Tuesday, December 7, 2021

WAZIRI MULAMULA APOKEA HATI ZA UTAMBULISHO ZA MKURUGENZI MKAZI WA FAO

Na Mwandishi wetu, Dar

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) amepokea Hati za Utambulisho za Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) Dkt. Nyabenyi Tipo katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam.

Mara baada ya kupokea hati hizo Balozi Mulamula ametumia fursa hiyo kumweleza Mkurugenzi Mkazi huyo vipaumbele vya Serikali katika mpango mzima wa kuendeleza kilimo pamoja na mpango Mkakati wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa ‘Strategic Development Cooperation programme’.

Pia viongozi hao wameangalia maeneo ambayo yatapewa kipaumbele katika uwekezaji wa miundombinu, uzalishaji zaidi lakini pia kuangalia jinsi gani mazao yanayolimwa yanatunzwa vizuri.

“Tumejadili mbalimbali ikiwa ni pamoja na mpango wa FAo wa kusaidia nchi kuwa na bidhaa zinazozitambulisha nchi husika katika masoko ya kimataifa,” amesama Balozi Mulamula.

Pamoja na mambo mengine, Balozi Mulamula amemhakikishia Mkurugenzi Mkazi wa FAO kuwa Tanzania itaendelea kushirikiana kwa karibu na FAO katika kutekeleza miradi mbalimbali hasa mradi wa maendeleo wa miaka mitano.

Kwa Upande wake, Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) Dkt. Nyabenyi Tipo amesema atahakikisha FAO inatekeleza vipaumbele vya Serikali ya Tanzania pamoja na kuongeza ushirikiano wake kwa maslahi ya pande zote mbili.

“Mara baada ya kuwasilisha Hati za Utambulisho kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, tumejadili jinsi ya kusaidia kupunguza athari za mabadiliko ya tabia nchi, kupunguza utapiamlo na kuona ni jinsi gani FAO inaweza kusaidia Tanzania katika kuboresha lishe kwa watanzania na changamoto mbalimbali zinazoikabili sekta ya kilimo kwa ujumla,” amesema Dkt. Tipo

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (Mb) akipokea Hati za Utambulisho za Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) Dkt. Nyabenyi Tipo katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akiongea na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) Dkt. Nyabenyi Tipo katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam


Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) Dkt. Nyabenyi Tipo akimueleza jambo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula mara baada ya kumkabidhi Hati za Utambulisho katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam


Mwakilishi Msaidizi wa FAO Bwana Charles Tulahi akieleza jambo wakati wa kikao baina ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) Dkt. Nyabenyi Tipo katika Ofisi ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa (FAO) Dkt. Nyabenyi Tipo wakiwa katika picha ya pamoja na badhi ya maafisa kutoka Wizarani pamoja na Ofisi za FAO 




No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.