Friday, July 29, 2016

Waziri Mahiga akutana na Balozi wa DRC nchini

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt Augustine Mahiga akizungumza na Balozi wa Jamhuri ya Demokrasia ya Congo (DRC) Mhe. Jean Pierre Tshampanga Mutamba, alipomtembelea Wizarani Jijiji Dar es Salaam. Katika Mazungumzo yao Mhe Waziri alieleza Serikali ya Tanzania inafanya jitihada za makusudi kuhakikisha wafanyabiashara kutoka nchini Congo hawapati shida katika kusafirisha bidhaa zao kupitia Bandari ya Dar es Salaam.
Mhe. Mutamba akizungumza ambapo alieleza umuhimu wa kufanyika vikao vya Tume ya Pamoja kati ya Tanzania na DRC, pamoja na kuweka makubaliano yatakayowezesha wafanyabiashara kunufaika na kuweza kukuza uchumi wa mataifa yao badala ya kuwa na tozo nyingi zinazorudisha nyuma biashara zao.
Wakati mazungumzo yakiendelea
Waziri Mahiga akiagana na Mhe. Balozi Mutamba

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.