Thursday, December 9, 2021

RAIS SAMIA AWAONGOZA WATANZANIA SHEREHE ZA MAADHIMISHO YA MIAKA 60 YA UHURU

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan amewaongoza Watanzania kwenye sherehe za Maadhimisho ya Miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara yaliyofanyika katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Marais na viongozi wa Mataifa mbalimbali pamoja na viongozi wakuu wa Serikali.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwasalimia Watanzania kwenye sherehe za maadhimisho ya Miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara yaliyofanyika katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam  


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Rais wa Jamhuri ya Rwanda, Mhe. Paul Kagame katika sherehe za maadhimisho ya Miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara yaliyofanyika katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam  


Rais wa Jamhuri ya Rwanda, Mhe. Paul Kagame akisalimiana na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Philip Mpango katika sherehe za maadhimisho ya Miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara yaliyofanyika katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam  


Rais wa Jamhuri ya Rwanda, Mhe. Paul Kagame akisalimiana na Rais Mstaafu wa Awamu ya nne Mhe. Jakaya Kikwete katika sherehe za Maadhimisho ya Miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara yaliyofanyika katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam    


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Hussein Ali Mwinyi akiwasili katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam kuhudhuria sherehe za maadhimisho ya Miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara  


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akihutubia wananchi katika sherehe za maadhimisho ya Miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara yaliyofanyika katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam   


Baadhi ya Mawaziri na Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi Pamoja na Viongozi waandamizi wa Serikali wakifuatilia maadhimisho ya Miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara yaliyofanyika katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam 


Baadhi ya Makatibu Wakuu wakifuatilia maadhimisho ya Miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara yaliyofanyika katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam 

Baadhi ya Mabalozi na Wakuu wa Mashirika ya Kimataifa wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini wakifuatilia maadhimisho ya Miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara yaliyofanyika katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam 




Sehemu ya Mawaziri wakifuatilia maadhimisho ya Miaka 60 ya Uhuru wa Tanzania Bara yaliyofanyika katika uwanja wa Uhuru Jijini Dar es Salaam 





No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.