Thursday, May 21, 2020

WATANZANIA 119 KUTOKA DUBAI WAREJEA NCHINI, KUISHUKURU SERIKALI


Serikali ya Tanzania imewarejesha nchini watanzania 119 ambao walikuwa wamekwama Abu Dhabi (Dubai) kufuatia kuzuiwa kwa safari za ndege kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa homa kali ya mapafu inayosabishwa na virus vya corona (COVID-19).

Ndege ya fly Dubai imewarejesha watanzania hao waliokuwa wamekwama Abu Dhabi (Dubai) tangu 25 Machi 2020 Serikali ya Falme za Kiarabu ilipotoa zuio la kuingia na kutoka kwa ndege.

Ndege hiyo imewasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) saa 8 mchana leo Alhamisi tarehe 21 Mei 2020 ikiwa na watanzania 119.

Kabla ya ndee hiyo kuwasili katika uwanja wa ndee wa Kimataifa wa Julius Nyerere, wazazi, ndugu, jamaa na marafiki wa watanzania hao walionekana wakiwa na nyuso za furaha na shauku ya kuonana na ndugu zao.

"Tunashukuru Serikali yetu ya Tanzania kwa kuweza kuturejesha nyumbani….binafsi namshukuru sana sana Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli kwa juhudi za kuturejesha, pia naushukuru ubalozi wa Tanzania katika Falme za Kiarabu kwa msaada wa hali na mali pamoja na nchi ya Falme za Kiarabu na watanzania kwa umoja na upendo kwani wengine tulikuwa hatuna fedha ya tiketi lakini kwa umoja tumeweza kuchangiwa na kurejea tena nchini kwetu," Amesema Mohhamed Juma Omary.

Kwa Upande wake, Bi. Christina Magige ambaye alikuwa amekwama Dubai kwa miezi mitatu ameipongeza Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na Serikali ya Falme za Kiarabu kwa kuweza kutoa ndege ambayo imeweza kuwarejesha nyumbani.

"Nampongeza sana Serikali yanu ya Tanzania kwa kuweza kufungua viwanja vya ndege ambapo kwa kufanya hivyo imetusaidia sisi watanzania tuliokuwa nje ya nchi kuweza kurejea nchini leo tunamshukuru sana, amesema bi. Magige.

Tarehe 15 Mei, 2020 jumla ya watanzania 246 waliokuwa wamekwama katika miji mbalimbali nchini India kutokana na zuio la kuingia na kutoka ndege za Kimataifa lililowekwa na Serikali ya India kama hatua mojawapo ya kudhibiti kuenea kwa maambukizi ya ugonjwa wa COVID-19 walirejea nchini.

Ndege ya flydubai iliyowarejesha watanzania 119 nchini kutoka Abu Dhabi (Dubai) ikitua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) leo jijini Dar es Salaam

Baadhi ya watanzania waliokuwa wamekwama Dubai wakishuka kwenye ndege ya flydubai mara baada ya ndee iyo kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) leo jijini Dar es Salaam

Baadhi ya watanzania waliokuwa wamekwama Dubai wakishuka kwenye ndege ya flydubai mara baada ya ndee iyo kutua katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) leo jijini Dar es Salaam

Baadhi ya watanzania waliokuwa wamekwama Dubai wakiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) leo jijini Dar es Salaam

Baadhi ya watanzania waliokuwa wamekwama Dubai wakiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) leo jijini Dar es Salaam

Baadhi ya watanzania waliokuwa wamekwama Dubai wakiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) leo jijini Dar es Salaam



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.