Wednesday, July 27, 2016

Tanzania na Korea Kusini kuimarisha ushirikiano

Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mbelwa Kairuki (katikati) akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa masuala ya Afrika na Mashariki ya Kati wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Korea Kusini, Bw. KWON Hee-seog (hayupo pichani). Mazungumzo hayo rasmi ambayo yalijikita katika kujadili masuala ya ushirikiano baina ya Tanzania na Korea Kusini yalifanyika katika Ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam tarehe 26 Julai, 2016. Wengine katika picha ni Maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia mazungumzo.
Mkurugenzi wa masuala ya Afrika na Mashariki ya Kati kutoka Wizara ya Mambo ya Nje ya Korea Kusini, Bw. Kwon Hee-seog (kulia) akizungumza ambapo alieleza nia ya Serikali ya Korea katika kuendelea kuimarisha ushirikiano na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania hususan katika sekta ya elimu, biashara, uwekezaji na masuala ya utamaduni. Kushoto ni Mkurugenzi Msaidizi masuala ya Mashariki ya Kati wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Korea ni Bw. JO Joosung.
Bw. Kwon Hee- seog akiwa pamoja na wajumbe aliofuatana nao wakifuatilia mazungumzo.
Mkutano ukiendelea

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.