Tuesday, July 12, 2016

Balozi wa Tanzania nchini Kuwait akutana na Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Maendeleo wa nchi hiyo

Balozi wa Tanzania nchini Kuwait, Mhe. Dkt. Mahdhi Juma Maalim akiwa katika picha ya pamoja na Bw. Abdulwahab Al-Bader, Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Maendeleo wa Kuwait-Kuwait Fund for Arab Economic Development (KFAED). Mhe. Dkt. Maalim alikutana na kufanya mazungumzo na Bw. Al-Bader ambapo walijadili masuala muhimu katika kuharakisha utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maedneleo ambayo inasubiri ufadhili wa mfuko huo. Aidha, Balozi Maalim alisifu mchango mkubwa wa KFAED katika kufanikisha miradi mbalimbali ya maendeleo nchini Tanzania na kumwahidi  Mkurugenzi huyo kuendelea kutoa ushirikiano wa kutosha katika juhudi za kuimarisha zaidi mahusiano kati ya Tanzania na Kuwait hususan KFAED.
Balozi Dkt. Maalim akiwa na Mkurugenzi Mkuu, Bw. Al-Bader pamoja na baadhi ya Maafisa wa KFAED.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.