Friday, September 4, 2020

Naibu Katibu Mkuu aongoza Ujumbe wa Tanzania kwenye majadiliano ya biashara baina ya EAC na Uingereza

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Mwinyi Talib Haji akifuatilia kikao cha  kuajadili namna bora ya kuendelea na majadiliao ya biashara baina ya Afrika Mashariki na Uingereza kilichokuwa kikiendelea kwa njia ya mtandao (Video Conference).

Dkt. Haji ameongoza ujumbe wa Tanzania kwenye kikoa cha Kanda cha Makatibu Wakuu wa Jamuiya ya Afrika Mashariki kujadili namna bora ya kuendelea na majadiliano ya biashara baina ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Uingereza.

Lengo la majadiliano baina ya Afrika Mashariki na Uingereza ni kuwa na Mkataba wa Biashara utakaowezesha Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kuuza bidhaa kwenye Soko la Uingereza na Uingereza kwenye Soko la Jumuiya ya Afrika Mashariki kuanzia tarehe 01 Januari, 2021.

Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa muda mrefu imekuwa mshirika mzuri wa biashara kwa nchi ya Uingereza. Hata biashara hiyo biashara hiyo awali imekuwa ikifanyika kwa kufuata sheria, miongozo na taratibu za Umoja wa Ulaya. Kufauatia hatua ya Uingereza kujitoa katika Umoja wa Ulaya imeenda sera na mwongozo mpya utakao  ifanya nchi hiyo kuendelea kufanya biashara na Mataifa mbalimbali. 


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Mwinyi Talib Haji akiachangia  hoja wakati wa kikao.
Kikao kikiendelea 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.