilia kwa makini Hotuba ya Wizara ilipokuwa ikiwasilishwa Bungeni na Mhe. Membe (hayupo pichani)


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John Haule (wa sita mstari wa mbele) akiwa na Naibu Katibu Mkuu, Balozi Rajabu Gamaha (kushoto kwa Katibu Mkuu) pamoja na Wakuu wa Idara, Vitengo na Taasisi za Wizara wakifuatilia kwa makini mwenendo wa Bunge mjini Dodoma.

Wakurugenzi wengine kutoka Wizarani na Taasisi wakiwa Bungeni Mjini Dodoma

Baadhi ya Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini na Wageni wengine wakifuatilia kwa makini Hotuba ya Mhe. Membe (hayupo pichani) Bungeni leo akiwemo Mkuu wa Mabalozi na Balozi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Mhe. Juma Khalfan Mpango na Balozi wa Umoja wa Ulaya (EU), Mhe. Balozi Filberto Ceriani Sebregondi.

Baadhi ya Wanafunzi wanaosomea Shahada ya Uhusiano wa Kimataifa katika Chuo Kikuu cha Dodoma wakifuatilia Hotuba ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa iliyowasilishwa na Mhe. Membe.

Mhe. Juma Nkamia (Mb.), Mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akiwasilisha Hotuba kwa niaba ya Kamati hiyo huku Mhe. Membe na Mhe. Maalim wakifuatilia.

Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Job Ndugai (Mb.) akiahirisha Kikao cha Bunge leo tarehe 30 Mei, 2013.

Mhe. Membe akiwaeleza Mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini sababu zilizopelekea Kikao cha Bunge kuahirishwa.

Mhe. Membe akiteta jambo na Balozi Sebregondi.

Wananchi kutoka Vijiji mbalimbali vya Mkoa wa Lindi wakiwemo kutoka Jimbo la Mtama linalowakilishwa na  Mhe. Membe wakipata picha ya pamoja mara baada ya kusikiliza Hotuba ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Mhe. Membe akisalimiana na baadhi ya Wananchi kutoka Lindi.

Mhe. Maalim akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya wananchi kutoka Jimbo la Muyuni, Zanzibar waliofika Bungeni kufuatilia Hotuba ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushiririkiano wa Kimataifa

Picha zaidi za Mhe. Maalim na wananchi kutoka Jimbo la Muyuni, Zanzibar.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.