Thursday, February 12, 2015

Mhe. Rais Kikwete amwapisha rasmi Balozi Haule



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete akimwapisha aliyekuwa  Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. John Michael Haule kuwa Balozi wa Tanzania nchini Kenya. Balozi John Michael Haule anachukua nafasi iliyoachwa  wazi na Balozi Batilda Buriani ambaye amehamishiwa Tokyo, Japan. Hafla hiyo ilifanyika Ikulu, Dar es Salaam tarehe 12 Februari, 2015
Balozi Haule akisaini kiapo chake mbele ya Mhe. Rais Kikwete
Mhe. Rais Kikwete akimkabidhi Balozi Haule vitendea kazi
Baadhi ya Wakurugenzi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakishuhudia Balozi Haule (hayupo pichani) akila kiapo. Kulia ni Balozi Joseph Sokoine, Mkurugenzi wa Idara ya Ulaya na Amerika na Balozi Simba Yahya, Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati.
Balozi Yahya (mwenye tai nyekundu) kwa pamoja na Balozi Sokoine, Bi. Mindi Kasiga, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Bw. James Bwana (kulia), Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Itifaki katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wakifuatilia tukio la kuapishwa kwa Balozi Haule (hayupo pichani)

Bi. Zuhura Bundala (mwenye kilemba), Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa akiwa pamoja na Bibi Rosemary Jairo (mwenye suti nyeusi), Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Diaspora wakifuatilia tukio la uapisho. Nyuma ya Bi. Bundala ni Bw. Nigel Msangi, Mkurugenzi wa Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu.
Mhe. Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Haule na Viongozi Wakuu wa Serikali akiwemo Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, mhe. Dkt. Mohamed Gharib Bilal (wa tatu kushoto), Waziri Mkuu, Mhe. Mizengo Pinda (wa nne kulia), Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard Membe (wa pili kulia) na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje, Mhe. Dkt. Mahadhi Juma Maalim (kulia).
Mhe. Rais Kikwete (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Haule na Mkewe
Mhe. Rais Kikwete akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Haule pamoja na Waziri Membe, Naibu Waziri, Wakurugenzi na Wakuu wa Vitengo wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.
Mhe. Dkt. Mahadhi akisalimiana na Mama Haule mara baada ya Balozi Haule kuapishwa
Balozi Haule akipongezwa na Balozi Mbelwa Kairuki, Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia.
Balozi Haule akipongezwa na Mkuu wa Kitengo cha Ukaguzi, Bw. Mathias Abisai
Balozi Haule akipongezwa na Mkuu wa Kitengo cha Uhasibu na Fedha katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Paul Kabale
Balozi Haule akipongezwa na Mkurugenzi wa Idara ya Ununuzi na Ugavi katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Balozi Haule akipongezwa na Katibu wa Waziri Membe, Bw. Thobias Makoba


Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Rajabu Gamaha akimpokea na kumkaribisha Balozi Haule  Wizarani rasmi mara baada ya kuapishwa
Sehemu ya Watumishi wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikinao wa Kimataifa wakimpokea kwa shangwe Balozi Haule mara baada ya kuapishwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Kenya
Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Utawala, Bibi Amisa Mwakawago akimkabidhi maua Balozi Haule mara baada ya kuwasili Wizarani akitokea kuapishwa
Balozi Haule akiwashukuru baadhi ya Watumishi wa Wizara kwa mapokezi mazuri na ushirikiano
Baadhi ya Watumishi wa Wizara wakiwa na nyuso za furaha wakati wa mapokezi ya Balozi Haule (hayupo pichani)

