Friday, September 18, 2020

TANZANIA YAKABIDHIWA HATI MILIKI YA ARDHI NA SERIKALI YA INDIA

Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Baraka Luvanda akiweka saini hati miliki ya ardhi ya jengo la Ubalozi, jijini New Delhi tarehe 17 Septemba 2020.

Naibu Afisa Mkuu wa Ardhi wa Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Miji ya India, Bw. Satish Kumar Singh akimkabidhi Balozi wa Tanzania nchini India, Mhe. Baraka Luvanda hati miliki ya ardhi ya jengo la Ubalozi, jijini New Delhi tarehe 17 Septemba 2020.

Picha ya jengo la Ubalozi wa Tanzania Jijini New Delhi, India.
=========================================

TANZANIA YAKABIDHIWA HATI MILIKI YA ARDHI MJINI NEW DELHI.

Ubalozi wa Tanzania nchini India umekabidhiwa rasmi na Serikali ya India Hati Miliki ya Ardhi yenye ukubwa wa eneo la mita za mraba 2120.60 ambapo ndipo lilipo jengo la Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania jijini New Delhi.

Akipokea hati hizo wakati wa hafla fupi ya makabidhiano iliyofanyika katika Ofisi za Wizara ya Nyumba na Maendeleo ya Miji ya India tarehe 17 Septemba 2020, Balozi wa Tanzania nchini humo, Mhe. Baraka H. Luvanda ameishukuru Serikali ya India kwa hatua hiyo ambayo inathibitisha uhusiano mzuri uliojengeka kati ya nchi hizi mbili.

Kwa upande wake, Naibu Afisa Mkuu wa Ardhi wa Wizara ya Nyumba na Maendeleo ya Miji ya India, Bw. Satish Kumar Singh amesifu uhusiano mzuri wa kihistoria uliopo kati ya India na Tanzania na kueleza kuwa, hiyo ndiyo sababu India imeona fahari kubwa kuipa Tanzania umiliki wa eneo katika sehemu mahsusi ya Jumuiya ya Kidiplomasia (Diplomatic Enclave).

Ni sera na mkakati wa Serikali ya Tanzania ya kuhakikisha kuwa, Balozi zote zilizopo katika maeneo ya kimkakati zinakuwa na majengo na nyumba za watumishi ili kuipunguzia Serikali gharama kubwa za kupanga majengo na nyumba hizo. Katika hafla hiyo Balozi Luvanda aliambatana na maofisa ubalozi, Bibi Natihaika Msuya na Dkt. Kheri Goloka.

 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.