Friday, July 1, 2016

Rais Dkt. John Pombe Magufuli ampokea Rais wa Jamhuri ya Rwanda Mhe.Paul Kagame

 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na  Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam. Mhe. Paul Kagame yupo nchini kwa ziara ya siku mbili kuanzia leo, ambapo anatarajiwa kufungua Maonyesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa ya Sabasaba yanayofanyika jijini Dar es Salaam 
 Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame akiwa na mkewe mama  Jeannette Kagame wakipokea zawadi ya maua mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na mgeni wake Mhe. Paul Kagame mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege jijini Dar es Salaam.


Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame akikagua gwaride la heshima mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege. 
Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame akiwa na mwenyeji wake, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege jijini Dar es Salaam.
 Waheshimiwa Marais wa Tanzania na Rwanda wakiangalia vikundi vya ngoma vilivyokuwa vikitumbuiza katika uwanja wa ndege.
 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mgeni wake wakisalimia wananchi waliofika viwanja vya Ikulu  kumlaki mgeni mara baada ya kuwasili.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli (wa sita kulia), akiwa katika Mkutano na Mgeni wake Mhe. Rais Paul Kagame pamoja na viongozi waandamizi wa Serikali wa pande zote mbili.
 Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame akizungumza na Wanahabari mara baada ya kumaliza mazungumzo na Mhe. Rais Dkt. Magufuli.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na wanahabari mara baada ya kumaliza mazungumzo na Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame.

Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb)(kushoto) na  Rwanda Mhe. Louise Mushikiwabo wakipongezana mara baada ya kukamilisha zoezi la kuwekeana saini makubaliano ya ushirikiano yaliyofikiwa katika kikao cha Tume ya pamoja ya kudumu ya Ushirikiano baina ya serikali ya Tanzania na Rwanda, kilichofanyika mwishoni mwa mwezi April. 
Uwekaji saini ni moja ya shughuli zilizoshuhudiwa na Wahemiwa Marais wa Tanzania na Rwanda.


No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.