Picha na Reginald Philip



Dkt. Mahadhi mgeni rasmi maadhimisho siku ya Taifa la Iran

 Balozi wa Iran nchini Tanzania,Mh.Mehdi Aghajafari akimpokea Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh.Dkt.Mahadhi Juma Maalim (Mb) alipowasili katika hafla ya kusherehekea siku ya Taifa la Iran iliyofanyika kwenye makazi ya Balozi huyo Jijini Dar es Salaam jana usiku.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh.Dkt.Mahadhi Juma Maalim (Mb) akizungumza mbele ya wageni mbalimbali walioalikwa katika hafla ya siku ya Taifa la Iran iliyofanyika kwenye makazi ya balozi wa Iran Jijini Dar es Salaam.
 Balozi wa Syria nchini, Mhe.Abdulmonem Annan (kushoto) Jaji mkuu wa Tanzania,  Mhe. Mohamed Chande Othman (katikati) na Balozi wa Yemen nchini, Mhe.Abdulla Hassan Alamri wakimsikiliza kwa makini Mgeni Rasmi kwenye hafla ya Siku ya Iran, Naibu waziri Dkt. Mahadhi.
 Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Hassan Simba Yahaya (kulia) akiwa na Maafisa kutoka Wizara hiyo Bw. Mkumbwa Ally (kushoto) na Bw. Leonce Bilauri (katikati) wakifuatilia hotuba ya Naibu Waziri (hayupo pichani) katika hafla hiyo.

 Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe.Dkt.Mahadhi Juma Maalim (Mb.) akisalimiana na Balozi wa Syria nchini Mhe. Abdulmonem Annan kwenye sherehe hizo.
 Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe.Mohamed Chande Othman akizungumza jambo na  Mhe.Dkt.Mahadhi kwenye hafla ya siku ya Iran.

Picha na Reuben Mchome
================================================


STATEMENT BY HON. DR. MAHADHI JUMA MAALIM, (MP) DEPUTY MINISTER OF FOREIGN AFFAIRS AND INTERNATIONAL COOPERATION OF THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA ON THE OCCASION OF THE NATIONAL DAY OF THE ISLAMIC REPUBLIC OF IRAN DAR ES SALAAM, 11TH FEBRUARY, 2015

Your Excellency Ambassador Mahdi, Aghajafari Ambassador of the Islamic Republic of Iran;
Your Excellency Juma Alfani Mpango, Ambassador of the Republic of Congo and Dean of the Diplomatic Corps;
Your Excellency Nasri Abujaish, Ambassador of the State of Palestine, and Dean of the Arab Group
Your Excellencies Ambassadors and High Commissioners;
Your Excellencies Heads of Diplomatic Missions;
Your Excellencies Heads of International Organizations;
Distinguished Guests;
Ladies and Gentlemen,

I feel very honoured to stand before you on this special evening when we mark the auspicious event of the 36th National Day of the Islamic Republic of Iran. Indeed it is a particular privilege to join you all this evening as I represent the Government and the people of the United Republic of Tanzania to celebrate this historic day in the history of your beautiful country Your Excellency.
Your Excellency,
Distinguished Guests,
Ladies and Gentlemen,
At this juncture, allow me therefore, on behalf of the Government and the People of the United Republic of Tanzania, to take this opportunity to extend to Your Excellency, and through you to the Government and the People of the Islamic Republic of Iran, our profound and heartfelt congratulations on the occasion of celebrating the 36th Anniversary of the Islamic Revolution of your country.
Your Excellency,
As we join you in this auspicious occasion, I wish to express my satisfaction on the bilateral relations that so happily exist between our two countries and our peoples despite being geographically separated by a long distance.
Such a good relationship can be traced back 1,000 years ago, when Iranians, then under the Shiraz Empire sailed to East Africa.

Tanzania and Iran also have a connection of culture, where there is some similarities of words in both Swahili as well as Persian languages. The Swahili words, "chai" = tea, "achari" = pickle, "serikali" = government, "diwani" = councillor, "sheha" = village councillor, are some of the words also used in Persian bearing testimony to the older connections with Persian merchants. 

