Friday, July 1, 2016

Rais Dkt. John Pombe Magufuli ampokea Rais wa Jamhuri ya Rwanda Mhe.Paul Kagame

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na  Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. Mhe. Paul Kagame yupo nchini kwa ziara ya siku mbili kuanzia leo, ambapo anatarajiwa kufungua Maonyesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa ya Sabasaba yanayofanyika jijini Dar es Salaam 
 Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame akiwa na mkewe mama  Jeannette Kagame wakipokea zawadi ya maua mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Mhe. Paul Kagame mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege jijini Dar es Salaam.


Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame akikagua gwaride la heshima mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege. 
Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame akiwa na mwenyeji wake, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege jijini Dar es Salaam.
 Waheshimiwa Marais wa Tanzania na Rwanda wakiangalia vikundi vya ngoma vilivyokuwa vikitumbuiza katika uwanja wa ndege.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mgeni wake wakisalimia wananchi waliofika viwanja vya Ikulu  kumlaki mgeni mara baada ya kuwasili.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli (wa sita kulia), akiwa katika Mkutano na Mgeni wake Mhe. Rais Paul Kagame pamoja na viongozi waandamizi wa Serikali wa pande zote mbili.
 Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame akizungumza na Wanahabari mara baada ya kumaliza mazungumzo na Mhe. Rais Dkt. Magufuli.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wanahabari mara baada ya kumaliza mazungumzo na Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame.

Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb)(kushoto) na  Rwanda Mhe. Louise Mushikiwabo wakipongezana mara baada ya kukamilisha zoezi la kuwekeana saini makubaliano ya ushirikiano yaliyofikiwa katika kikao cha Tume ya pamoja ya kudumu ya Ushirikiano baina ya serikali ya Tanzania na Rwanda, kilichofanyika mwishoni mwa mwezi April. 
Uwekaji saini ni moja ya shughuli zilizoshuhudiwa na Wahemiwa Marais wa Tanzania na Rwanda.


Rais Dkt. John Pombe Magufuli ampokea Rais wa Rwanda Mhe.Paul Kagame Nchini


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amempokea Mhe. Paul Kagame Rais wa Jamhuri ya Rwanda kwa ziara rasmi ya kiserikali. Rais Magufuli ameambatana na Mkewe Mama Janeth Magufuli na Rais Kagame ameambatana na mkewe Mama Jeannette Kagame. Ziara hii ni ya siku mbili.Baada ya Hapo ataelekea Ikulu jijini Dar es Salaam kwa ajili ya Kufanya Mazungumzo.

Baada ya hapo wataelekea katika Viwanja vya Maonesho ya Kimataifa ya Sabasaba jijini Dar es Salaam kwa ajili ya ufunguzi rasmi ya maonesho ya 40 ya Kimataifa katika viwanja vya Sabasaba  leo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli aakiwa ameambatana na mgeni wake Mhe. Paul Kagame Rais wa Jamhuri ya Rwanda mara baada ya kuwasili asubuhi hii katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere kwa ziara rasmi ya siku mbili ya kiserikali. Rais Magufuli ameambatana na Mkewe Mama Janeth Magufuli na Rais Kagame ameambatana na mkewe Mama Jeannette Kagame.  

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na mgeni wake Mhe. Paul Kagame Rais wa Jamhuri ya Rwanda wakipata Gwaride la heshima uwanjani hapo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli pamoja na mgeni wake Mhe. Paul Kagame Rais wa Jamhuri ya Rwanda wakitazama kikundi cha ngoma za asili kilichokuwa kikitumbuiza uwanjani hapo.

Rais Paul Kagame akiwapungi mkono baadhi ya wananchi mbalimbali waliofika kumlaki uwanjani hapo,kushoto kwake ni  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli .