Wednesday, October 28, 2015

Rais Kikwete apokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Mabalozi wa Misri, Singapore, Israel na Ufilipino

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (kushoto) akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Ufilipino nchini Tanzania mwenye makazi nchini Kenya,  Mhe. Bayani V. Mangibin. Hafla hiyo imefanyika Ikulu Dar es Salaam tarehe 28 Oktoba, 2015. 
Balozi Mangibin akizaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili Ikulu Jijini Dar es Salaam
Balozi Mangibin (kulia) akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberatta Mulamula (kushoto) mara baada ya kuwasilisha Hati za Utambulisho kwa Mhe. Rais Jakaya Kikwete (katikati mwenye tai nyekundu)
Balozi Mangibin (kulia) akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Khatibu Makenga (wa kwanza kushoto) alipokuwa akitambulishwa na Mhe. Rais. 
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga (wa kwanza kushoto) akisalimiana na Balozi Mangibin (kulia).
Mhe. Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Mangibin.
Picha ya pamoja

=========Balozi wa Singapore
Balozi wa Singapore nchini Tanzania, Mhe. Tan Puay Hiang akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili Ikulu kwa ajili ya kuwasilisha Hati zake za Utambulisho kwa Mhe. Rais.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete (kushoto) akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi wa Singapore mwenye kazi yake nchini Singapore,  Mhe. Tan Puay Hiang (kulia)
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberatta Mulamula (kushoto) akisalimiana na Balozi Tan Puay Hiang (kulia)
Mhe. Rais Kikwete akizungumza na Balozi Hiang mara baada ya kupokea hati zake za utambulisho kama Balozi mpya wa Singapore hapa nchini. Kushoto ni Afisa aliyefuatana na Balozi Hiang.

.......Balozi wa Misri 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akipokea Hati za Utambulisho kutoka kwa Balozi mpya wa Misri hapa nchini, Mhe. Yasser Ahmed Al Eldin Elshawaf. Hafla hiyo imefanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 28 Oktoba, 2015.
Mhe. Rais Kikwete akimkaribisha Balozi Elshawaf.
Mhe. Rais Kikwete akimtambulisha kwa Balozi Elshawaf, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula.
Balozi Elshawaf akisalimiana na Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Samwel Shelukindo 
Balozi Elshawaf akisalimiana na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. 
Picha ya pamoja
Mhe. Rais Kikwete akiwa kwenye mazungumzo na Balozi mpya wa Misri hapa nchini Mhe. Elshawaf
Mazungumzo yakiendelea

......Balozi wa Israel

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akisalimiana na Balozi mpya wa Israel hapa nchini mwenye Makazi yake nchini Kenya, Mhe. Yahel Vilan mara baada ya kupokea Hati zake za utambulisho. Hafla hiyo imefanyika Ikulu, Dar es Salaam tarehe 28 Oktoba, 2015.
Mhe. Rais Kikwete akimtambulisha kwa Balozi Vilan, Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula.
Balozi Vilan akisalimiana na Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Elibariki Maleko.
Balozi Vilan akisalimiana na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga
Balozi Vilan akisalimiana na Bw. Batholomeo Jungu, Afisa Mambo ya Nje
Mhe. Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Vilan
Mhe. Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Vilan na Balozi Mulamula
Balozi Elshawaf (katikati) akipokea heshima ya wimbo wa taifa mara baada ya kuwasili Ikulu. Kulia ni Mkuu wa Itifaki Balozi Juma Maharage na kushoto Mnikulu.
Bendi ya polisi ikipiga wimbo wa taifa wa Misri kwa heshima ya Balozi Elshawaf
Balozi Elshawaf akisalimiana na Bw. Celestine Kakele, Afisa Mambo ya Nje
Balozi Elshawaf akisalimiana na Kiongozi wa Bendi ya Polisi
Picha na Reginald Philip

Taarifa kwa Vyombo vya Habari - Uhamisho wa Kituo

Balozi Peter A. Kallaghe 


Mheshimiwa Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amemuhamisha kituo Balozi Peter A. Kallaghe aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Uingereza kwenda kuwa Balozi wa Tanzania nchini Brazil.

Uhamisho huo unaanzia tarehe 23 Oktoba, 2015.


Imetolewa na:
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,
Dar es Salaam

28 Oktoba, 2015

Tuesday, October 27, 2015

Timu za Waangalizi za AU, SADC na Jumuiya ya Madola waisifu Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

Kiongozi wa Timu ya Waangalizi wa Uchaguzi Mkuu wa Tanzania kutoka Umoja wa Afrika (AU), ambaye pia ni Rais Mstaafu wa Msumbiji Mhe. Armando Emilio Guebuza, akitoa ripoti ya timu hiyo mbele ya Waandishi wa Habari na Mabalozi mbalimbali wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini  tarehe 27 Oktoba, 2015 katika Hoteli ya White Sands Jijini Dar es Salaam.
Pamoja na mambo mengine, timu hiyo ya Waangalizi ya Umoja wa Afrika (AU) imeisifu Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kwa kuendesha uchaguzi katika hali ya haki na uwazi bila upendeleo wowote.
Kamishna anayeshughulikia masuala ya Siasa katika Kamisheni ya Umoja wa Afrika, Dkt. Aisha Abdulahi nae akizungumza wakati wa uwasilishaji ripoti ya Umoja huo kuhusu Uchaguzi Mkuu wa hapa nchini.
Baadhi ya Waheshimiwa Mabalozi  wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini wakimpigia makofi kiongozi wa timu ya Waangalizi ya Afrika Mhe. Armando Guebuza (hayupo pichani).
Kiongozi wa Timu ya Waangalizi wa Uchaguzi Mkuu kutoka  Jumuiya ya Madola, ambaye pia ni Rais Mstaafu wa Nigeria, Mhe. Goodluck Jonathan akitoa ripoti ya timu yake  mbele ya Waandishi wa Habari na Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini tarehe 27Oktoba, 2015 katika Hoteli ya White Sands jijini Dar es Salaam.
Mheshimiwa Goodluck Jonathan ameisifu Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Vyombo vya Dola, Wagombea, Viongozi wa vyama vya siasa pamoja na Watanzania wote kwa ujumla kwa kuendesha uchaguzi katika mazingira ya haki, uwazi na amani.
Mkurugenzi wa Idara ya Afrika, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Samwel Shelukindo (katikati), Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bi. Mindi Kasiga (kulia) pamoja na Afisa wa Wizara hiyo Bw. Celestine Kakere, wakifuatilia ripoti hizo.
Baadhi ya Waheshimiwa Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini wakifuatilia ripoti ya kiongozi wa timu ya Waangalizi ya Jumuiya ya Madola Mhe. Goodluck Jonathan.
Wajumbe wa timu za Waangalizi wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC)Umoja wa Afrika (AU) na Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Madola nao wakifuatilia Ripoti ya Mhe. Goodluck Jonathan.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Msumbiji ambaye pia ndiye Kiongozi wa Timu ya Waangalizi wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), Mhe. Oldemiro Baloi naye akitoa taarifa ya timu yake ya uangalizi wa Uchaguzi Mkuu hapa nchini tangu kipindi cha kampeni hadi siku ya uchaguzi.

Baadhi ya Waheshimiwa Mabalozi  wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini wakifuatilia ripoti ya kiongozi wa timu ya waangalizi ya SADC.
Mkutano huo ukiendelea.
Waheshimiwa Mabalozi wakiendelea kufuatili uwasilishwaji wa ripoti hizo za waangalizi wa Kimataifa wa Uchaguzi Mkuu nchini Tanzania.

Mmoja wa Waandishi wa Habari akiuliza swali juu ya ripoti hizo.
Waandishi wa Habari wakiendelea kuwajibika kuchukua kila kinachoelezwa na timu hizo za kimataifa za waangalizi wa Uchaguzi Mkuu unaoendelea hapa nchini.
Mkutano ukiendelea.
===========================
PICHA NA: REUBEN MCHOME.

Jukwaa la Vijana wa ICGLR watembelea Wizara ya Mambo ya Nje

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula (katikati) akizungumza na wawakilishi kutoka Jukwaa la Vijana la Jumuiya ya Nchi za Ukanda wa  Maziwa Makuu (ICGLR Youth Forum) (hawapo pichani) walipofika Wizarani kwa lengo la kumsalimia na kumpongeza kwa kuteuliwa katika nafasi ya Katibu Mkuu. Timu  hiyo ya vijana  kutoka nchi wanachama wa Ukanda wa Maziwa Makuu ipo nchini kama Waangalizi wa Uchaguzi Mkuu wa Tanzania. Wengine katika picha ni Balozi Muburi Muita, Mkuu wa Msafara na Mratibu wa Kitaifa wa ICGLR nchini Kenya pamoja na Bi. Nancy Kaizilege.
Sehemu ya Vijana hao wakimsikiliza Balozi Mulamula (hayupo pichani). Vijana hao wanatoka nchi za Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Angola, Zambia, Sudan Kusini, Sudan, Tanzania na DRC.
Balozi Muburi nae akizungumza wakati wa mkutano kati ya Wawakilishi wa Jukwaa la Vjana wa ICGLR na Balozi Mulamula.
Sehemu nyingine ya vijana wakifuatilia mkutano wao na Balozi Mulamula (hayupo pichani)
Bi. Nancy nae akitoa maelezo mafupi kuhusu dhumuni la ziara ya Vijana hao hapa Wizarani.
Vijana wakifuatilia

Picha ya pamoja. 



