Tuesday, February 8, 2022

RAIS WA BENKI YA MAENDELEO YA AFRIKA (AFDB) DKT. ADESINA AWASILI DODOMA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula akisalimiana na Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina alipowasili katika uwanja wa ndege wa Dodoma akiwa katika ziara ya kikazi ya siku tatu nchini.

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akisalimiana na Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina alipowasili katika uwanja wa ndege wa Dodoma akiwa katika ziara ya kikazi ya siku tatu nchini.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki BaloziLiberata Mulamula (katikati) akizungumza na Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina (kushoto) huku Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk (kulia) akiwasikiliza wakati Dkt. Adesina alipowasili katika uwanja wa ndege wa Dodoma.


Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina (wa pili kushoto) akizungumza na wenyeji wake waliompokea katika Uwanja wa ndege Dodoma alipowasili katika uwanja wa ndege wa Dodoma huku Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Mwigulu Nchemba (kushoto) na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula (kulia) wakifuatilia mazungumzo hayo.




Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Akinwumi Adesina awasili jijini Dodoma akiwa katika ziara ya kikazi ya siku tatu nchini. Katika uwanja wa ndege wa Dodoma Dkt. Adesina amepokelewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Liberata Mulamula na Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Mwigulu Nchemba.

Dkt. Adesina yuko nchini kwa ziara ya siku tatu ambapo tarehe 09 February 2022 atashiriki katika uzinduzi wa ujenzi wa barabara za mzunguko zinazojengwa katika jiji la Dodoma utakaofanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan.

Ujenzi wa barabara hizo za mzunguko zenye urefu wa kilomita 112.3 unagharamiwa kwa pamoja kati ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na benki hiyo. Ujenzi wa barabara hizo utalifanya jiji la Dodoma kuwa na barabara za aina yake katika ukanda wa Afrika Mashariki na Kati.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.