Friday, December 4, 2020

WIZARA YA MAMBO YA NJE YAJIPANGA KUWAJENGEA UWEZO WA KAZI WATUMISHI WAKE

Mkurugenzi wa Kitengo cha Dispora katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Anisa Mbega akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Brig. Gen. Wilbert Ibuge wakati wa ufunguzi rasmi wa Awamu ya Kwanza ya  Mafunzo Maalum kwa Maafisa Waandamizi wa Wizara kuhusu Utaalamu katika Uchambuzi wa masuala mbalimbali (Analytical Skills). Mafunzo hayo yanalenga kuwajengea uwezo Maafisa hao ili kuboresha utendaji kazi wao wa kila siku. Kadhalika, Mafunzo hayo ambayo yalifanyika jijini Dodoma hivi karibuni, yaliandaliwa na Wizara kwa kushirikiana na Taasisi ya UONGOZI na Shirika la UNDP.

Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Mizengo Peter Pinda akizungumza na mmoja wa Washiriki wa Mafunzo hayo alipotembelea eneo hilo akiwa kwenye shughuli zake za ujenzi wa Taifa na kuwasalimia Washiriki 

Sehemu ya Washiriki wa Mafunzo ya Utaalam katika Uchambuzi wakifurahia jambo

Washiriki wengine wakiwa tayari kuanza kujifunza mbinu mbalimbali za kufanya uchambuzi

Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Bw. Kadari Singo akiwasilisha Mada kwa Washiriki kuhusu "Umuhimu wa Uchambuzi katika Kufanya Maamuzi".

Sehemu ya Washiriki wakimsikiliza Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya UONGOZI, Bw. Singo (hayupo pichani) 

Sehemu nyingine ya Washiriki wakifuatilia mafunzo

Mwezeshaji kutoka Taasisi ya UONGOZI, Bibi Zuhura Muro akiwasilisha Mada kwa Washiriki kuhusu "Umuhimu wa Kutumia Akili Hisia (Emotional Intelligence) katika Uongozi". 

Mmoja wa Washiriki, Bw. Suleiman Magoma akichangia jambo wakati wa mafunzo hayo

Mwezeshaji kutoka Taasisi ya UONGOZI, Prof. Joseph  akiwasilisha Mada kwa Washiriki kuhusu "Umuhimu wa Uchambuzi katika Kutafuta Suluhisho la Matatizo mbalimbali".

Mmoja wa Washiriki, Bw. Ismail akieleza jambo kwa Washiriki wenzake ikiwa ni sehemu ya Washiriki kufanyia kazi yale waliyojifunza 

Washirki wakiwa kwenye mjadala

Sehemu nyingine ya Washiriki wa Mafunzo hayo.

 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.