Thursday, September 15, 2022

TANZANIA NA DRC ZAAHIDI UTEKELEZAJI WA MAAZIMIO YA MKUTANO WA JPC


                                                                                

 
                            
    
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akisoma hotuba ya kufunga Mkutano wa Tatu wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) uliofanyika jijini Dar Es Salaam tarehe 12 hadi 14 Septemba 2022

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akiwa meza kuu kwa ajili ya Mkutano wa Tatu wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC). Wengine katika picha, kulia ni Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mtangamano wa Kikanda na Nchi zinazongumza Kifaransa wa DRC, Mhe. Zacharie Tshimbinda Bilolo. 

Waziri wa Mtangamano wa Kikanda na Nchi zinazozungumza Kifaransa wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Mhe. Didier Mazenga Mukanzu akisoma hotuba ya kufunga Mkutano wa Tatu wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) uliofanyika jijini Dar Es Salaam tarehe 12 hadi 14 Septemba 2022
Wajumbe wakifuatilia hotuba za viongozi wakati wa kufunga  Mkutano wa Tatu wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Liberata Mulamula na Waziri wa Mtangamano wa Kikanda na Nchi zinazozungumza Kifaransa wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Mhe. Didier Mazenga Mukanzu wakisaini Taarifa ya Mkutano wa Tatu wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) uliofanyika jijini Dar Es Salaam tarehe 12 hadi 14 Septemba 2022 

Wajumbe wakifuatilia hotuba za viongozi wakati wa kufunga  Mkutano wa Tatu wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Liberata Mulamula na Waziri wa Mtangamano wa Kikanda na Nchi zinazozungumza Kifaransa wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Mhe. Didier Mazenga Mukanzu wakibadilishana Taarifa ya Mkutano wa Tatu wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) uliofanyika jijini Dar Es Salaam tarehe 12 hadi 14 Septemba 2022 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula akimpa zawadi ya picha za kuchora za twiga Waziri wa Mtangamano wa Kikanda na Nchi zinazozungumza Kifaransa wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ya Kongo (DRC), Mhe. Didier Mazenga Mukanzu

Picha ya pamoja ya viongozi Wakuu walioshiriki Mkutano wa Tatu wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano (JPC) kati ya Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo(DRC) uliofanyika jijini Dar Es Salaam


 

WAZIRI MULAMULA AKUTANA NA BALOZI WA UFARANSA


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula amekutana kwa mazungumzo na Balozi wa Ufaransa nchini, Mhe. Nabil Hajlaoui katika Ofisi Ndozo za Wizara Jijini Dar es Salaam tarehe 14 Septemba 2022.

Katika mazungumzo yao viongozi hao wamejadili juu ya kuimarisha ushirikiano baina ya mataifa yao katika sekta za uwekezaji, ujenzi na uboreshaji wa miundombinu, biashara, usafiri na uchukuzi, nishati, kilimo, uchumi wa blue, elimu na utamaduni.

Pia wamejadili umuhimu wa kuwa na kamati za kitaifa kwa ajili ya ufuatiliaji wa masuala ya msingi ya utekelezaji yaliyokubaliwa wakati wa ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan nchini Ufarasa mwezi Februari 2022, pamoja na masuala mengine ya ushirikiano baina ya nchi zao.

Vilevile wamejadili juu ya mchango unaotolewa na serikali ya Ufaransa katika masuala ya ulinzi wa amani pamoja na nafasi ya tanzania katika kusimamia masuala ya ulinzi na amani kikanda hususan katika  Nchi wanachama za Jumuiya ya Maendeleo kusini mwa Afrika (SADC), Nchi wanachama za Jumuiya ya Afrika Mashariki(EAC) na katika Umoja wa Afrika (AU).

Mhe. Nabil Hajlaoui akimweleza Mhe. Balozi Liberata Mulamula jitihada zinazofanya na Serikali yake katika kuunga mkono jitihada za kusaidia shughuli za maendeleo barani Afrika kwa kushirikiana na mataifa mengine ya Ulaya walipokutana kwa mazungumzo katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam tarehe 14 Septemba 2022.

