Wednesday, December 8, 2021

WAZIRI MULAMULA AKUTANA KWA MAZUNGUMZO NA VIONGOZI MBALIMBALI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula leo tarehe 08 Disemba 2021 amekutana kwa nyakati tofauti na kufanya mazungumzo na Viongozi kutoka nchi mbalimbali ambao wapo nchini kwa ajili ya kushiriki maadhimisho ya miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara yatakayofanyika jijini Dar es Salaam tarehe 09 Desemba 2021.

Miongoni mwa Viongozi aliokutana nao ni pamoja na Rais Mstaafu wa Malawi, Mhe. Dkt. Joyce Banda, Waziri wa Mambo ya Nje wa Msumbiji, Mhe. Veronica Macamo, Waziri wa Mambo ya Nje wa Eswatini, Mhe. Seneta Thulisile Dladla na Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda, Mhe. Dkt. Vicent Biruta.

Katika mazungumzo yao, Mhe. Balozi Mulamula amewakaribisha nchini  viongozi hao na kuwashukuru kwa kukubali mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan wa kuja kushiriki maadhimisho hayo pamoja na wananchi wa Tanzania. Kadhalika, viongozi hao wamekubaliana kuimarisha ushirikiano kati ya nchi zao na Tanzania kwenye maeneo mbalimbali.

Rais Mstaafu wa Malawi, Mhe. Dkt. Joyce Banda akiwa katika mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula jijini Dar es Salaam


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje wa Msumbiji, Mhe. Veronica Macamo katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam  


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje wa Eswatini, Mhe. Seneta Thulisile Dladla katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda, Mhe. Dkt. Vicent Biruta katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Balozi wa Rwanda nchini Tanzania Mhe. Meja Jenerali Charles Karamba.    



No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.