Tuesday, August 20, 2013

Katibu Mtendaji mpya wa SADC apokelewa kwa shangwe Wizara ya Mambo ya Nje


 

Mhe. Bernard K. Membe (Mb.), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akimlaki kwa furaha Katibu Mtendaji mpya wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika (SADC),  Mhe. Dkt. Stergomena Lawrence Tax mara baada ya kuwasili Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
 

Mhe. Membe akimkabidhi shada la maua Dkt. Tax kwa niaba ya Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje mara baada ya kuwasili Wizarani hapo.
 
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John Haule nae akimkarisha Dkt. Tax kwa furaha Wizarani.
 
Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Irene Kasyanju akimpongeza kwa shada la maua Dkt. Tax mara nbaada ya kuwasili Wizarani.
 
Mapokezi yakiendelea.
 
Dkt. Tax akipongezwa na kukaribishwa Wizarani na Naibu Katibu Mkuu, Balozi Rajabu Gamaha.
 
Balozi mpya  wa Tanzania nchini Ethiopia, Mhe. Naimi Aziz, nae pia aliungana na Wafanyakazi wa Wizara kumpongeza dkt. Tax. Anayeshuhudia pembeni ni Bw. Ali Mwadini, Katibu wa Naibu Waziri. 
 
Dkt. Tax akipongezwa na Bw. Omar Mjenga, Mkurugenzi Msaidizi, Idara ya Asia na Australasia huku Mkurugenzi wa Idara ya Sera na Mipango, Bw. James Lugaganya (kushoto) akishuhudia.
 
Balozi Bertha Semu-Somi, Mkurugenzi wa Diaspora akimlaki kwa shangwe Dkt. Tax wakati wa mapokezi.
 
Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati, Balozi Simba Yahya nae akitoa pongezi zake za dhati kwa Dkt. Tax
 
Maafisa mbalimbali wa Wizara nao pia walikuwa mstari wa mbele kumpongeza Dkt. Tax.
 
Dkt. Tax akisaini Kitabu cha Wageni mara baada ya mapokezi makubwa aliyoyapata kutoka kwa Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, huku Mhe. Membe akishuhudia.
 

Mhe. Membe akifurahia jambo na Makatibu Wakuu wakati Dkt. Tax akisaini Kitabu cha Wageni.

 
Picha na Reginald Philip.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.