Saturday, February 11, 2023

TANZANIA, IRAN KUSHIRIKIANA SEKTA ZA KIMKAKATI

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran zimeahidi kushirikiana katika sekta za kimkakati hususani kilimo, pamoja na biashara na uwekezaji kwa lengo la kukuza na kuimarisha diplomasia ya uchumi.

Hayo yamebainishwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) katika sherehe za maadhimisho ya miaka 44 ya siku ya Taifa ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na maadhimisho ya miaka 40 ya uhusiano wa kidiplomasia baina ya Iran na Tanzania zilizofanyika tarehe 10 Februari 2023 Jijini Dar es Salaam.

“Tanzania na Iran tumekuwa tukishirikiana katika maeneo mbalimbali, hadi sasa tumekuwa tukishirikiana katika sekta za elimu, afya, utalii, nishati, madini. Pia kwa sasa Irani imeonesha nia ya kuwekeza katika sekta ya kilimo hasa ukizingatia kilimo ni kipaumbele cha Serikali,” alisema Dkt. Tax

Waziri Tax ameongeza kuwa, Serikali itaendelea kushirikiana na Iran katika maeneo mapya ya kimkakati ikiwemo sekta ya kilimo ili kupata uzoefu katika maendeleo na uwekezaji wa kuifanya nchi kuwa na uwezo wa kuzalisha chakula cha kutosha pamoja na kuongeza viwanda. 

Akielezea kuhusu biashara na uwekezaji, Dkt. Tax alisema kuwa kupitia kongamano la wafanyabiashara na wawekezaji lililofanyika Mwezi Agosti, 2022 limefungua fursa za biashara na uwekezaji. “Tanzania inaendelea kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji ili kuwavutia wafanyabiashara na wawekezaji wengi zaidi kuwekeza nchini,” alisema Dkt. Tax

Naye Balozi Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini, Mhe. Hossein Alvandi Bahineh alisema kuwa Iran imekuwa na uhusiano wa kidiplomasia na Tanzania kwa miaka 40 hadi sasa na mataifa hayo yamekuwa yakishirikiana kijamii, kisiasa, kiuchumi na utamaduni kwa maslahi ya pande zote mbili.

Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Tanzania zimekuwa marafiki wa muda mrefu na itaendelea kushirikiana na Tanzania katika kukuza na kuimarisha sekta za kilimo, elimu, afya pamoja na biashara na uwekezaji kwa maslahi ya mataifa yote mawili.

Balozi Alvandi aliongeza kuwa mazingira ya biashara kati ya Iran na Tanzania yanaridhisha kwani hadi mwaka jana 2022 biashara kati ya Iran na Tanzania iliongezeka kutoka dola milioni 20 hadi dola milioni 70.

“Biashara kati ya Iran na Tanzania imeongezeka kutoka dola milioni 20 hadi dola milioni 70 mwaka jana, hii ni ishara kuwa uchumi wa mataifa yetu mawili unazidi kuimarika,” alisema Balozi Alvandi 

Tanzania na Iran zilianzisha uhusiano wa kidiplomasia mwaka 1983 na zimekuwa zikishirikiana katika sekta za biashara, kilimo, masoko, utalii, uwekezaji, afya, madini, nishati na utaalamu.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akiwasiliha hotuba yake katika sherehe za maadhimisho ya miaka 44 ya siku ya Taifa ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na maadhimisho ya miaka 40 ya uhusiano wa kidiplomasia baina ya Iran na Tanzania zilizofanyika tarehe 10 Februari 2023 Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akiwa amesimama na Balozi Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini, Mhe. Hossein Alvandi Bahineh katika sherehe za maadhimisho ya miaka 44 ya siku ya Taifa ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na maadhimisho ya miaka 40 ya uhusiano wa kidiplomasia baina ya Iran na Tanzania zilizofanyika tarehe 10 Februari 2023 Jijini Dar es Salaam

Balozi Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini, Mhe. Hossein Alvandi Bahineh akizungumza katika maadhimisho ya miaka 44 ya siku ya Taifa ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na maadhimisho ya miaka 40 ya uhusiano wa kidiplomasia baina ya Iran na Tanzania tarehe 10 Februari 2023 Jijini Dar es Salaam

