Thursday, July 21, 2016

KATIBU MKUU AKUTANA NA MKURUGENZI MKAZI WA SHIRIKA LA TRADEMARK EAST AFRIKA

Mkurugenzi wa Shirika la TradeMark East Afrika (TMEA) Bw. John Ulanga (kushoto) akizungumza na Katibu Mkuu Balozi Dkt. Aziz P. Mlima (kulia) alipotembelea Wizarani leo. Bw. John Ulanga amechukua nafasi iliyoachwa wazi na aliyekuwa Mkurugenzi wa Shirika hilo Dkt. Josaphat Kweka baada ya kumaliza mkataba wake wa kulitumikia shirika. Katika mazungumzo hayo Mkurugenzi mpya wa shikirika la TradeMark East Afrika Bw. John Ulanga  aliahidi kudumisha na kukuza ushirikiano na serikali katika kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo Nchini.
Katibu Mkuu Balozi Dkt. Aziz P. Mlima (wa pili kushoto) akimsikiliza Mkurugenzi mpya wa Shirika la TradeMark East Afrika Bw. John Ulanga (kushoto). Wengine ni Kaimu Mkurugenzi wa Sera na Mipango Bw. Osward Kyamani (kulia) na Mkurugenzi wa Biashara, Uwekezaji na Sekta za Uzalishaji Bw. Bernard Haule (wapili kulia)
Katibu Mkuu Balozi Dkt. Aziz P. Mlima na Mkurugenzi Mkazi wa Shirika la TradeMark East Afrika wakiendelea na mazungumzo. Tokea kushoto ni Afisa Uchumi kutoka Wizarani na Mratibu wa maratibu wa mradi wa TMEA  Bi. Joyce (wakwanza kushoto) Kimei na Afisa kutoka TMEA Bi. Monika Hangi (wapili kushoto)
Mkurugenzi wa TMEA Bw. John Ulanga akielezea jambo kwa Katibu Mkuu Balozi Dkt. Aziz P. Mlima

No comments:

Post a Comment

Note: Only a member of this blog may post a comment.