Your Excellency,
Distinguished Guests,
Ladies and Gentlemen,

Our two countries already have a good framework for bilateral cooperation.
This is the Joint Permanent Commission (JPC), to coordinate cooperation in the trade, economic, technical and cultural spheres. We are all aware of the inherent obstacles that have militated against the role initially envisaged for the Joint Commission. It is our duty, to learn from our experiences and work together to find ways to make (JPC) arrangement more effective to strengthen our cooperation.

The two countries maintain good cooperation in different sectors; these include health, agriculture, culture, and from vocational to higher education. The two countries are geared to expand and strengthen cooperation in many areas of mutual interests of both countries.

At the Government level there have been exchange of visits at the national levels, to mention a few and recent ones include the then First Vice President of the Islamic Republic of Iran who visited Tanzania in 2012 and the then Minister of Information, Youth, Culture and Sport Dr. Emmanuel Nchimbi visited Iran in 2012. Last week Hon. Dr. Mohammad Javad Zarif, Foreign Minister of Iran, was in our country for a two day official visit.

At global spheres, both countries have been cooperating in all matters of common concerns in Non Alignment Movements (NAM) and United Nations (UN). Allow me at this occasion to reaffirm our commitment to strengthen the close cooperation that exists between our two friendly countries and people.

Your Excellency,
In contemporary world, we all recognize the power and position of private sector.
Thus, the existing friendly relations between our two countries are set to be the corner stone for further expansion and deepening in trade and investment between our private sectors. The just recent visit by Hon. Dr. Zarif to Tanzania with heavy weight CEOs and other prospective investors from Iran to Tanzania set a stepping stone for forging a close economic cooperation between the two countries by increasing trade and investments. Investors from Iran had fruitful discussions with their counterparts organized by Tanzania Chambers of Commerce, Industries and Agriculture (TCCIA).

Through this spirit of enhancing strong cooperation, Tanzania invites more investors from Iran to come to Tanzania to explore opportunities for investment for mutual benefit of both countries. We can expand economic relations to include areas like agribusiness, agro-processing, iron ore and ore extraction and processing, banking and tourism. To walk the talk, I am very happy to note that during the visit by Hon. Zarif, Tanzania and Iran have signed Bilateral Agreement on the Promotion and Protection of the Investments between the two Countries. On the same vein, the third round of negotiations on Avoidance of Double Taxation and Prevention from Fiscal Evasion (DTA) are underway.

Your Excellency,
Distinguished Guests,
Ladies and Gentlemen,
Your Excellency, once again, it is an honour for me to share with you this celebrations of your great country National Day, and I wish to reiterate our sincere congratulations to Your Excellency and  through you, to the Government and brotherly people of the Islamic Republic of Iran, for marking 36th anniversary of your great Islamic Revolution.

We wish you more success in the coming years and decades.
Thank you all for listening.



Wednesday, February 11, 2015

Cuban Ambassador visits SUZA

An official visit of Cuban Ambassador to Tanzania His Excellency Mr. Jorge Luis Lopez Tormo (with white shirt in the centre) at the State University of Zanzibar (SUZA) on Wednesday 11th February, 2015. On the Ambassador’s left is his host, Prof. Idris A. Rai, the SUZA Vice Chancellor.
During this official visit, Prof. Rai and his guest discussed on various issues including how Cuban government through her higher learning institutions collaborate with SUZA in education related matters.
The Cuban government through the Zanzibar Ministry of Health currently provides academicians teaching at the School of Health and Medical Sciences of the State University of Zanzibar.

Tuesday, February 10, 2015

Press Release

H.E. Hassan Rouhani, President of Iran


PRESS RELEASE

His Excellency Dr. Jakaya Mrisho Kikwete, President of the United Republic of Tanzania has sent a congratulatory message to His Excellency Hassan Rouhani, President of the Islamic Republic of Iran on the occasion of celebrating 36th Anniversary of the Islamic Revolution of Iran. The message reads as follows;

“Your Excellency
Hassan Rouhani,
President of the Islamic Republic of Iran,
TEHRAN

Your Excellency and Dear Brother,

On behalf of the Government and People of the United Republic of Tanzania and indeed on my own behalf, I would like to take this opportunity to extend to Your Excellency and through you, to the Government and People of the Islamic Republic of Iran our profound congratulations and best wishes on this historic occasion of celebrating the 36th anniversary of the Islamic Revolution of Iran.

