Thursday, July 13, 2017

Ziara ya Mhe. Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Morocco nchini 12 -13 Julai, 2017


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Ziara ya Mhe. Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Morocco nchini 12 -13 Julai, 2017

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kutoka Serikali ya Ufalme wa Morocco Mhe.Mounia Boucetta na ujumbe wake wametembelea Wizara leo tarehe 13 Julai, 2017 na kufanya mazungumzo na mwenyeji wake Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Suzan Kolimba katika ukumbi wa Wizara, Dar es Salaam. Mhe. Mounia Boucetta yupo nchini kwa ziara ya kikazi tangu tarehe 12 Julai, 2017.

Lengo la ziara hiyo ni kufuatilia utekelezaji wa Maazimio na makubaliano ya Ushirikiano kati ya taasisi za Tanzania na Morocco katika sekta mbalimbali, yaliyosainiwa wakati wa ziara ya Mfalme Mohammed VI wa Morocco nchini Tanzania tarehe 23 – 25 Octoba, 2016. 

Itakumbukwa katika ziara hii jumla ya mikataba 21 ya Ushirikiano katika maeneo mbalimbali ilisainiwa. Mikataba hiyo ni katika masuala yafuatayo; Masuala ya Usafiri wa Anga, Kilimo na Uvuvi, Nishati, Utalii, Viwanda Usafiri wa Reli, Biashara, Masuala ya Bima, Masuala ya Afya, Masuala ya Gesi, Masuala ya Siasa, Uchumi, Sayansi na Utamaduni. 

Aidha Mheshimiwa Mfalme Mohamed VI aliahidi mambo makuu matatu
·        Ujenzi wa msikiti mkubwa wa kisasa jijini Dar es salaam
·        Ujenzi wa uwanja wa kisasa wa mpira mjini Dodoma
·        Kuanzisha programu ya mafunzo kwa maafisa wa majeshi yetu ya ulinzi na usalama

Tangu ziara hiyo ifanyike Serikali ya Ufalme wa Morocco, katika kuimarisha urafiki na ushirikiano ilifungua Ubalozi wake jijini Dar es salaam, na Mwezi Februari, 2017 Mheshimiwa Balozi Abdelillah Benryane aliwasilisha hati zake za utambulisho Nchini.

Wizara inawataarifu kuwa Ubalozi umeanza kufanya kazi nzuri, kazi mojawapo kubwa ni kufuatilia utekelezaji wa mikataba hiyo iliyosainiwa wakati wa ziara ya Mheshimiwa Mfalme.

Hivyo ujio wa Mheshimiwa Naibu Waziri Mounia Boucetta ni sehemu ya ufuatiliaji wa hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa mikataba hiyo iliyosainiwa.

Wizara ilifanya kikao na Mheshimwa Mounia Boucetta  na kupitia taarifa ya utekelezaji wa mikataba hiyo kwa sekta ya umma na sekta binafsi, na kwa kweli tunaridhishwa na kasi ya utekelezaji.

Pamoja na kasi nzuri hiyo ya utekelezaji Wizara imezielekeza taasisi husika kuongeza kasi zaidi ili tukamilishe utekelezaji wa maeneo hayo tuliokubaliana na kuwawezesha Watanzania wafanyabiashara, wakulima, wazalishaji na wasomi kunufaika na fursa mbalimbali.

Aidha, akizungumza katika majadiliano hayo Naibu Waziri Mhe. Dr. Suzan Kolimba (Mb) amesema wamekubaliana kuundwa Kamati ya Ufuatiliaji ya utekelezaji wa makubaliano mbalimbali yaliyofikiwa kati ya Tanzania na Morocco. 

Mhe. Mounia Boucetta pamoja na ujumbe wake leo saa 4:00 asubuhi watakutana na ujumbe wa wadau wa biashara na uwekezaji kutoka Wizara na taasisi za Serikali pamoja na taasisi binafsi za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Hoteli ya Serena, Dar es Salaam

-Mwisho-

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali,
Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,
Dar es Salaam, 13 Julai, 2017
Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Aziz Mlima akitoa neno la ukaribisho kwa ujumbe wa Morocco kabla ya kumkaribisha Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt Suzan Kolimba (Mb) kusoma hotuba ya ufunguzi wa kikao kazi cha kufuatilia utekelezaji wa maazimio na Makubaliano mbalimbali baina ya sekta za Tanzania na Morocco yaliyofikiwa wakati wa ziara ya Mfalme VI wa Morocco nchini Tanzania.

Naibu Waziri Suzan Kolimba akisoma hotuba yake katika kikao hicho
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Ufalme wa Morocco, Mhe. Mounia Boucetta akisoma hotuba katika kikao kazi cha kufuatilia utekelezaji wa makubaliano ya Tanzania na Morocco

Ujumbe wa Tanzania ukiwajumuisha Makatibu Wakuu na Wakuu wa Taasisi mbalimbali wanaounda kikosi kazi cha kufuatilia utekelezaji wa makubaliano ya Morocco na Tanzania
Ujumbe wa Morocco katika kikao hicho
Washiriki wa kikao kazi cha kufuatilia utekelezaji wa makubaliano kati ya Tanzania na Morocco wakiwa katika kikao cha tathmini ya utekelezaji kilichofanyika Serena Hoteli

Mhe. Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt.Suzan Kolimba (kulia) akiwa katika mazungumzo na Mhe. Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kutoka  Ufalme wa Morocco Mhe.Mounia Boucetta katika ukumbi wa Wizara- Dar es Salaam, tarehe 13 Julai,2017.
 
