Tuesday, June 12, 2018

Balozi Chana pamoja na Balozi Mboweto wawasilisha Hati za Utambulisho.

Balozi wa Tanzania nchini Kenya Mhe. Pindi Chana akiwa katika picha ya pamoja na Rais wa Sudan ya Kusini Mhe. Salvar Kiir mara baada ya kuwasilisha Hati za utambulisho. Balozi Chana mwenye makaazi jijini Nairobi nchini Kenya pia anaiwakilisha Tanzania nchini Sudani Kusini.  


Balozi Mteule wa Tanzania nchini Nigeria Mhe. Muhidini Ally Mboweto, alikabidhi Hati za Utambulisho kwa Rais wa Shirikisho la Jamhuri ya Nigeria Mhe. Muhammadu Buhari. Hafla hiyo ilifanyika katika Ikulu ya nchi hiyo Jijini Abuja na kuhudhuriwa na Mkewa Mhe. Balozi Hajat Ashura Ally Mboweto, Maafisa wa Ubalozi na viongozi mbalimbali wa Serikali ya Nigeria.
Balozi Muhidin Ally Mboweto akisindikizwa na Mkuu wa Itifaki kuelekea eneo la gwaride.
Balozi wa Tanzania nchini Nigeria Mhe. Muhidin Ally Mboweto akipigiwa wimbo wa Taifa na tayari kwa ukaguzi wa gwaride.
Ukaguzi wa gwaride
Balozi Mboweto akisaini kitabu cha wageni alipowasili Ikulu ya Nigeria tayari kwa kukabidhi Hati za Utambulisho kwenye taifa hilo.
Rais wa Shirikisho la  Jamhuri ya Nigeria Mhe. Muhammadu Buhari akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi Muhidin Ally Mboweto kama Balozi wa Tanzania nchini Nigeria.
Mhe. Buhari akizungumza na Balozi Mboweto mara baada ya kuwasilisha Hati za Utambulisho. 






No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.