The People of Tanzania and Iran enjoy cordial relations cemented by historic and cultural bonds dating back long ago. These relations provide a strong foundation for fraternal relations between our two countries that have been nurtured and developed by successive leadership in our two countries. In that regard, Tanzania and Iran maintain close cooperation in a number of important areas such as health and education. We wish to consolidate further and expand these relations to include other sectors such as transport, trade, investments, technology, oil, gas and communication.  

Your Excellency,

I would like to assure you of my personal commitment as well as that of my Government to continue working closely with your Government at bilateral and international levels. It is my sincere hope that our traditional cooperation through NAM and the UN aimed at enhancing peace and security as a basis for socio-economic development not only in our countries but also at global level.

While wishing you continued personal good health, happiness and prosperity for the people of Iran, please accept, Your Excellency the assurances of my highest consideration”.

Issued by: The Ministry of Foreign Affairs and International Cooperation, Dar es Salaam
10th February, 2015

Monday, February 9, 2015

Hotuba ya Waziri Membe kwenye Maadhimisho ya Kanisa la Wasabato SDA

Waziri Membe akiwahutubia mamia ya Waumini wa Kanisa la Sabatoikiwa ni siku ya kilele cha Kongamano la Kimataifa la Utume kwa  Makanisa ya Sabato.  Wengine katika picha waliokaa ni Rais wa Kanisa hilo duniani, Askofu Wilson na Mkewe pamoja na Mhe. Wasira wakimsikiliza.
=============================


Before I start my speech, let me also recognize the presence of Honorable Minister Stephen Wasira the Seventh Day Adventist disciple, who has traveled 500 kilometers to be here. Mheshimiwa Wasira karibu sana.

Before I continue with my speech let me also mention other government officials who are also members of the SDA apart from Honorable Wasira;
The Chief Secretary, Hon. Sefue is an SDA member,
The Attorney General of Tanzania Mr. Masaju is an SDA member,
The Permanent Secretary Mr. Maswi of Energy and Mineral, is an SDA member,

So, I mean there are so many others in government that are not only members but they acknowledge many good things that the SDA has been doing.
….continue in English version, see the Swahili translation….


Before I start my speech, let me also recognize the presence of Honorable Minister Stephen Wasira the Seventh Day Adventist disciple, who has traveled 500 kilometers to be here. Mheshimiwa Wasira karibu sana.

Before I continue with my speech let me also mention other government officials who are also members of the SDA apart from Honorable Wasira;
The Chief Secretary, Hon. Sefue is an SDA member,
The Attorney General of Tanzania Mr. Masaju is an SDA member,
The Permanent Secretary Mr. Maswi of Energy and Mineral, is an SDA member,

So, I mean there are so many others in government that are not only members but they acknowledge many good things that the SDA has been doing.
….continue in English version, see the Swahili translation….


Kwa muhtasari tu kwa Watanzania mlioko wengi, na Watanzania wanaotusikiliza;

Nimemshukuru Rais wa Baraza Kuu la Makanisa ya Sabato Duniani, kwa kujumuika nasi na kuamua Tanzania kuwa mwenyeji wa Kongamano hili kubwa sana la bara la Afrika.

Na ni imani yangu kwamba mtapokea salamu hizi nilizotoa kwa niaba ya Serikali…...