Sehemu ya washiriki wakifuatilia maadhimisho ya miaka 44 ya siku ya Taifa ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na maadhimisho ya miaka 40 ya uhusiano wa kidiplomasia baina ya Iran na Tanzania tarehe 10 Februari 2023 Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akikata keki pamoja na Balozi Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini, Mhe. Hossein Alvandi Bahineh wakati wa maadhimisho ya miaka 44 ya siku ya Taifa ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na maadhimisho ya miaka 40 ya uhusiano wa kidiplomasia baina ya Iran na Tanzania zilizofanyika tarehe 10 Februari 2023 Jijini Dar es Salaam



WAZIRI TAX APOKEA NAKALA ZA HATI ZA UTAMBULISHO ZA MABALOZI WA MISRI, MAREKANI

 



Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akipokea nakala za Hati za Utambulisho za Balozi mteule wa Misri nchini, Mhe. Sherif Abdelhamid Ismail katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam
 


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akizungumza na Balozi mteule wa Misri nchini, Mhe. Sherif Abdelhamid Ismail katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akipokea nakala za Hati za Utambulisho za Balozi mteule wa Marekani nchini, Mhe. Michael Battle katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akimsikiliza Balozi mteule wa Marekani nchini, Mhe. Michael Battle katika Ofisi Ndogo za Wizara Jijini Dar es Salaam



Friday, February 10, 2023

DKT. TAX ASAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO UBALOZI WA UTURUKI

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) amesaini kitabu cha maombolezo Ubalozi wa Uturuki Jijini Dar es Salaam, kufuatia tetemeko la ardhi lililotokea Uturuki tarehe 6 Februari, 2023.

Baada ya kusaini kitabu cha maombolezo, Dkt. Tax ametoa salamu za pole kwa Serikali ya Uturuki na kuwasihi kuendelea kuwa wavumilivu wakati huu wa msiba mkubwa kwa Taifa hilo uliosabaisha vifo vya watu zaidi ya 18,000.

“Serikali ya Tanzania na Watanzania kwa ujumla tunaungana na Serikali ya Uturuki katika kuombeleza msiba huo mzito,” alisema Dkt. Tax.

Mwaka 1999 Uturuki ilikumbwa na tetemeko la ardhi ambapo watu wapatao 17,000 walipoteza maisha kutokana na tetemeko hilo. Kadhalika, mwaka 2011 ilikumbwa na tetemeko la ardhi katika mji wa Van lilipelekea vifo vya watu 500.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akisaini kitabu cha maombolezo Ubalozi wa Uturuki Jijini Dar es Salaam








TANZANIA YASHIRIKI MKUTANO WA 18 WA BARAZA LA MAWAZIRI LA KISEKTA LA UCHUKUZI, MAWASILIANO NA HALI YA HEWA WA JUMUIYA YA AFRIKA MASHARIKI


Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeshiriki Mkutano wa 18 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Uchukuzi, Mawasiliano na Hali ya Hewa (TCM) unaofanyika jijini Bujumbura, Burundi 

Ujumbe wa Tanzania katika Mkutano huo umeongozwa na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Fatma M. Rajabu

Mkutano huo ulianza tarehe 6 - 8 February 2023 kwa ngazi ya wataalamu waandamizi, ulifuatiwa na kikao cha ngazi ya makatibu wakuu uliofanyika tarehe 9 Februari 2023 na utakamilishwa kwa kuwakutanisha Mawaziri katika kikao kitakachofanyika tarehe 10 Februari 2023 jijini humo. 

Mkutano wa ngazi ya Makatibu Wakuu umepokea na kujadili taarifa za utekelezaji wa Programu na Miradi; Maamuzi; na Maagizo ya Mikutano ya awali katika sekta za Mawasiliano; Hali ya Hewa na Miundombinu ya Uchukuzi inayojumuisha sekta za Barabara, Vituo vya Huduma kwa pamoja Mipakani (OSBP), Reli, Usafiri wa anga na Bandari kwa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. 

Mkutano huo pia ulipokea taarifa ya utekelezaji wa Maagizo 12 kati 34 ya mikutano ya awali ya Baraza la Mawaziri wa sekta husika yaliyokamilika na maagizo mengine yaliyosalia utekelezaji wake upo katika hatua mbalimbali. 