 Mhe. Balozi Mulamula akiagana na Mhe. Nabil Hajlaoui baada ya mazungumzo katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam tarehe 14 Septemba 2022.

Mazungumzo yakiendelea.

Picha ya Pamoja, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (wa pili kulia), Mhe. Nabil Hajlaoui (wa pili kushoto) na maafisa waliombatana nao katika mazungumzo yao.

 

TANZANIA YAPONGEZWA KWA KUWA MWANACHAMA HAI WA UMOJA WA AFRIKA

Pongezi hizo zimetolewa na Makamu Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika, Mhe. Monique Nsanzabaganwa alipokutana kwa mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula pembezoni mwa Mkutano wa Wanawake na Vijana katika Biashara katika Eneo Huru la Biashara Barani Afrika (AfCFTA) uliofanyika kuanzia tarehe 12 hadi 14 Septemba 2022 Jijini Dar es Salaam.

Akifafanua shughuli za utekelezaji zinazofanywa na Kamisheni ya Umoja wa Afrika kwa kushirikiana na Nchi Wanachama Mhe. Nsanzabaganwa alieleza kuwa Tanzania ni miongoni mwa wadau muhimu katika Umoja wa Afrika ambapo, licha ya nafasi yake ya kuunga mkono uanzishwaji wa umoja huo pia imekuwa ikikamilisha michango yake ya uanachama kwa wakati.

"Ukamilishaji wa michango kwa wakati kutoka kwa Nchi wanachama unawezesha uendeshaji wa shughuli za Sekretarieti kutekelezeka kwa tija na kusaidia kupatikana kwa maslahi ya watumishi." alisema Mhe. Nsanzabaganwa.

Naye Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula amemuhakikishia Mhe. Nsanzabaganwa kuwa Tanzania itaendelea kuheshimu makubaliano yaliyokubaliwa katika Umoja wa Afrika sambamba na kuhakikisha inanufaika na fursa mbalimbali zinazopatikana kama vile ajira na biashara.

Pia ameshukuru kwa jitihada zinazofanywa na Umoja wa Afrika kupitia Mkataba wa Eneo Huru la Biashara Barani Afrika (AfCFTA) kwa kumtambua Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama Kinara wa Uhamasishaji wa Masuala ya Wanawake na Vijana katika biashara, sambamba na heshima iliyotolewa kwa Tanzania ya kuwa mwenyeji wa Mkutano wa Wanawake na Vijana katika Biashara katika Eneo Huru la Biashara Barani Afrika.

Aidha, Mhe. Waziri amesema kuwa mkutano huo ni muhimu sana kwakuwa umebeba agenda ya wanawake na vijana yenye lengo la kujenga haki na usawa wa kijinsia katika ajira, kupunguza changamoto ya ukosefu wa ajira, kuwajengea uwezo na kushirikishana uzoefu katika biashara na kuingia katika ushindani wa biashara kitaifa, kikanda na kimataifa.


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akizungumza na Makamu Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika, Mhe. Monique Nsanzabaganwa katika ofisi za Wizara jijini Da es Salaam tarehe 14 Septemba 2022. 

Mazungumzo yakiendelea

Picha ya pamoja baada ya mazungumzo.
 

Tuesday, September 13, 2022

BALOZI WA TANZANIA NCHINI INDONESIA AWASILISHA HATI ZA UTAMBULISHO

Balozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Indonesia Mhe. Macocha Tembele mapema leo tarehe 13/09/2022 amewasilisha hati zake za utambulisho kwa Rais wa Indonesia Mhe. Joko Widodo katika hafla iliyofanyika kwenye Kasri la Merdeka jijini Jakarta. 

Katika hafla hiyo, wawili hao walipata fursa ya kubadilishana mawazo kuhusu masuala mbalimbali ikiwemo namna ya kuimarisha ushirikiano katika sekta ya biashara na uwekezaji. 