 Mhe. Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt.Suzan Kolimba akipokea zawadi kutoka kwa, Mhe. Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Ufalme wa Morocco baada ya mazungumzo.

Mhe. Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt.Suzan Kolimba, Mhe. Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Ufalme wa Morocco na ujumbe wake, wengine ni wataalam kutoka Wizarani wakiwa katika picha ya pamoja baada ya mazungumzo 





Wednesday, July 12, 2017

Kuwaiti Ambassador visit Ministry of Foreign Affairs

Ambassador of Kuwait to Tanzania H.E Jasem Al-Najem (L) gets greetings with the Permanent Secretary for the Ministry of Foreign Affairs and East African Cooperation, Dr. Aziz Mlima, when the two met today at the Ministry's office to discuss various issues relating to the bilateral relations between the two countries.

Dr. Mlima and Ambassador of Kuwait proceed with their conversations in which among other things, Dr. Mlima promised that the Government will work on to see the possibility of hosting the First Joint Permanent Commission meeting with Kuwait where its agreement was signed since 2013.


Conversation are in progress. Another in the photo is the Kuwait Desk Officer, Mr. Hangi Mgaka.

Group photo

Monday, July 10, 2017

Balozi wa Italia atembelea Wizara ya mambo ya Nje

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Suzan Kolimba (Mb), akimkaribisha ofisini kwake Balozi wa Italia nchini Tanzania, Mhe. Roberto Mengoni na ujumbe wake kwa ajili ya kufanya mazungumzo.

Dtk. Kolimba akisisitiza jambo kwenye mazungumzo na Balozi wa Italia nchini, Mhe. Roberto Mengoni.   Katika mazungumzo hayo alikuwepo pia Makamu wa Rais wa Shirika la Taifa la Reli la Italia, Bw. Giovanni Roca ambaye amekuja nchini kuangalia fursa za uwekezaji katika sekta ya reli baada ya kuhamasishwa na Mhe. Naibu Waziri alipotembelea Italia hivi karibuni.


Ujumbe wa Italia uliofuatana na Mhe. Balozi ukifuatilia mazungumzo.

Bw. Charles Faini (kulia), Katibu wa Naibu Waziri na Bw. Salvatory Mbilinyi wa Wizara ya Mambo ya Nje wakinukuu taarifa muhimu
Picha ya pamoja


Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje ya India atembelea Wizara ya Mambo ya Nje

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Dkt. Aziz Mlima akiwa katika mazungumzo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje wa India anayeshughulikia Masuala ya nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika, Bi. Neena Malhotra.  Wawili hao walizungumzia namna nchi zao zinatakavyoweza kuendeleza ushirikiano katika sekta mbalimbali kama za uwekezaji, miundombinu, afya, elimu, TEHAMA, biashara na kilimo. Aidha, Balozi Mlima alimuomba asaidie kuhamasisha wawekezaji kutoka India kuja kuwekeza nchini katika viwanda ili kuunga mkono agenda ya Serikali ya awamu ya tano inayoweka mkazo kwenye viwanda. 
Ujumbe wa Tanzania (kulia) na ule wa India ukiongozwa na Makatibu Wakuu wao ukiwa katika majadiliano ya namna ya kuboresha zaidi mahusiano kati ya Tanzania na India ambayo yemedumu kwa miaka mingi sasa

Balozi Mlina akikabidhi zawadi kwa Katibu Mkuu wa India

picha ya pamoja



Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Korea-Afrika atembelea Wizara ya Mambo ya Nje

Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki ,Balozi Dkt. Aziz Mlima (kulia) akibadilishana kadi za mawasiliano na Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Korea-Afrika (Korea-Africa centre) cha Jamhuri ya Korea, Balozi KIM IL Soo kabla ya kufanya mazungumzo.

Balozi Mlima akiwa katika mazungumzo na Balozi KIM ambapo walijadiliana namna ya Tanzania na Korea zitakavyoboresha mahusiano ya kidiplomasia na kusisitiza umuhimu wa Chuo cha Diplomasia na Kituo cha Korea-Afrika kuwa na ushirikiano katika nyanja mbalimbali ikiwemo kubadilishana walimu na wanafunzi.

Ujumbe wa Tanzania ukifuatilia mazungumzo. kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia, Bi. Justa Nyange

Ujumbe wa Jamhuri ya Korea ukifuatilia mazungumzo

Mazungumzo yakiendelea

Balozi Mlima akimkabidhi Balozi KIM kifurushi cha zawadi ya kahawa na chai ya Tanzania

Picha ya Pamoja