Friday, July 29, 2016

Waziri Mahiga akutana na Balozi wa Saharawi nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga akimkaribisha Balozi wa Saharawi nchini Mhe. Brahim Salem Buseif alipomtembea katika ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam na kufanya naye mazungumzo tarehe 29 Julai, 2016
Mhe. Waziri Mahiga akizungumza na Mhe. Buseif, ambapo katika mazumgumzo yao alimpa pole kwa  msiba wa aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama Tawala cha Polisario cha nchini Saharawi. Pia alisisitiza kuwa mataifa haya mawili yataendelea kuimarisha ushirikiano katika masuala mbalimbali.
Mhe. Buseif akizungumza ambapo alieleza kuwa nchi ya Saharawi ipo tayari kushirikiana na Tanzania na kuishukuru kwa kuiunga mkono katika masuala mbalimbali.
Mkurugenzi wa Idara ya Afrika katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Samuel Shelukindo pamoja na Afisa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakifuatilia mazungumzo.
Mazungumzo yakiendelea.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.