Hatua hiyo ya Mhe. Balozi Makocha Tembele kuwasilisha hati zake za utambulisho inaashiria kuanza rasmi kwa utumishi wake katika nchi hiyo. 
Balozi wa Tanzania nchini Indonesia Mhe. Macocha Tembele akiwasilisha hati zake za utambulisho kwa Rais wa Nchi hiyo Mhe. Joko Widodo
Balozi wa Tanzania nchini Indonesia Mhe. Macocha Tembele akiwasili katika Kasri la Merdeka jijini Jakarta ambapo aliwasilisha hati zake za utambulisho kwa Rais wa Indonesia Mhe. Joko Widodo
Balozi wa Tanzania nchini Indonesia Mhe. Macocha Tembele akisalimiana na Rais wa Nchi hiyo Mhe. Joko Widodo

Monday, September 12, 2022

TANZANIA YASISITIZA KUBORESHA MIFUMO KUWAINUA WANAWAKE NA VIJANA KIUCHUMI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan ameahidi kuendelea kusimamia mifumo ya utendaji kazi katika Serikali yake ili kuwawezesha wanawake na vijana washiriki kikamilifu katika biashara.

Ahadi hiyo imetolewa wakati wa Mkutano wa Wanawake na Vijana katika Biashara ulioandaliwa na Sekretarieti ya Eneo Huru la Biashara Barani Afrika (AfCFTA) na kufanyika katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam kuanzia tarehe 12 hadi 14 Septemba 2022.

Akiongea katika mkutano huo, Mhe. Rais Samia ameeleza baadhi ya maeneo ambayo Serikali ya Awamu ya Sita imeyafanyia maboresho ili biashara zinazofanywa na Wanawake na Vijana nchini zilete matokeo chanya sambamba na kuinua kipato chao na uchumi wa Taifa kwa ujumla.

Maeneo hayo ni pamoja na: Kuondoa vikwazo vya biashara, kuwawezesha wanawake kupata mikopo ya riba nafuu, maboresho katika mifumo ya tozo katika sekta mbalimbali kama vile kilimo na madini, kuwezeshwa kupata vyeti vya ubora kwa ajili ya kuingia katika ushindani wa soko la kimataifa na kupunguza ushuru unaotozwa na mamlaka mbalimbali za Serikali.

Aidha, Mhe, Rais Samia amesema kuwa Serikali yake inatoa nafasi za upendeleo kwa sekta binafsi kushiriki katika shughuli za maendeleo, na kwa sasa Tanzania imetoa kipaumbele kwa wanawake ambapo asilimia 30 ya manunuzi yote makubwa ya Serikali yanatolewa kwa makampuni ya wanawake.

“Mapema mwezi Mei 2022 nikiwa nchini Ghana kwenye mkutano ulioratibiwa na Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) na Serikali ya Ghana ambao uliwakutanisha Wakuu wa Nchi na Serikali  nilipewa heshima ya kuwa kinara wa hamasa ya kuinua Wanawake na Vijana kwenye biashara, hivyo naahidi kuendelea kusimamia mapambano hayo”. Alisema Mhe. Rais Samia.

Akieleza zaidi, Mhe. Rais Samia ameeleza kuwa ili kufikia malengo ya kuinua biashara ni vema sasa nchi za Afrika zikawekeza kwenye miundombinu ili ziweze kufikika na kurahisisha shughuli za biashara kwa wananchi wake ambapo sehemu kubwa ya wajasiliamali wake ni wanawake na vijana.

Pia amesisitiza kuwa manufaa ya itifaki ya Wanawake na Vijana katika biashara kwenye Mkataba wa Eneo Huru Barani Afrika hayawezi kupatikana moja kwa moja kama mipango ya kitaifa ya nchi wanachama haitowajumuisha wanawake na vijana katika utekelezaji wake. 

Hivyo, ni vema nchi wanachama zikawekeza pia kwenye tafiti ili kufahamu namna bora ya kuondoa changamoto kwenye uhalisia wa jambo husika ambapo alieleza kwa nyakati tofauti Tanzania imefanya tafiti katika masoko ili yaweze kunufaisha wanawake na kusaidia kuwajengea miundombinu wezeshe kwa shughuli za biashara.