Mkataba wa Makubaliano kuhusu Misaada ya Kibinadamu kwa Wakimbizi huko Kigoma wasainiwa

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula kwa pamoja na Bw. Anton Breve, Naibu Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Madaktari wasio na Mipaka wakisaini Mkataba wa Makubaliano kuhusu Misaada ya Kibinadamu kwa Wakimbizi waliopo Kigoma. Uwekaji saini huo umefanyika Wizarani tarehe 27 Oktoba, 2015.
Balozi Mulamula na Bw. Breve wakibadilishana Mkataba huo wa Makubaliano mara baada ya kusainiwa
Balozi Mulamula akiwa kwenye mazungumzo na Bw. Breve kabla ya kusaini Mkataba wa Makubaliano kuhusu Misaada ya Kibinadamu kwa Wakimbizi waliopo Mkoani Kigom.
Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Baraka Luvanda (kushoto)  kwa pamoja na Maafisa katika Kitengo hicho Bw. Gerald Mbwafu (katikati) na Bw. Elisha Suku (kulia) wakifuatilia mazungumzo kati ya Balozi Mulamula na Bw. Breve (hawapo pichani). 

Monday, October 26, 2015

Balozi Mwakasege awasilisha Hati za Utambulisho nchini Malawi

Tarehe 22 Oktoba, 2015 Mhe. Balozi Victoria Richard Mwakasege alipata fursa ya kuwasilisha Hati za Utambulisho kwa Mhe. Prof. Arthur Peter Mutharika katika Ikulu ya Kamuzu Palace mjini Lilongwe.
Mhe. Balozi Victoria Richard Mwakasege akipigiwa nyimbo za taifa za Malawi na Tanzania huku akishuhudiwa na maafisa Ubalozi.
Mhe. Balozi Victoria Richard Mwakasege akisaini kitabu cha wageni mara baada ya kuwasili katika Ikulu ya Kamuzu Palace mjini Lilongwe. Wanaoshuhudia ni maafisa Ubalozi Wilbroad A. Kayombo kushoto, Elyneema Lissu, Nimpha Marunda na Mbonile Mwakatundu
Mhe. Balozi Victoria Richard Mwakasege akiwasilisha Hati za Utambulisho kwa Mhe. Rais Prof. Arthur Peter Mutharika
Mhe. Balozi Victoria Richard Mwakasege akiagana na Mhe. Prof. Arthur Peter Mutharika 
Watumishi wa Ubalozi wakiwa na Mhe. Balozi Victoria Richard Mwakasege nyumbani kwake

Friday, October 23, 2015

Mabalozi wa Nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya wamtembelea Katibu Mkuu Nje.

Balozi wa Umoja wa Ulaya hapa nchini Mhe. Filiberto Sebregondi akizungumza na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Liberata Mulamula.
Ujumbe ulioambatana na Balozi Sebregondi, wakifuatilia mazungumzo hayo.
Mkurugenzi wa Idara ya Amerika na Ulaya Balozi Joseph Sokoine (kulia) na Mkurugenzi wa Idara ya Afrika Balozi Samwel Shelukindo, wakifuatilia mazungumzo hayo. 
 Ujumbe ulioambatana na Balozi Sebregondi, wakifuatilia mazungumzo hayo.
 Mkutano ukiendelea.
===============
PICHA NA: REUBEN MCHOME.

