Tuesday, February 8, 2022

WAZIRI MULAMULA AONGOZA UJUMBE WA TANZANIA KWENYE MKUTANO WA 46 WA DHARURA WA BARAZA LA MAWAZIRI WA EAC


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula, akiwa jijini Dodoma ameongoza ujumbe wa Tanzania kushiriki katika Mkutano wa 46 wa Dharura wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

Mkutano huu wa dharura umeitishwa kwa lengo la kujadili ripoti ya majadiliano yaliyofanyika tarehe 15 hadi 24 Januari 2022 jijini Nairobi, Kenya kati ya Jumuiya ya Afrika Mashariki na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kuhusu Nchi hiyo kujiunga na Jumuiya. 

Pamoja na muasula mengine yaliyojadiliwa Mkutano umekubaliana kuendelea kufanyia kazi kwa wakati hoja za pande zote mbili za majadiliano (EAC na Congo DRC), na kuandaa taarifa itakayowasilishwa kwa Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ili kuharakisha uridhiaji wa maombi ya DRC

Mkutano huu wa dharura ambao umefanyika kwa njia ya mtandao umehudhuriwa na Nchi zote wanachama wa Jumuiya na kuongozwa na Mwenyekiti wa Baraza hilo Waziri anayesimamia masuala ya Mtangamano wa Afrika Mashariki Mhe. Adam Mohamed kutoka nchini Kenya. 

Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo iliwasilisha maombi ya kujiunga na Jumuiya ya Afrika Mashariki tarehe 4 Juni 2019. 
Mkutano ukiendelea
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula, Katibu Mkuu Balozi Joseph Sokoine (katika) na Mkurugenzi wa Siasa, Ulinzi na Usalama Balozi Stephen Mbundi wa Wizara hiyo wakifuatilia Mkutano wa 46 wa Dharura wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliokuwa ukiendelea
Ujumbe wa Tanzania ukifuatilia Mkutano wa 46 wa Dharura wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki uliokuwa ukiendele
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akifuatilia mjadala uliokuwa ukiendelea kwenye Mkutano wa 46 wa Dharura wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Liberata Mulamula akichangia hoja kwenye Mkutano wa 46 wa Dharura wa Baraza la Mawaziri wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ulifanyika kwa njia ya mtandao.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.