Thursday, July 21, 2016

Waziri Mahiga akutana na Balozi wa Iran nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akizungumza na Balozi wa Iran nchini Mhe. Mehdi Agha Jafari alipomtembelea leo katika Ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam. Katika Mazungumzo yao Mhe. Waziri alimweleza  Balozi huyo kuwa Serikali ya Tanzania itaendelea kudumisha ushirikiano na Iran  hususan katika kuhakikisha Diplomasia ya uchumi baina ya mataifa hayo inaimarika kwa manufaa ya mataifa hayo. 
Mhe. Balozi Mehdi Agha Jafari akizungumza ambapo alieleza kuwa Serikali ya Iran itazidi kushirikiana na Tanzania katika sekta za Elimu, Biashara, Afya na Kilimo.
Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati Balozi Abdallah Kilima (kushoto) pamoja na Msaidizi wa Waziri, Bw. Adolf Mchemwa wakifuatilia kwa makini mazungumzo.
Mhe. Balozi Mehdi Agha Jafari akimkabidhi ujumbe maalum Mhe. Waziri Mahiga 
Mazungumzo yakiendelea

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.