Friday, July 8, 2016

WAZIRI MAHIGA AZUNGUMZIA ZIARA WA WAZIRI MKUU WA INDIA NCHINI


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga (kushoto) akizungumza katika Mkutano na wanahabari kuhusu ziara ya Waziri Mkuu wa India Mhe. Narendra Modi anayetarajiwa kuwasili nchini kwa ziara ya siku mbili kuanzia tarehe 9-10 Julai, 2016. Mkutano huo ulifanyika leo katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam. Katikati ni Naibu Waziri  wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Susan Kolimba na Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Balozi Dkt. Aziz P. Mlima. 
Mstari wa mbele ni baadhi ya Mabalozi na Wakurugenzi kutoka Wizarani wakifuatilia Mkutano 

Katibu Mkuu Balozi Dkt. Aziz P. Mlima (katikati) akifafanua jambo wakati wa Mkutano na wanaandishi wa habari uliofanyika katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam. 
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali na Msemaji wa Wizara Bi. Mindi Kisiga akifafanua jambo kwenye Mkutano na Wanahabari.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda (wapili kushoto) akitoa maelekezo juu ya masuala mbalimbali kuhusu ziara ya Waziri Mkuu wa India Nchini Mhe. Narendra Modi wakati wa Mkutano na Wanahabari uliofanyika katika Ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Jijini Dar es Salaam Julai.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.