Katika hatua nyingine, Mhe. Rais ameeleza kuwa Tanzania inaandaa mpango wa kusimamia usawa kwa kizazi kijacho ili kuwawezesha wanawake kupata fursa sawa na wanaume na kuhakikisha wanawake na vijana wanawezeshwa kiuchumi na kuwekewa mfumo utakaowawezesha kupata ajira rasmi na zenye ujira utakaowainua kiuchumi kwa maendeleo ya Taifa.

Mhe. Rais Samia pia alitumia fursa ya mkutano huo kunadi fursa za uwekezaji zilizopo nchini katika sekta za kilimo cha mazao ya chakula, matunda na mbogamboga, sekta ya mifugo hususan nyama na bidhaa za ngozi, madini na utalii.

Wakati huo huo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika, Mhe Balozi Liberata Mulamula katika mkutano huo aliongoza majadiliano yaliyokuwa na mada isemayo “Kuunga mkono Uongozi wa Wanawake na Vijana katika Biashara” (Supporting Women and Youth’s Leadership in Trade).

Mjadala huo ulihusisha viongozi wakuu wanawake wa nchi za Afrika ambao ni: Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Malawi, Mhe. Joyce Banda, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Liberia, Mhe. Dkt. Jewel Taylor-Howard, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Uganda, Mhe. Jessica Allupo, Katibu Mtendaji wa Sekretarieti ya Eneo Huru la Biashara Barani Afrika,Mhe. Wamkele Mene na Naibu Mwenyekiti, Kamisheni ya Umoja wa Afrika, Mhe. Dkt. Monique Nsanzabaganwa.

Washiriki wengine wa mkutano huo ni pamoja na: Mabalozi, Mawaziri wanaohusika na Biashara na Mawaziri wanaohusika na masuala ya jinsia. wanawake na vijana wanaojishughulisha na masuala ya biashara, watunga será na wadau wa maendeleo.

Sanjari na mkutano huo, wajasiriamali zaidi ya 80 wameshiriki kwenye maonesho ya bidhaa mbalimbali ambapo Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ina washiriki wapatao 72.

 ==============================================================

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Wanawake na Vijana katika Biashara katika Eneo Huru la Biashara Barani Afrika (AfCFTA) unaofanyika kuanzia tarehe 12 hadi 14 Septemba 2022 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (JNICC) Jijini Dar es Salaam. 

 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akifuatilia hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Wanawake na Vijana katika Biashara kwenye Eneo Huru la Biashara Barani Afrika (AfCFTA) unaofanyika kuanzia tarehe 12 hadi 14 Septemba 2022 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (JNICC) Jijini Dar es Salaam. 

Sehemu ya Mawaziri na Viongozi Waandamizi kutoka Serikali ya Mapinduzi Zanzibar wakifuatilia hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Wanawake na Vijana katika Biashara kwenye Eneo Huru la Biashara Barani Afrika (AfCFTA) unaofanyika kuanzia tarehe 12 hadi 14 Septemba 2022 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (JNICC) Jijini Dar es Salaam. 



Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab akifuatilia hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Wanawake na Vijana katika Biashara kwenye Eneo Huru la Biashara Barani Afrika (AfCFTA) unaofanyika kuanzia tarehe 12 hadi 14 Septemba 2022 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (JNICC) Jijini Dar es Salaam. 

Katibu wa Waziri Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika, Bw. Seif Kamtunda akifuatilia hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Wanawake na Vijana katika Biashara kwenye Eneo Huru la Biashara Barani Afrika (AfCFTA) unaofanyika kuanzia tarehe 12 hadi 14 Septemba 2022 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (JNICC) Jijini Dar es Salaam. 

Rais wa Jamhuri ya Uganda, Mhe. Jessica Allupo akihutubia wakati wa hafla ya ufunguzi wa Mkutano wa Wanawake na Vijana katika Biashara kwenye Eneo Huru la Biashara Barani Afrika (AfCFTA) unaofanyika kuanzia tarehe 12 hadi 14 Septemba 2022 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (JNICC) Jijini Dar es Salaam. 

Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mindi Kasiga akisherehesha wakati wa Mkutano wa Wanawake na Vijana katika Biashara kwenye Eneo Huru la Biashara Barani Afrika (AfCFTA) unaofanyika kuanzia tarehe 12 hadi 14 Septemba 2022 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (JNICC) Jijini Dar es Salaam. 


Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Fatma Rajab akisalimiana na sehemu ya Mawaziri walioshiriki Mkutano wa Wanawake na Vijana katika Biashara kwenye Eneo Huru la Biashara Barani Afrika (AfCFTA) unaofanyika kuanzia tarehe 12 hadi 14 Septemba 2022 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (JNICC) Jijini Dar es Salaam. 

Picha ya pamoja

Mhe. Balozi Liberata Mulamula akiongoza majadiliano yaliyokuwa na mada isemayo “Kuunga mkono Uongozi wa Wanawake na Vijana katika Biashara” (Supporting Women and Youth’s Leadership in Trade) wakati wa Mkutano wa Wanawake na Vijana katika Biashara kwenye Eneo Huru la Biashara Barani Afrika (AfCFTA) unaofanyika kuanzia tarehe 12 hadi 14 Septemba 2022 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (JNICC) Jijini Dar es Salaam.

Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Malawi, Mhe. Joyce Banda akichangia hoja kwenye majadiliano yaliyokuwa na mada isemayo “Kuunga mkono Uongozi wa Wanawake na Vijana katika Biashara” (Supporting Women and Youth’s Leadership in Trade) wakati wa Mkutano wa Wanawake na Vijana katika Biashara kwenye Eneo Huru la Biashara Barani Afrika (AfCFTA) unaofanyika kuanzia tarehe 12 hadi 14 Septemba 2022 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano (JNICC) Jijini Dar es Salaam.

Majadiliano yakiendelea.
Picha ya pamoja, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Malawi, Mhe. Joyce Banda (wa pili kushoto) Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Liberia, Mhe. Dkt. Jewel Taylor-Howard (wa pili kulia), Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Uganda, Mhe. Jessica Allupo (katikati) na Naibu Mwenyekiti, Kamisheni ya Umoja wa Afrika, Mhe. Dkt. Monique Nsanzabaganwa (wa kwanza kushoto).

TANZANIA NA DRC ZAKUTANA DAR KUJADILI BIASHARA NA UWEKEZAJI



Mkurugenzi wa Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Naimi Aziz akiwakaribisha Makatibu Wakuu wa Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Balozi Joseph Sokoine na Mhe. Zacharie Tshimbinda Bilolo  kusoma hotuba za ufunguzi za Mkutano wa Tatu wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na DRC. 
Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine akipitia hotuba yake ya ufunguzi ya Mkutano wa Tatu wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na DRC. 

Mkurugenzi wa Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Naimi Aziz akifafanua jambo kwa viongozi kuhusu Mkutano wa Tatu wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na DRC. 

Sehemu ya Ujumbe wa DRC unaoshiriki Mkutano wa Tatu wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na DRC. 

Mkutano wa Tatu wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na DRC ngazi ya wataalam unaendelea jijini Dar Es Salaam. 
Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine akizungumza jambo na Konseli Mkuu wa Tanzania, Lubumbashi, Bw. Selestine Kakere kabla ya ufunguzi wa Mkutano wa Tatu wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na DRC. 

Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Joseph Sokoine na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mtangamano wa Kikanda na Nchi zinazongumza Kifaransa wa DRC, Mhe. Zacharie Tshimbinda Bilolo wakiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Tanzania na DRC wanaoshiriki Mkutano wa Tatu wa Tume ya Kudumu ya Pamoja ya Ushirikiano kati ya Tanzania na DRC. 


 

Sunday, September 11, 2022

TANZANIA MWENYEJI WA MKUTANO WA WANAWAKE NA VIJANA KATIKA BIASHARA WA AfCFTA

Tanzania inatarajia kuwa mwenyeji wa Mkutano wa Wanawake na Vijana katika Biashara kwenye Eneo Huru la Biashara Barani Afrika utakaofanyika kuanzia tarehe 12 hadi 14 Septemba, 2022 kwenye Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar-es-salaam. 

Tanzania inatarajia kuwa mwenyeji wa mkutano wa “Wanawake na Vijana katika Biashara kwenye Eneo Huru la Biashara Barani Afrika” utakaofanyika kuanzia tarehe 12 hadi 14 Septemba, 2022 Jijini Dar es Salaam. 

