Wednesday, July 20, 2016

Waziri Mahiga azungumza na Waandishi wa Habari kuhusu mkutano wa AU

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari mapema leo mchana kuhusu Mkutano wa Wakuu wa Nchi wa Umoja wa Afrika uliomalizika hivi karibuni nchini Rwanda. Katika mkutano huo Mhe. Waziri alielezea mambo mbalimbali yaliyojadiliwa katika Mkutano huo ikiwemo suala zima la Haki za Wanawake katika kufanya maamuzi, kupata nafasi za Uongozi na kushirikishwa kwenye utatuzi wa migogoro mbalimbali Barani Afrika. Kaulimbiu ya mkutano huo ilihusu "Haki za binadamu hususan za Wanawake".  Kulia ni Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Serikali Wizarani, Bi. Mindi Kasiga.
Dkt. Mahiga akionyesha kwa waandishi wa habari Hati yake ya Kusafiria (passport) aliyopatiwa wakati wa mkutano wa AU. Hati hiyo imeanzishwa na Umoja wa Afrika kwa lengo la kuimarisha umoja na kurahisisha mawasiliano. Kulia  ni Bi. Kasiga.
Waandishi wa Habari wakimsikiliza Waziri Mahiga kwenye mkutano uliowakutanisha naye.


Picha na Reginald Philip

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.