Nimemshukuru kwa mwaliko wake kwangu kuja kujumuika nanyi na kufunga Kongamano hili. Nimekubali kwa sababu mbili, kwanza, jambo lenyewe hili la kiroho mnalosimamia na kulifanya ni jambo jema sana kwa ustawi wetu sote. Pili, kongamano hili ni la kimataifa na hivyo linauhusiano na kazi yangu ya uanadiplomasia. Katika miaka 9 ya kuwa Waziri wa Mambo ya Nje na miaka 8 ya kuwa Mshauri wa Balozi wa Tanzania nchini Canada, nimejifunza kuwa diplomasia na hofu ya Mungu/imani vikifanya kazi kwa kushirikiana, hakuna changamoto yoyote ya kidunia isiyoweza kukabiliwa. (MAKOFI)

 Nimezungumzia uhusiano kati ya Serikali na Dini. Nimesema kuwa vitu hivi viwili havitenganishiki, ni sura mbili za sarafu. Kwa sababu, binadamu ni mwili na roho na kila kimoja hakina budi kuendelezwa. Serikali inashughulika na miili na akili, Dini zinashughulika na roho. Dini na Serikali zikifanya kazi pamoja sawasawa, tutahitaji sheria chache, polisi wachache, magereza machache. Dunia itakuwa mahala pazuri pa kuishi. Tunahitajiana.(MAKOFI)

Wenzetu wa vyombo vya dini wanahubiri amani wanakiri imani, sisi wanadiplomasia na Serikali tunatengeneza amani na wakati mwingine tunatumia vyombo vya dola kuitengeneza hiyo amani. Kwa hiyo lengo letu ni moja, kuleta amani, utulivu, katika nchi. Wenzetu njia yao ni nyembamba --sorry-- ni nyembamba lakini ina mapana na ni nzuri zaidi, kuliko ile tunayoitumia sisi. (MAKOFI)

Lakini diplomasia na dini zinakutana kwenye kukuza amani, ulinzi na usalama duniani.

Lakini pia tunakutana kwenye maadili. Viongozi wanaolelewa vizuri na dini zao, wanakuwa waadilifu. Na SDA ni miongoni mwa dini zinazoweka viongozi wazuri sana wa nchi yetu. (MAKOFI)

Na kwasababu hiyo basi, unapoona diplomasia inatengeneza mahusiano mazuri ya dunia, dunia inaangalia uadilifu kwanza, kama kigezo cha uongozi bora, na kama kigezo cha watu wenye amani na utulivu. Na kawaida Serikali, diplomasia na dini hata Rais mwenyewe, tunakutana tunapozungumzia masuala ya uadilifu wa viongozi wake. (MAKOFI)

Tunzeni hiyo, hubirini uadilifu, na mshiriki katika kutengeneza viongozi bora kwa misingi ya uadilifu. (MAKOFI)

Lakini jingine, nimeshukuru sana Kanisa la Sabato kwa kazi na mwenendo mzuri unaofanywa katika nchi yetu. Unapoona kwamba watu milioni nne waliomo nchini kwetu, wa SDA, wana shule za msingi 10, wana shule za sekondari 15, wana vyuo vikuu 2, wana hospitali kubwa 2, wana vituo vya albino vinavyofanya kazi hapa nchini. (MAKOFI)

Hivi kama kingekua chama cha siasa, nani angeshindwa kuwapa ushindi wa utawala wa nchi hii. (MAKOFI)

Nani angeshindwa kuwapa ushindi. Lakini ukiachia hayo, ni Chama cha Mapinduzi peke yake chenye kumudu kazi hiyo. (MAKOFI, VIGELEGELE, VICHEKO)

Lakini naomba niweke wazi kabisa, kama chombo cha dini, kama SDA, kinajali wananchi wake, kitaacha vipi kupanuka kutoka watu 15,000 mwaka 1960 hadi kufikia watu milioni nne mwaka 2012. (MAKOFI) Wataacha vipi kupanuka na kuwa watu wengi kwa huduma hii, wanayoitoa kwa wananchi. (MAKOFI)

Nawapongeza sana watu wa SDA, mbele ya kiongozi wenu wa dunia, kwa kazi nzuri mnayoifanya na shule mnayofundisha Watanzania kwamba ukitaka kuongoza Watanzania, fanya kama SDA. (MAKOFI)