Balozi Luvanda akutana kwa mazungumzo na Balozi wa Uturuki

Mkurugenzi wa Kitengo cha Sheria katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Baraka Luvanda akiwa katika mazungumzo na Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Mhe. Yasemin Eralp. Mazungumzo hayo yalihusu ukimalishaji wa Makubaliano mbalimbali kati ya Tanzania na Uturuki ili yaweze kusainiwa na kuanza kutekelezwa.
Balozi Luvanda akisisitiza jambo katika mazungumzo hayo
Balozi wa Uturuki nchini Tanzania, Mhe. Yasemin Eralp akimsikiliza kwa makini Balozi Luvanda ambaye hayupo pichani
Balozi wa Uturuki akibadilishana mawazo na Afisa wake wakati wa mazungumzo hayo
Balozi wa Uturuki, Mhe. Yasemin Eralp akimkabidhi nyaraka Balozi Luvanda
Balozi Luvanda pamoja na Afisa wake, Bw. John Pangipita wakimsikiliza Balozi wa Uturuki hayupo pichani.

Mazungumzo yanaendelea





Tanzania na Malawi zawasilisha Rasimu ya Azimio kuhusu Watu wenye Ualbino

Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania  katika Umoja wa Mataifa  Balozi Tuvako Manongi akifurahia jambo na Bi Ikponwosa Ero mwenye Ualibino mara  baada ya mazungumzo yao  ambapo walibadilisha mawazo kuhusu pamoja na mambo mengine,   changamoto zinazowakabili watu wenye ualibino na namna gani jumuiya ya kimatifa inaweza kushirikiana katika kuzikabili changamoto hizo. Bi Ikponwosa  aliteuliwa mwezi Agosti Mwaka huu na  Kamisheni ya  Haki za Binadamu  ya Umoja wa Mataifa kama  Mtaalamu huru anayeendesha kampeni,  uhamasishaji, uelimishaji  na  uwezeshaji kuhusu watu wenye ualibino na changamoto  zinazowakabili  watu wenye ualibino. Bi Ero ni   Mzaliwa wa Nigeria mwenye uraia wa Canada.
 
Na  Mwandishi Maalum, New York

Kutokana na changamoto mbalimbali zinazowakabili watu wenye ualibino, Wakilishi za Kudumu za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Malawi katika Umoja wa Mataifa, zimewasilisha rasimu ya azimo kuhusu watu wenye ualibino.

Rasimu ya azimio hilo inalenga katika kuzishawishi na kuzitaka Jumuiya ya Kimataifa kuendelea na juhudi za kutetea haki na ustawi wa watu wenye ualibino ikiwa ni pamoja na kuliwanda.

Azimio hilo limewasilishwa kupitia Kamati ya Tatu ya Utamaduni,  Haki za Binadamu na Jamii ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa,  na ambalo limekwisha kusambazwa kwa nchi wanachama na wadau wengine kwa ajili ya kupata maoni na kuungwa mkono.

Azimio hilo linajielekeza pia katika kusisitiza upatikanaji wa fursa za elimu, huduma za afya na ajira kwa watu wenye ualibino, maeneo ambayo ni changamoto kubwa kwa watu hao.

Kupitia azimio hilo, Tanzania na Malawi,  zinaitaka Jukumuiya ya Kimataifa kuunga  mkono jitihada zinazofanywa na nchi ambazo tayari zimejiwekea sera, sheria na mipango ya pamoja na  mambo mengine, kuwalinda watu wenye ualbino na kuwapatia fursa mbalimbali za maendeleo kama raia wengine.

Vile vile, azimio hilo linamwomba Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,  kuwasilisha taarifa kuhusu hali za watu wenye ualibino mkazo ukiwa katika changamoto wanazokabiliana nazo,  na juhudi ambazo zimechukuliwa na nchi wanachama katika kuzikabili.

Taarifa hiyo ya Katibu Mkuu inaombwa kuwasilishwa wakati wa Mkutano wa  71 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa chini ya ajenda ya Maendeleo ya Jamii.

Azimio hilo pia linasisitiza haja na umuhimu wa kutambua juhudi zinazofanywa katika ngazi ya nchi na Ki- Kanda, na hivyo Katibu Mkuu anaombwa kuwasilisha katika Baraza Kuu la 71 la Umoja wa Mataifa,  mapendekezo ya namna ya kuimarisha uwezo na juhudi za nchi husika katika kulitafutia ufumbuzi tatizo la  watu wenye ualibino kwa kadri nchi hizo zitakavyoomba.

Katika sehemu ya utangulizi wa Azimio, Azimio linatambua juhudi mbalimbali na taarifa za vyombo vingine kama Vile Baraza la Haki za Binadamu, Kamisheni ya Umoja wa Afrika kuhusu haki za watu ,kuzuia vitendo viovu na ubaguzi dhidi ya watu wenye ualbino.

Azimio linaeleza hofu dhidi ya uovu wanaofanyiwa watu wenye ualibino wakiwamo wanawake na watoto.