Friday, July 29, 2016

Mtanzania atunukiwa Tuzo ya Juu ya Malkia wa Thailand

Profesa Pauline Peter Mella aliyetunukiwa Tuzo ya Juu ya Malkia wa Thailand Srinagarindra kwa kutambua mchango wake kwenye sekta ya afya, akizungumza wakati wa hafla fupi ya kumpongeza iliyoandaliwa na Ubalozi wa Thailand nchini kwa kushirikiana na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki. Tuzo hiyo inatolewa  na Malkia wa Thailand Srinagarindra kwa kutambua mchango wa watu mbalimbali kwenye sekta ya afya. Profesa Mela ambaye kitaaluma ni Muuguzi kwa sasa ni Mkufunzi katika Chuo Kikuu cha masuala ya Tiba cha Hubert Kairuki cha Jijini Dar es Salaam.
Sehemu ya wageni waalikwa wakimsikiliza Profesa Pauline Peter Mella hayupo pichani. Wa pili kutoka kulia ni Balozi Mteule wa Thailand nchini, Mhe. Prasittiporn Wetprasit
Profesa Pauline Peter Mella akiwa ameshikilia Tuzo yake kwenye picha ya pamoja na Balozi Mteule wa Thailand hapa nchini mwenye makazi yake nchini Nairobi Mhe. Prasittiporn Wetprasit na familia yake.

Profesa Mella akiwa katika picha ya pamoja na wageni waalikwa

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.