Saturday, July 2, 2016

Rais Magufuli na Kagame washiriki dhifa ya Kitaifa

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, akitakiana afya njema na ushirikiano ulio imara na Mgeni wake Rais wa Jamhuri ya Rwanda, Mhe. Paul Kagame kwenye dhifa ya kitaifa,iliyofanyika Jijijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu, Wenza wa Marais Mama Janeth Magufuli na Mama Jeannette Kagame, Rais Mstaafu wa awamu ya pili Mhe. Ali Hassan Mwinyi na viongozi wengine wakuu wa Serikali.  
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli, Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu (wa kwanza kulia) na Mke wa Rais wa Jamhuri ya Rwanda mama Jeannette Kagame(wa kwanza kushoto) wakiwa wamesimama wakati nyimbo za taifa zikipigwa 
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Augustine Mahiga (Mb) (katikati), Waziri wa Mambo ya Nje wa Rwanda Mhe. Loiuse Mushikiwabo (wa kwanza kulia) na Jaji Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Othmani Chande nao wakiwa wamesimama wakati nyimbo za taifa zikipigwa
Mhe. Rais Magufuli akizungumza kwenye Dhifa ya kitaifa ambapo alimshukuru Mhe.Rais Kagame kwa kuitikia mwaliko wake na Kufungua maonyesho ya 40 ya Kimataifa ya Biashara (Sabasaba).
Mhe. Rais Kagame naye akizungumza katika Dhifa hiyo ambapo alimshukuru mwenyeji wake Mhe. Magufuli kwa mapokezi na kuahidi kuendeleza mahusiano mazuri yaliyopo kati ya Tanzania na Rwanda yaliyodumu kwa muda mrefu.
Sehemu ya Viongozi wa Serikali waliohudhuria hafla hiyo wakifuatilia kwa makini hotuba zilizokuwa zikitolewa na Waheshimiwa Marais.
Sehemu nyingine ya viongozi wa Serikali waliohudhuria Hafla hiyo wakifuatilia hotuba zilizokuwa zikitolewa na Waheshimiwa Marais
Balozi wa China nchini Tanzania (wa pili kulia) na Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Bw. Alvaro Rodriguez (wa kwanza kushoto) pamoja na maafisa kutoka Ubalozi wa China hapa nchini pia walishiriki katika hafla hiyo.  
Rais Magufuli akisalimiana na Waziri Mkuu Mstaafu Mhe. Jaji Sinde Warioba na Rais Kagame akisaliamiana na Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Ackson Tulia.
Rais Kagame akisalimiana na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt.Susan Kolimba(Mb)

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.