Tuesday, June 12, 2018

Naibu Katibu Mkuu afanya mazungumzo na Mabalozi wa Uturuki, Algeria, Kuwait na Palestina.

Naibu Katibu Mkuu Balozi Ramadhan M. Mwinyi( wa kwanza kushoto) akiwasikiliza Mabalozi wa Uturuki, Palestina, Algeria na Kuwait ( hawapo pichani) walipomtembelea Wizarani tarehe 12 Juni,2018,Dar es Salaam. Kulia kwake ni Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati Bw. Suleiman Saleh na Mwisho ni Afisa Mambo ya Nje Bw. Fidelis Odiro wakifuatilia mazungumzo hayo. 
Pamoja na mambo mengine mazungumzo hayo yalijikita katika kujadili namna ya kuendelea kuboresha mahusiano yaliyopo kati ya Tanzania na nchi hizo. Pia walizungumzia kuhusu azimio la Baraza kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu haki za watu wa Palestine.
Balozi wa Algeria Mhe. Saad Belabeb(wa kwanza kushoto), Balozi wa Kuwait nchini Mhe.Jasem Ibrahim Al Najem, Balozi wa Palestine nchini Mhe.Hazem Shabat na mwisho ni Balozi wa Uturuki nchini Mhe.Ali Davutaglu wakimsikiliza Balozi Mwinyi (hayuko pichani) katika mazungumzo hayo.

Wakiwa katika picha ya pamoja baada ya mazungumzo.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.