Wednesday, September 2, 2020

KATIBU MKUU WA MAMBO YA NJE AFANYA MAZUNGUMZO NA MRATIBU MKAZI WA UMOJA WA MATAIFA NCHINI

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brigedia Generali Wilbert A. Ibuge akizungumza na Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini,
Bw. Zlatan Milišić
 alipomtembelea Ofisini kwake jijini Dodoma tarehe 2 Septemba 2020.

Katika mazungumzo yao walijadili masuala mbalimbali ya ushirikiano kati ya Tanzania na Shirika la Umoja wa Mataifa ambapo Balozi Ibuge alitoa shukrani kwa Shirika hilo kwa ushirikiano uliopo kati yake na Serikali hususan kwenye masuala mbalimbali ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii. Kwa upande wake, Bw. 
Milišić aliipongeza Tanzania kwa kudumisha amani na utulivu ambao ni chanzo cha uchumi wa nchi kustawi. Pia aliipongeza kwa kuendelea kuchangia vikosi vya ulinzi wa amani kwenye mataifa mbalimbali  yenye  migogoro duniani na kuitakia Tanzania uchaguzi wa amani na utulivu hapo mwezi Oktoba 2020.

Ujumbe wa Wizara ukimjumuisha Bw. Hangi Mgaka, Katibu wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Bi. Prisca Mwanjesa, Afisa Mambo ya Nje wakifuatilia mazungumzo kati ya Balozi Ibuge na Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini, Bw. Milišić (hawapo pichani)

Mazungumzo yakiendelea
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ibuge akiwa katika picha ya pamoja na Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa nchini, Bw. Milišić mara baada ya kukamilisha mazungumzo yao.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ibuge akiagana na Mratibu Mkazi wa Umoja wa Mataifa hapa nchini, Bw. Milišić mara baada ya mazungumzo kati yao.

 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.