Thursday, December 9, 2021

RAIS KENYATTA AWASILI NCHINI KUSHIRIKI MAADHIMISHO YA MIAKA 60 YA UHURU NA KUANZA ZIARA RASMI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akimtambulisha Balozi wa Tanzania nchini Kenya, Mhe. Dkt. John Simbachawene kwa Rais wa Jamhuri ya Kenya, Mhe. Uhuru Kenyatta wakati wa mapokezi ya Mhe. Rais Kenyatta alipowasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimaifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam tarehe 09 Desemba 2021 kwa ajili ya kushiriki maadhimisho ya miaka 60 ya uhuru wa Tanzania Bara pamoja na kuanza ziara rasmi ya siku mbili nchini.


Mhe. Rais Kenyatta akisalimiana na Balozi wa Kenya hapa nchini, Mhe. Dani Kazungu wakati wa hafla ya mapokezi yake
Mhe. Balozi Mulamula akiendelea na zoezi la utambulisho wa viongozi mbalimbali  wa hapa nchini  waliofika kumpokea Mhe. Rais Kenyatta 

Mhe. Rais Kenyatta akisalimiana na Bi. Felister Rugambwa, Afisa Mambo ya Nje na Mkuu wa Utawala katika Ubalozi wa Tanzania nchini Kenya ambaye yupo nchini kushiriki ziara ya Rais.

Gwaride la Heshima

Mhe. Rais Kenyatta akiwa ameongozana na Mhe. Balozi Mulamula wakipita katikati ya gwaride maalum lililoandaliwa kwa  heshima yake.

Mhe. Rais Kenyatta akiwa kwenye mazungumzo na Mhe. Balozi Mulamula mara baada ya kuwasili nchini

Mazungumzo yakiendelea. Kushoto ni Waziri wa Mambo ya Nje wa Kenya, Mhe. Raychaelle Omamo pamoja na Balozi wa Kenya nchini, Mhe. Dani Kazungu.
























No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.