Monday, June 25, 2018

Washindi wa TBL watembelea Ubalozi wa Tanzania nchini Urusi

Balozi wa Tanzania nchini Urusi Mhe. Simon Mumwi amekutana na Washindi wa shindano la Tanzania Breweries Ltd. kupitia bia rasmi ya Kombe la Dunia - Kilimanjaro Premium Lager siku chache mara baada ya kuwasili jijini Moscow Urusi, kwa ajili ya kushuhudia Mechi za Kombe la Dunia zinazoendelea nchini humo.

 Pichani katikati ni Balozi Mumwi, 
watatu kutoka kulia ni Bw. Charles John, wa pili kutoka kulia ni Afisa Mwandamizi wa Ubalozi wa Tanzania nchini Urusi Dkt. Mkama, na wa kwanza kulia ni Joel Terry. 
Wa kwanza kushoto ni Bw. Leodigard Isack,  Bw. Kironde Mwijage (wa pili kushoto), Bi. Mary Mushi (wa tatu kutoka kushoto),  wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuwasili ubalozini hapo.
Balozi Mumwi akifanya mazungumzo na washindi hao.
Balozi Mumwi akipokea zawadi ya Majani ya Chai yanayotengenezwa nchini Tanzania kutoka kwa mmoja wa washindi wa shindano hilo Bw. Leodigard Isack kwa niaba ya Kundi la Washindi wa Shindano la TBL kupitia bia ya Kilimanjaro Premium Lager, ambapo washindi hao walidhaminiwa safari ya Urusi kushuhudia mojawapo ya Mashindano ya Kombe la Dunia yanayoendelea nchini humo.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.