Tuesday, July 19, 2016

Taasisi ya Aga Khan kuendelea kushirikiana na Tanzania katika miradi ya maendeleo

Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Ramadhani Muombwa Mwinyi (kulia) akizungumza na Mkurugenzi wa masuala ya Kidiplomasia katika Taasisi ya Aga Khan, Balozi Arif Lalani alipotembelea Wizarani kwa ajili ya kujitambulisha na kueleza nia ya Taasisi hiyo ya kuendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika miradi ya maendeleo hususan katika sekta ya elimu na afya.
Sehemu ya wageni walioambatana na Balozi Lalani (hayupo pichani). Kulia ni Mwakilishi Mkazi wa Taasisi ya Aga Khan nchini, Bw. Amin Kurji nao wakisikiliza mazungumzo kati ya Balozi Muombwa na Balozi Lalani (hawapo pichani).
Balozi Lalani naye akizungumza na Balozi Mwinyi  alipotembelea Wizarani.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa Bi. Ramla Khamis (kushoto), pamoja na Afisa Mambo ya Nje na UShirikiano wa Afrika Mashariki, Bi. Hellen Mgeta wakifuatilia mazungumzo.
Mazungumzo yakiendelea
Balozi Mwinyi akiagana na  Balozi Lalani na Bw. Kurji  mara baada ya kumaliza mazungumzo.

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.