Friday, June 22, 2018

Naibu Katibu Mkuu afanya mazungumzo na Balozi wa Kuwait


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Ramadhani M.Mwinyi akisalimiana na Balozi wa Kuwait nchini Mhe.Jasem Ibrahim Al-Najem, alipomtembelea Wizarani tarehe 22 Juni,2018, Dar es Salaam.

Pamoja na mambo mengine walizungumzia kuhusu jinsi ya kuboresha mahusiano yaliyopo katika kati ya Tanzania na Kuwait, nchi ya Kuwait imekuwa ni kati ya wadau muhimu wa Maendeleo hapa nchini kupitia mradi wa Mfuko wa Maendeleo wa Kuwait(Kuwait Fund).

            Mhe. Al-Najem akifafanua jambo katika mazungumzo hayo.

 Balozi Mwinyi akisisitiza jambo katika mazungumzo hayo.
 Mazungumzo yakiendelea, wanaofuatilia kulia kwa Balozi Mwinyi ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Mashariki ya Kati Bw. Suleiman Salehe, Bw. Hangi Mgaka na Bw. Fidelis Odilo Maafisa wa Mambo ya Nje, wakifuatilia mazungumzo hayo.
Wakiwa katika picha ya pamoja baada ya mazungumzo.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.