Mkutano huo unahudhuriwa na washiriki kutoka nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kupitia sekta za ujenzi, uchukuzi, mawasiliano na fedha.
 Mkutano wa 18 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Uchukuzi, Mawasiliano na Hali ya Hewa (TCM) ukiendelea jijini Bujumbura, Burundi 
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Fatma M. Rajabu (kushoto) akifuatilia Mkutano wa 8 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Uchukuzi, Mawasiliano na Hali ya Hewa (TCM) unaoendelea jijini Bujumbura, Burundi. Kulia ni Balozi wa Tanzania nchini humo Mhe. Balozi Jilly Maleko
Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Fatma M. Rajabu (kushoto) akifuatilia Mkutano wa 8 wa Baraza la Mawaziri la Kisekta la Uchukuzi, Mawasiliano na Hali ya Hewa (TCM) unaoendelea jijini Bujumbura, Burundi

Thursday, February 9, 2023

TANZANIA YAJIZATITI KUTUMIA FURSA ZINAZOPATIKANA NDANI NA NJE YA NCHI KUKUZA UCHUMI


Serikali ya Tanzania inaendelea kutekeleza Diplomasia ya Uchumi kwa kushirikiana na nchi mbalimbali duniani ili kukuza  uchumi wa nchi kupitia fursa za biashara, uwekezaji na utalii zilizopo ndani na nje ya nchi.

 

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk, Bungeni leo tarehe 09 Februari,2023 wakati akijibu swali la  Mhe. Felista Njau, Mbunge wa Viti Maalum kuhusu umuhimu wa Serikali wa kuainisha nchi zenye fursa za biashara na uwekezaji ili kukuza pato la Taifa.

 

Amesema Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki kwa kushirikiana na Wizara za kisekta na Balozi za Tanzania imeendelea kutangaza fursa za biashara na uwekezaji zenye manufaa kwa Taifa na kwamba Wizara inaandaa Mpango wa Kitaifa wa kutekeleza Diplomasia ya Uchumi utakaojumuisha Sekta ya Umma na Sekta Binafsi ili kufikia malengo tarajiwa. 

 

Amesema Mpango huu ambao unatarajiwa kukamilika kabla ya mwezi Desemba 2023, pamoja na mambo mengine unalenga kuhakikisha fursa za biashara, uwekezaji na utalii zinakuwa na tija zaidi kwa wananchi wa Tanzania. Pia Mpango huo utajumuisha Sekta zote husika ikiwa ni pamoja na kuainisha maeneo muhimu ya kisekta yatakayo changia katika kukuza uchumi na pato la Taifa.

 

Akichangia hoja kuhusu mkakati wa utoaji elimu kwa wananchi kuhusu dhana ya Diplomasia ya Uchumi, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki,  Mhe. Dkt. Stergomena Tax, amesema Wizara inaendelea kutoa elimu kwa umma kupitia njia mbalimbali na kufafanua kwamba Mpango Mkakati wa Kitaifa wa Utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi unaoandaliwa pia utajumuisha Mpango  wa kutoa elimu kwa umma kuhusu dhana hiyo ili kuwawezesha wananchi kuielewa dhana hii na kuwawezesha kutumia fursa mbalimbali zinazotokana na ushirikiano kati ya Tanzania na nchi mbalimbali.


Kuhusu taarifa hasi zinazotolewa na vyombo vya kimataifa dhidi ya Tanzania, Mhe. Dkt. Tax amesema tayari Wizara imeanza kushirikiana na vyombo vya habari vya Nje hususan vile vinavyorusha matangazo yake kwa Kiswahili ili kupitia vyombo hivyo fursa  na taarifa chanya kuhusu Tanzania zitangazwe duniani kote.

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax akichangia hoja kuhusu Utekelezaji wa Diplomasia ya Uchumi wakati wa kipindi cha maswali na majibu kilichofanyika Bungeni jijini Dodoma tarehe 09 Februari, 2023
Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akijibu swali bungeni jijini Dodoma tarehe 09 Februari 2023
 

Wednesday, February 1, 2023

BALOZI LUVANDA AWASILISHA HATI ZA UTAMBULISHO, NEW ZEALAND

Balozi wa Tanzania nchini New Zealand mwenye makazi yake Tokyo, Japan, Mhe. Baraka Luvanda akisalimiana na Gavana Jenerali na Amiri Jeshi Mkuu wa New Zealand, Mhe. Cindy Kiro kabla ya zoezi la kuwasilisha Hati za Utambulisho lililofanyika tarehe 31 Januari 2023. 

