Friday, February 11, 2022

Balozi Kilima ateta na Wawekezaji kutoka Ujerumani

Balozi wa Tanzania nchini Oman, Mhe. Abdallah Kilima amefanya mazungumzo na wawekezaji wa nishati ya jua kutoka Oman jijini Muscat hivi karibuni.
Wawekezaji hao ambao ni Dkt. Michael Voch na Bw. Claus Heim kutoka Ujerumani na Bw. Khalid Hamdoun M. Aljabri  na Bw. Mohammed Al Riyami kutoka Taasisi ya  IGD ya Oman wanakusudia kuwekeza katika sekta ya uzalishaji wa nguvu ya umeme wa kutumia Jua kwa teknolojia mpya inayoitwa Solar Container. Teknolojia hiyo inatumua maji kuzalisha hydrojen ambayo ndiyo inayotoa umeme na oxygen kama mabaki ya uzalishaji (byproducts)
Teknolojia hiyo tayari inatumika katika nchi za Ulaya na hivi karibuni itaanzishwa nchini Oman inaweza kutosheleza nyumba 200 Kwa kontena moja na pia inaweza kuunganishwa na Gridi ya Taifa
Wawekezaji hao pia wanakusudia kuanzisha miradi ya kilimo inayotumia Teknolojia ya Hydroponic system ambacho kinatunia eneo dogo lakini tija kubwa.
Wawekezaji imeiomba Serikali ya Tanzania kuwapatia eneo la uwekezaji pamoja na kuunganishwa na makampuni yatakayoweza kununua bidhaa watakazozalisha kama wanavyofanya nchini UAE, waneingia mkataba na Shirika la Ndege la Emirate kununua bidhaa za vyakula watakavyozalisha.
Kwa upande wake, Mhe. Balozi aliwaeleza wawekezaji hao kwamba Tanzania inakarubisha uwekezaji katika sekta ya uzalishaji wa nguvu za umeme wa kutumia Jua kwani ni nishati mbadala na rahisi kutumika. Kwa upande wa mradi wa kilimo cha hydroponic, Mhe. Balozi alieleza kwamba kilimo hicho kinaweza kuwa mkombozi wa kilimo cha kutegemea mvua ambacho huwa ni cha msimu. Hivyo mradi huo unaweza kuongeza uzalishaji na kupata ziada ya kuuza nje ya nchi. 

Balozi wa Tanzania nchini Oman, Mhe. Abdallah Kilima akizungumza na wawekezaji kutoka Ujerumani. Kulia Kwake ni Dkt. Michael Voch na Bw. Claus Heim

 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.