Tuesday, July 26, 2016

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje awa mgeni rasmi siku ya Taifa la Misri

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Susan Kolimba akitoa hotuba kama mgeni rasmi wakati wa maadhimisho ya Siku ya Taifa la Misri yaliyofanyika Jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Katika hotuba yake Mhe. Dkt. Kolimba alisifu ushirikiano uliopo kati ya Tanzania na Misri na kuahidi kuendelea kuuimarisha kwa ajili ya manufaa ya wananchi wa mataifa haya.

Sehemu ya Mabalozi wanaowakilisha nchi zao nchini wakimsikiliza Mhe. Dkt. Kolimba (hayupo kwenye picha) kwenye maadhimisho ya siku ya Taifa la Misri
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Suzan Kolimba akitakiana afya njema na Balozi wa Misri nchini, Mhe. Yasser Ahmed Al Eldin Elshawaf wakati wa maadhimisho ya Taifa la Misri yaliyofanyika hivi karibuni Jijini Dar es Salaam.

Sehemu ya wageni waalikwa akiwemo Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani, Balozi Simba Yahya (wa tatu kutoka kushoto), Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samwel Shelukindo (wa pili kushoto), Msaidizi wa Naibu Waziri, Bw. Adam Isara (kushoto)  na Maafisa wa Ubalozi wa Misri (k
Sehemu ya Wageni waalikwa


   

Balozi wa Misri nchini pamoja na mkewe wakimkaribisha Rais Mstaafu, Mhe. Ali Hassan Mwinyi kwenye maadhimisho ya Taifa la Misri
Meza kuu wakifurahia burudani kutoka kwa mtumbuizaji ambaye ni raia wa Misri anayeishi hapa nchini
Picha ya pamoja
Maafisa wa Ubalozi wa Misri wakiagana na Mhe. Mwinyi
Mhe. Dkt. Susan akiagana na Balozi wa Misri mara baada ya maadhimisho ya Taifa hilo
Balozi Yahya na Balozi Shelukindo wakiwa na mmoja wa wageni waalikwa
Picha ya pamoja

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.