Nalipongeza kanisa la SDA kuwa mfano mzuri wa ustahimilivu na uvumilivu wa dini na imani katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Katika miaka yangu yote ya nafasi yangu ya uwaziri, na kaka yangu Mzee Wasira ataniunga mkono kwenye hili, sijawahi kusikia mgogoro wa kimatatizo wala mfarakano unaoongozwa na SDA (MAKOFI) dhidi ya madhehebu mengine, au dhidi ya wananchi. (MAKOFI)

Mpo, mnafanya kazi zenu, mnachapa shuguli zenu kwa amani na utulivu, hamjachokoza mtu, na hamtachokoza mtu, na hiyo ni sifa mojawapo ya nchi yenye amani duniani. (MAKOFI)

Hongereni sana wana SDA. (MAKOFI)

Narudia, kama wananchi wote wa dini zote tukiiga mfano wenu, Tanzania tutasonga mbele kama Taifa. (MAKOFI)

Nawashukuruni kwa kunisikiliza na ninawatakia maandalizi mazuri ya kongamano la kidunia litakalofanyika baadae mwaka huu huko Marekani. (MAKOFI)

Saturday, February 7, 2015

Waziri Membe atoa rai kwa madhehebu kuombea uadilifu kwa viongozi

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,  Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) (wa pili  kulia), akiongozana na Rais wa Baraza Kuu la Makanisa ya Sabato Duniani,  Askofu Ted Wilson (wapili  kushoto),  Waziri wa Kilimo, Mhe. Stephen  Wassira (kushoto), pamoja  na  Mchungaji Blasius Luguri, Mwenyeji wa Kongamano la Kimataifa la Utume  kuingia katika Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam. Mhe. Membe alikuwa mgeni rasmi katika Sherehe za ufungaji Kongamano la Kimataifa la Utume kwa Kanisa la Sabato  lililofanyika hapa nchini na kuyashirikisha Mataifa zaidi ya 20.

Waziri wa mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa Mh. Bernard Kamilius Membe akijumuika na Waamini wa Kanisa la Sabato katika kuimba wimbo wa Taifa katika Sherehe za ufungaji Kongamano la Kimataifa la Utume kwa Kanisa la Sabato  lililofanyika jijini Dar es Salaam.

  Waziri Membe akiwahutubia mamia ya Waumini wa Kanisa la Sabatoikiwa ni siku ya kilele cha Kongamano la Kimataifa la Utume kwa  Makanisa ya Sabato.  Wengine katika picha waliokaa ni Rais wa Kanisa hilo duniani, Askofu Wilson na Mkewe pamoja na Mhe. Wasira wakimsikiliza.
Rais wa Baraza Kuu la Makanisa ya Sabato Duniani,  Askofu Wilson akimpongeza Waziri Membe mara baada ya kumaliza kuwahutubia Waumini wa kanisa hilo waliokusanyika Uwanja wa Taifa kwa ajili ya Kongamano la Kimataifa lilililofikia kilele leo.
Waumini wakishangilia na  kufurahia  hotuba nzuri iliyotolewa na Waziri Membe
Kikundi cha watoto kikitoa burudani katika maadhimisho hayo.
Waziri Membe akizungumza na Askofu Wilson kabla ya kuhutubia
Mazungumzo yakiendelea
Waziri Membe (Katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Askofu wilson na Mkewe (wapili kutoka kushoto), na wa pili kutoka kulia ni Mchungaji Blasius Luguri na mkewe.