Mgeni rasmi katika mkutano huo anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, ambaye ataufungua rasmi mkutano huo tarehe 12 Septemba 2022 katika Kituo Cha Kimataifa Cha Mikutano (JNICC), Dar es Salaam.

Mkutano huo utahudhuriwa na  Viongozi Wakuu wa Nchi na Serikali, Marais Wastaafu, Makamu wa Rais, Mawaziri Wakuu, Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika, Mabalozi, Mawaziri wa Biashara na Mawaziri wa masuala ya jinsia.
 
Mkutano huu pia utawakutanisha, Wanawake na Vijana wanaojishughulisha na masuala ya biashara, watunga sera, wafadhili, wadau wa maendeleo, na wadau wengine muhimu wa biashara barani Afrika ambao watajadili kwa kina agenda Wanawake na Vijana katika biashara barani Afrika.

Viongozi Wakuu walioawasili nchini na kupokelewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula ili kuhudhuria mkutano huo ni pamoja na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Liberia, Mhe. Dkt. Jewel Howard-Taylor na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Uganda, Mhe. Jessica Allupo.
============================

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Liberia, Mhe. Dkt. Jewel Howard-Taylor (kushoto) amewasili nchini kushiriki Mkutano wa Wanawake na Vijana katika biashara kwenye Eneo Huru la Biashara Barani Afrika (AfCFTA) utakaofanyika kuanzia  tarehe 12 hadi 14 Septemba, 2022 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.
Dkt. Howard-Taylor amepokelewa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam tarehe 11 Septemba 2022.

Mhe. Dkt. Jewel Howard-Taylor (kushoto) akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (kulia) baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam tarehe 11 Septemba 2022.

==================================
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula pia amempokea Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Uganda Mhe. Jessica Allupo.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula akimpokea Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Uganda, Mhe. Jessica Allupo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam tarehe 11 Septemba 2022.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (kulia) akizungumza na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Uganda, Mhe. Jessica Allupo (kushoto) katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam tarehe 11 Septemba, 2022.

 Mhe. Allupo amewasili nchini kushiriki Mkutano wa Wanawake na Vijana katika biashara kwenye Eneo Huru la Biashara Barani Afrika (AfCFTA) utakaofanyika 
kuanzia  tarehe 12 hadi 14 Septemba, 2022 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.

===============================
Wakati huo huo Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula alipata  wasaa wa kuagana na Kiongozi wa Jumuiya ya Mabohola duniani, Mtukufu Syden Mufaddal Saifuddin aliyekuwa nchini kwa ziara. 


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula  akizungumza na Kiongozi wa Jumuiya ya Mabohora duniani, Mtukufu Syden Mufaddal Saifuddin katika Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.

Friday, September 9, 2022

WAZIRI MULAMULA ASAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO UBALOZI WA UINGEREZA NCHINI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Liberata Mulamula (Mb.) akisaini kitabu cha maombolezo katika Ubalozi wa Uingereza nchini kufuatia kifo cha Malkia Elizabeth II. Kulia ni Balozi wa Uingereza nchini, Mhe. David Concar 
  


Mkurugenzi Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Swahiba Mndeme  akisaini kitabu cha maombolezo katika Ubalozi wa Uingereza nchini kufuatia kifo cha Malkia Elizabeth II.

Mkurugenzi wa Kitengo cha Mawasiliano katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki , Balozi Mindi Kasiga (kulia) akisalimiana na Balozi wa Uingereza nchini, Mhe. David Concar (kushoto) alipowasili katika ubalozi wa Uingereza kutoa pole kufuatia kifo cha Malkia Elizabeth II.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Liberata Mulamula (kulia) akizungumza na Balozi wa Uingereza nchini, Mhe. David Concar (kushoto) alipowasili katika ubalozi wa Uingereza kutoa pole kufuatia kifo cha Malkia Elizabeth II.


Balozi wa Uingereza nchini, Mhe. David Concar akizungumza na Mhe. Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe, Balozi Liberata Mulamula (wa tatu kulia).

Mazungumzo yakiendelea.