Friday, July 29, 2016

Waziri Mahiga apokea Nakala za Hati za Utambulisho za Mabalozi Wateule nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Augustine Mahiga (Mb.), akipokea Nakala za Hati za Utambulisho za Balozi Mteule wa Italia hapa nchini, Mhe. Roberto Mengon. Hafla hiyo ilifanyika katika Ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam hivi karibuni.
Waziri Mahiga akizungumza na Balozi Mteule wa Italia hapa nchini mara baada ya kupokea Nakala zake za utambulisho. Wengine katika picha ni Mkurugenzi wa Idara ya Amerika na Ulaya Balozi Joseph Sokoine akifuatiwa na  Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Itifaki, Bw. James Bwana .

...Nakala za Hati za Balozi wa Jamhuri ya Watu wa Korea

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb.), pia akipokea Nakala za Hati za Utambulisho za Balozi Mteule wa Jamhuri ya Watu wa Korea (DPRK) hapa nchini, Balozi Kim Yong Su hafla iliyofanyika katika Ofisi za Wizara Jijini Dar es Salaam hivi karibuni

...Nakala za Utambulisho za Balozi wa Thailand

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Dkt. Augustine Mahiga (Mb.), amepokea Nakala za Hati za Utambulisho za Balozi Mpya wa Thailand hapa nchini mwenye makazi yake nchini Nairobi Balozi Prasittiporn Wetprasit (kushoto) leo katika Ofisi yake jijini Dar es Salaam
Waziri Mahiga akimweleza jambo Balozi Mteule, Mhe. Wetprasit mara baada ya kupokea nakala zake za utambulisho.

...Nakala za Hati za Utambulisho za Balozi wa Somalia

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Augustine Mahiga (Mb.), akiisoma Nakala ya Hati ya  Utambulisho  ya a Balozi Mpya wa Jamhuri ya Somalia hapa nchini Balozi Mteule wa Somalia nchini, Mhe. Mohammed Hassan Abdi mara baada ya kuipokea. Tukio hilo lilifanyika Wizarani hivi karibuni.
Dkt. Mahiga akizungumza na Balozi Mohammed Hassan Abdi mara baada ya kupokea nakala zake
Waziri Mahiga akiwa katika picha ya pamoja na Balozi Hassan Abdi

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.