Balozi wa Tanzania nchini New Zealand mwenye makazi yake Tokyo, Japan, Mhe. Baraka Luvanda akiwasilisha Hati za Utambulisho kwa Gavana Jenerali na Amiri Jeshi Mkuu wa New Zealand, Mhe. Cindy Kiro kwenye hafla iliyofanyika kwenye makazi ya Gavana huyo tarehe 31 Januari 2023. 

Balozi wa Tanzania nchini New Zealand mwenye makazi yake Tokyo, Japan, Mhe. Baraka Luvanda akiweka saini Kitabu cha Wageni alipowasili kwenye Makazi ya Gavana Jenerali na Amiri Jeshi Mkuu wa New Zealand, Mhe. Cindy Kiro kuwasilisha Hati za Utambulisho 

Balozi wa Tanzania nchini New Zealand mwenye makazi yake Tokyo, Japan, Mhe. Baraka Luvanda (wa tatu kutoka kulia) akiwa katika picha ya pamoja na Gavana Jenerali na Amiri Jeshi Mkuu wa New Zealand, Mhe. Cindy Kiro (katikati) baada ya hafla ya kuwasilisha Hati za Utambulisho iliyofanyika kwenye makazi ya Gavana huyo tarehe 31 Januari 2023. 

 

Tuesday, January 31, 2023

UBALOZI WA UFARANSA WAFUNGUA OFISI NDOGO JIJINI DODOMA


Balozi wa Ufaransa nchini Mheshimiwa Nabil Hajloui akimkaribisha Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax alipowasili eneo la Kilimani jijini Dodoma kwa ajili ya kufungua rasmi Ofisi ndogo ya Uwakilishi ya Ubalozi wa Ufaransa katika makao makuu tarehe 31 Januari 2023

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax akiwa na Balozi wa Ufaransa nchini Mheshimiwa Nabil Hajloui wakati nyimbo za Taifa za Tanzania na Ufaransa zikipigwa  alipowasili eneo la Kilimani jijini Dodoma kwa ajili ya kufungua rasmi Ofisi ndogo ya Uwakilishi ya Ubalozi wa Ufaransa katika makao makuu
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax akiwa na  Balozi wa Ufaransa nchini Mheshimiwa Nabil Hajloui akizindua rasmi Ofisi ndogo ya Uwakilishi ya Ubalozi wa Ufaransa katika eneo la Kilimani jijini Dodoma 



Balozi wa Ufaransa nchini Mheshimiwa Nabil Hajloui akizungmza wakati wa uzinduzi rasmi wa Ofisi ndogo ya Uwakilishi ya Ubalozi wa Ufaransa katika eneo la Kilimani jijini Dodomaakisikilizwa na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax  na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mhe. Rose Senyamule wa (kwanza kushoto) 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa ofisi ya Uwakilishi ya Ubalozi wa Ufaransa jijinii Dodoma 

Baadhi ya wageni waalikwa waliohudhuria uzinduzi wa ofisii ya Uwakilishi ya Ubalozi wa ufaransa wakifuatilia tukio hilo

Balozi wa Ufaransa nchini Mheshimiwa Nabil Hajloui akiagana na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax baada ya kukamilika kwa hafla ya uzinduzi wa  Ofisi ndogo ya Uwakilishi ya Ubalozi wa Ufaransa jijini Dodoma  tarehe 31 Januari 2023

 




 


 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb) ameupongeza Ubalozi wa Ufaransa nchini kwa kufungua Ofisi Ndogo ya Uwakilishi jijini Dodoma na kuzihamasisha Balozi nyingine kuendelea kuitikia wito wa kuhamia Makao Makuu ya Nchi.

Akizungumza katika ufunguzi wa Ofisi hiyo, Mhe. Dkt. Tax amesema anaupongeza ubalozi huo kwa kuitikia wito wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan alioutoa mwanzoni mwa mwaka 2023 wa kuwasihi Mabalozi kuhamia Makao Makuu ya Serikali jijini Dodoma.

“Tuko hapa kwa ajili ya kufungua Ofisi ndogo za Uwakilishi za Ubalozi wa Ufaransa nchini, baada ya Serikali kuhamia rasmi Dodoma, ofisi hii ni ya tatu baada ya zile za Ujerumani na China, niwapongeze sana kwa uamuzi wenu huu, mmeiunga mkono Serikali katika kuhamia kwake hapa Dodoma’, alisema Dkt. Tax.

