Saturday, July 2, 2016

Rais Kagame afungua maonyesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa

Rais Paul Kagame akihutubia katika halfa ya ufunguzi wa Maonyesho ya Biashara ya Kimataifa yanayofanyika katika Viwanja vya Mwl. Julius Nyerere (Sabasaba) jijini Dar es Salaam, ambapo alikuwa mgei rasmi katika maonyesho hayo.
Sehemu ya viongozi wa Serikali, Mabalozi, wawakilishi wa Mashirika ya Kimataifa nchini na wafanyabishara kutoka mataifa mbalimbali walioshiriki katika maonyesho hayo wakifuatilia hafla ya ufunguzi.
Mratibu Mkazi wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez akipokea zawadi kutoka kwa Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame, pembeni akishuhudiwa na Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli (wa kwanza kulia) wakati wa ufunguzi wa Maonyesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa.
Wageni mbalimbali waliohudhuria hafla hiyo wakishangilia kwa kupiga makofi wakati Mhe. Rais Kagame akitoa Zawadi kwa washindi mbalimbali waliohudhuria katika maonyesho ya Biashara ya Kimataifa
Rais Kagame akibonyeza Kitufe maalumu kilichoandaliwa kuashiria ufunguzi rasmi wa maonyesho ya Biashara ya Kimataifa ya Sabasaba 
Mhe.Rais Kagame na Mwenyeji wake Mhe. Rais Magufuli wakitembelea Mabanda yaliyopo katika viwanja hivyo vya sabasaba na kujionea thamani mbalimbali zikiwemo vitanda vilivyotengenezwa kwa mbao zitokanazo na mti wa Mnazi
Kaimu Mkuu wa Itifaki wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. James Bwana(wa kwanza kushoto) akiwa pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mhe. Paul Makonda, kushoto kwao ni Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bw. Joseph Mwasota 
Rais Kagame akisalimiana na Mtoto aliyejitokeza katika maonyesho hayo katika viwanja vya sabasaba.
Mama Janeth Magufuli na Mgeni wake Mama Jeannette Kagame nao wakiendelea kutembelea mabanda yaliyokuwepo katika viwanja hivyo vya sabasaba

Kutoka kushoto ni Msaidizi wa Rais - Hotuba Bw. Bujiku Sakila akiwa pamoja na Maafisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Bw. Batholomeo Jungu na Bw. John Pangipita

 

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.