Picha na Reginald Philip

Waziri Membe atoa rai kwa madhehebu kuombea uadilifu kwa viongozi

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard Membe ametoa rai kwa waumini wa Kanisa la Waadiventista Wasabato nchini kushiriki kikamilifu katika kutengeneza viongozi bora wa Serikali wanaozingatia misingi ya uadilifu, upendo na unyenyekevu.
Waziri Membe ameyasema hayo wakati akitoa hotuba ya kufunga Kongamano la Kimataifa la Utume la Kanisa la Waadventista Wasabato lililofanyika katika Uwanja wa Taifa, Jijini Dar es Salaam tarehe 07 Februari, 2015.
Mhe. Membe alisema kuwa Dini na madhehebu yanayo nafasi kubwa katika kujenga jamii yenye maadili na hofu ya Mungu wakiwemo viongozi na hivyo kupelekea taifa kuwa na amani, upendo na mshikamano. Alieleza kuwa kama Waziri wa Mambo ya Nje, amejifunza kuwa diplomasia na hofu ya Mungu vikifanya kazi pamoja hakuna changamoto yoyote isiyoweza kukabiliwa.
“Dini na Diplomasia vina husiana pale masuala ya amani, ulinzi na usalama yanapoguswa. Hivyo nawaomba mshiriki katika kutengeneza viongozi bora katika jamii zetu kwa misingi ya uadilifu ambao watasimamia amani na kujiepusha na vitendo viovu ikiwemo rushwa,” alisema Mhe. Membe.
Aidha, alilipongeza Kanisa hilo kwa kuwa mfano mzuri wa ustahimilivu na uvumilivu wa kidini hapa nchini. Alieleza kwamba kamwe hajawahi kusikia Kanisa la Waadiventista Wasabato limeingia katika mgogoro na Serikali, dhehebu au dini nyingine na hilo ni funzo kubwa kwa Watanzania, kwamba kutofautiana kiitikadi, kidini, kikabila au rangi si sababu tosha ya kuwagombanisha na kuvuruga amani ya nchi.
“Nalipongeza Kanisa lenu kwa kuwa mfano mzuri wa uvumilivu wa kidini na imani, mnaendesha mambo yenu kwa uvumilivu mkubwa  na kushirikiana na dini zote na hili linatufundisha kuwa kutofautiana kwetu sio sababu tosha ya kugombana” alisisitiza Membe.
Pia, Mhe. Membe alilihakikishia Kanisa hilo dhamira ya Serikali ya kuendelea kushirikiana nalo kwa ajili ya ustawi wa nchi na kufafanua kuwa Serikali itaendelea kulinda uhuru wa kuabudu kwa dini zote kama inavyoelezwa kwenye Katiba ya nchi. “Serikali inao wajibu wa kusaidia dini na madhehebu kufanyakazi  kwa uhuru. Bahati nzuri Katiba inayopendekezwa imezingatia kulinda uhuru huo hivyo tuiunge mkono” alifafanua Waziri Membe.
Vilevile alilisifu Kanisa hilo kwa kuanzisha miradi ya huduma zikiwemo Shule15 za Sekondari na Msingi, Chuo Kikuu na Hospitali mbili ambavyo vinatoa mchango mkubwa kwa Serikali na Wananchi kwa ujumla.
Awali akimkaribisha Waziri Membe kufunga Kongamano hilo, Rais wa Baraza Kuu la Makanisa ya Sabato Duniani, Askofu Ted Wilson alisema kuwa anawaombea  Viongozi wa Tanzania waendelee kuwa na maono kwa ajili ya kuwatumikia wananchi  na kwamba wakimtumaini Mungu atawawezesha kupata maono mapya kwa ajili ya kulitumikia Taifa hili.
Kwa upande wake, Mwenyeji wa Mkutano huo, Mchungaji Blasius Luguri aliipongeza Tanzania kwa kudumisha amani ambayo imepelekea Tanzania kuchaguliwa kuwa mwenyeji wa Kongamano hilo ulioyashirikisha Mataifa zaidi ya 20. Aidha, alimwomba Mhe. Membe kufikisha ujumbe kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa wana imani na Tanzania kuwa ni nchi ya amani, usalama na utulivu.
Kanisa la Sabato ni Kanisa linalokua duniani likiwa na Waumini milioni 307 huku Waumini milioni 30 wakiwa Afrika na takriban milioni 5 wakiwa Tanzania.

-Mwisho-