Dkt. Tax ameuhakikishia na kuuahidi Ubalozi huo kuwa, Serikali itatoa msaada wowote watakaouhitaji ili kuiwezesha ofisi hiyo kufanya kazi zake kwa ufanisi na kwamba Serikali itaendelea kushirikiana nao katika kuhakikisha ndoto ya kuwa na ubalozi kamili inakamilika.

Amesema  hatua ya kufunguliwa kwa Ofisi hiyo ni muhimu katika kuimarisha uhusiano na urafiki uliopo baina ya Tanzania na Ufaransa  na kwamba ina dhamira ya kuupeleka uhusiano huo katika ngazi nyingine.

Ameeleza kuwa tayari Serikali imewapatia viwanja na hati Balozi zote na Taasisi za Kimatifa zenye uwakilishi nchini na kuongeza kuwa Serikali imewekeza kwa kiasi kikubwa katika jiji la Dodoma ili kuhakikisha Jiji hili linakuwa na miundombinu na huduma bora za kijamii zinazotosheleza mahitaji ya wakazi wake wote.

Ameongeza kusema ana imani kuwa wito wa Serikali wa kuhamia makao makuu ya nchi utaenziwa na kuungwa mkono na Balozi na Mashirika ya Kimataifa na kuihakikishia jumuiya ya wanadiplomasia nchini kuwa Serikali itatoa msaada wowote utakaohitajika ili kurahisisha uhamiaji wao jijini Dodoma.

Naye Balozi wa Ufaransa nchini Mheshimiwa Nabil Hajloui amesema Ufaransa imefungua Ofisi yake jijini Dodoma ikiwa ni hatua za kuunga mkono uamuzi wa Serikali ya Tanzania wa kuhamishia Makao Makuu yake jijini humo, lakini pia kurahisisha huduma mbalimbali za kibalozi kwa wananchi wa Dodoma na mikoa jirani.

Amesema wataendelea kushirikiana na Serikali katika kuimarisha uhusiano kwa manufaa ya pande zote mbili na kuahidi kuwa Ufaransa kupitia Shirika lake la Maendeleo la AFD itaendelea kushirikiana na Serikali katika jitihada zake za kuboresha na kuinua maisha ya wananchi wa Tanzania kupitia Sekta za Maji, Nishati, Afya, Kilimo na Elimu kwa Tanzania Bara na Zanzibar

Kufunguliwa kwa Ofisi hizo kunafanya Dodoma kuwa na ofisi tatu za Ubalozi baada ya zile za Ujerumani na China. Ofisi hizo ambazo zipo eneo la Kilimani jijini Dodoma zitatoa huduma mbalimbali kwa Serikali na wananchi wote kwa ujumla na zinajumuisha pia Ofisi za Shirika la Msaada la Ufaransa la Agence Francaise de Development (AFD).

 



TANZANIA INASHIRIKIANA NA COMESA KUPITIA AfCFTA- BALOZI MBAROUK

Naibu Waziri Mmambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk akijibu swali bungeni jijini Dodoma tarehe 31 Januari 2023


Tanzania inaendelea kushirikiana na nchi zinazounda Soko la Pamoja la Mashariki na Kusini mwa Afrika (COMESA) kupitia utekelezaji Mkataba wa Eneo Huru la Biashara Barani Afrika (AfCFTA) na pia kupitia Utatu unaoundwa na nchi za COMESA, Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC).

Naibu Waziri Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mbarouk Nassor Mbarouk amesema hayo bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Momba, Mhe. Condester Michael Sichalwe aliyetaka kujua kwa nini Tanzania haioni haja ya kujiunga tena na COMESA.

Amesema Tanzania ilikuwa miongoni mwa nchi 19 zilizokuwa waanzilishi wa Jumuiya ya Soko la Pamoja la Mashariki na Kusini mwa Afrika (COMESA) mwaka 1994. Hata hivyo, Tanzania ilijitoa katika COMESA mwaka 2000 kwa sababu ilikuwa ni mwanachama wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), ambapo baadhi ya nchi za jumuiya hizo pia ni wanachama wa COMESA.

Ameongeza kusema Tanzania pia ilijitoa COMESA baada ya kujiridhisha kuwa nchi haitaathirika kiuchumi kwa kuwa bado ni mwanachama wa EAC na SADC na kwamba lengo ni kulipunguzia taifa gharama hasa michango ya uanachama kwenye Jumuiya hizo.

Pia amesema kitendo cha Bunge cha kuridhia kwa Mkataba wa kuanzisha Eneo Huru la Biashara la Bara la Afrika (AfCFTA) hapo mwezi Septemba 2021, kunaifanya Tanzania kuendelea kushirikiana na nchi za COMESA.

“Ikumbukwe kuwa mwaka 2008 nchi za COMESA, EAC na SADC zilikubaliana kuanzisha Utatu na hivyo Tanzania inaendelea kushirikiana na COMESA kupitia Utatu huo wa COMESA–EAC-SADC,” alisema Mhe. Mbarouk.

 


FURSA ZA UTAFITI NCHINI JAPAN


 

TANZANIA NA FINLAND ZAAHIDI KUIMARISHA USHIRIKIANO KATIKA BIASHARA

Serikali za Tanzania na Finland zimeahidi kuendelea kuimarisha ushirikiano katika sekta zenye maslahi mapana ya kiuchumi kwa wananchi wa nchi hizi mbili ikiwemo biashara, utalii na uwekezaji.

Ahadi hiyo imetolewa katika mazungumzo baina ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax na Waziri wa Uchumi wa Finland, Mhe. Mika Lintilä walipokutana katika ofisi za Wizara jijini Dodoma tarehe 31 Januari 2023.

Katika mazungumzo hayo viongozi hao wamejadili juu ya kuimarisha ushirikiano katika sekta za biashara, uwekezaji, utalii, teknolojia ya habari na mawasiliano, usafirishaji, afya, kilimo, madini, nishati, elimu, mazingira na tafiti ili kupitia sekta hizo wananchi hususan wa Tanzania wanufaike kiuchumi na kijamii.

Dkt. Tax ameeleza kuwa amefurahishwa na ziara ya Mhe. Mika Lintilä na ujumbe wake nchini ikiwemo ujumbe wa wafanyabiashara alioambatana nao kutoka katika sekta za msingi kwa maendeleo ya pande zote mbili.

“Tanzania na Finland zina ushirikiano wa kihistoria ulioasisiwa kati ya nchi hizo mara baada ya uhuru wa Tanganyika mwaka 1962. Tupo tayari kuendelea kushirikiana na Finland katika kujenga uchumi wa kidigitali ili kuyafikia mapinduzi ya viwanda” alisema Dkt. Tax.

Vile vile, ametumia nafasi hiyo kuishukuru Serikali ya Finland kwa kuwa mwenyeji wa Mkutano wa 19 wa Nchi za Nordic na Afrika uliofanyika mwezi Juni 2022. Pia ameeleza kuwa Tanzania itaendelea kushiriki kwenye majukwaa mbalimbali ili kuwasilisha mchango wake katika masuala ya kikanda na kimataifa.

Kwa upande wake, Mhe. Mika Lintilä ameeleza kuwa Umoja wa Ulaya umetenga fedha kiasi cha Euro Billioni 300 kwa ajili ya kushirikiana na nchi zinazoendelea na zile za Kusini mwa Jangwa la Sahara katika sekta za maendeleo.

Vile vile, ameongeza kuwa tarehe 23 na 24 Februari 2023 kampuni za biashara zipatazo 40 kutoka Finland zitashiriki katika Jukwaa la Wafanyabiashara wa Tanzania na Umoja wa Ulaya litakalofanyika jijini Dar es Salaam.

Wakati huo huo, Waziri Lintilä amekutana na Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji ambapo viongozi hao wamekubaliana kuimarisha ushirikiano katika masuala ya biashara na uwekezaji ili kukuza uwiano wa biashara kati ya nchi hizi mbili ambao bado ni mdogo.

Pia Dkt. Kijaji ameongeza kuwa, Tanzania itaendelea  kuongeza samani ya bidhaa zake kama mbao, chakula na madini ili kuziwezesha kuingia katika soko la kimataifa ikiwemo Finland.

Waziri Lintilä yupo nchini kwa ziara ya siku nne (4) ambapo ameambatana na kundi la wafanyabiashara wapatao 18 kutoka katika sekta mbalimbali za kiuchumi ili kujionea maeneo mbalimbali ya uwekezaji  na biashara.

 

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (kati)akizungumza na Waziri wa Uchumi wa Finland, Mhe. Mika Lintilä (hayupo pichani)  katika ofisi za Wizara jijini Dodoma tarehe 31 Januari 2023. Kushoto ni Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Swahiba Mndeme na kulia ni Afisa Mambo ya Nje, Bw. Albert Philip.

Waziri wa Uchumi wa Finland, Mhe. Mika Lintilä (kulia) akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (hayupo pichani) katika ofisi za Wizara jijini Dodoma tarehe 31 Januari 2023. Pembeni ya Mhe. Lintilä ni Balozi wa Finland nchini, Mhe. Theresa Zitting.

Mazungumzo yakiendelea.

Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji akisalimiana na Waziri wa Uchumi wa Finland, Mhe. Mika Lintilä alipomtembelea ofisini kwake jijini Dodoma tarehe 31 Januari 2023. 

Dkt. Tax akimkabidhi zawadi Mhe.Mika Lintilä


Monday, January 30, 2023

DIPLOMATIC CORPS IN TANZANIA REMINDED TO OBSERVE THE VIENNA CONVENTION

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax (katikati), Naibu Waziri Mhe. Balozi  Mbarouk Nassor Mbarouk (kushoto) na Naibu Katibu Mkuu Balozi Fatma Rajab (kulia) wakiwa kwenye Mkutano na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya  Kimataifa waliopo nchini uliofanyika jijini Dodoma.
Naibu Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Fatma Rajab  akizungumza wakatika wa Mkutano kwenye Mkutano baina ya Wizara na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya  Kimataifa waliopo nchini uliofanyika jijini Dodoma.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb) akizungumza  kwenye Mkutano baina ya Wizara na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya  Kimataifa waliopo nchini uliofanyika jijini Dodoma.
Sehemu ya Mabalozi wa Wakifuatilia Mkutano 
Sehemu ya Mabalozi wa Wakifuatilia Mkutano 
Mkutano baina ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya  Kimataifa waliopo nchini ukiendelea jijini Dodoma
Mkutano baina ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya  Kimataifa waliopo nchini ukiendelea jijini Dodoma
Balozi wa Rwanda hapa nchini Mhe. Meja Jenerali Charles Karamba akichangia jambo  kwenye Mkutano baina ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya  Kimataifa waliopo nchini uliofanyika jijini Dodoma. 
Balozi wa Ujerumani hapa nchini Mhe. Regine Hess akichangia jambo  kwenye Mkutano baina ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya  Kimataifa waliopo nchini uliofanyika jijini Dodoma
Sehemu ya Wakuu wa Idara wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia Mkutano baina ya Wizara na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya  Kimataifa waliopo nchini uliofanyika jijini Dodoma.
Sehemu ya Wakuu wa Idara na Vitengo wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia Mkutano baina ya Wizara na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya  Kimataifa waliopo nchini uliofanyika jijini Dodoma.
Balozi wa Rwanda hapa nchini Kanali Mstaafu Fredy Mwesigye akichangia jambo  kwenye Mkutano baina ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya  Kimataifa waliopo nchini uliofanyika jijini Dodoma. 
Sehemu ya Mabalozi wa Wakifuatilia Mkutano 
Mwakilishi wa Ubalozi wa Marekani hapa nchini akichangia jambo kwenye Mkutano baina ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya  Kimataifa waliopo nchini uliofanyika jijini Dodoma
Meza Kuu wakiwa katika picha ya pamoja na Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini mara baada ya Mkutano baina  yao, Wizara na Wawakilishi wa Mashirika ya  Kimataifa waliopo nchini uliofanyika jijini Dodoma.
Meza Kuu wakiwa katika picha ya pamoja na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa hapa nchini mara baada ya Mkutano baina yao, Wizara na Mabalozi wanaoziwakilisha Nchi zao hapa nchini uliofanyika jijini Dodoma
Meza Kuu wakiwa katika picha ya pamoja na Menejimenti ya Wizara 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb) akizungumza  na Waandishi wa Habari mara baada ya  Mkutano baina ya Wizara na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa waliopo nchini uliofanyika jijini Dodoma
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb) akifafanua jambo kwenye Mkutano baina ya Wizara na Mabalozi na Wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa waliopo nchini uliofanyika jijini Dodoma.